Tested HIV positive, looking for a soul mate

sielewi kwa nini watu wanakupa pole!! wewe ni shujaa. Hongera sana mkuu Pave kwa kuwa muwazi. Mungu akupe hitajio lako. mzae na watoto.

Unahitaji pongezi, wote wanamudu ujasiri wa namna hii. Hongera mkuu umekuwa wa kipekee katika hili. Mungu akusaidie upate hitaji lako na zaidi akupe ujasiri zaidi!

Pamoja wakuu! Mungu asikie maombi yenu. Natambua (kwa namna zangu) thamani ya kuwepo kwangu duniani...... ni vizuri kubadilika kwa haraka na kuendana na hali....... ni jambo zuri kupenda na kujali wengine. Ni vyema kujenga furaha maishani kuliko kujenga huzuni kwako na kwa wengine.
 
Umenikumbusha jamani kuna mtu mmoja nlimsave soul mate!
 
Umenikumbusha jamani kuna pakashume mmoja nlimsave soul mate!

Paka shume tena:what:....from soul mate to Paka shume jamani..

Pole Dada yangu najua ali ku disappoint sana mpaka wamwita Paka shume toka soulmate Kwel....

Mimi mbona sipati wa kuniita hivyo jamani at least na mimi nijione nimo kwa wanaopendwa....Duuh mi ndio mpendaji tuuu....
 

Wee acha tu yani! Pole wee utapata tu
 
Kama ni kweli basi naamini nami itakuwa hivyo, nitakuja

Lakini uwe mwangalifu sana usije ukatapeliwa. Maana makanisa mengi wanatafuta watoa sadaka. Wanaweza kukufilisi kwa kutake advantage ya tatizo lako na baadae kukuacha katika hali mbaya zaidi. Uwe na taadhari kubwa na utumie akili zako vyema.
 
Lakini uwe mwangalifu sana usije ukatapeliwa. Maana makanisa mengi wanatafuta watoa sadaka. Wanaweza kukufilisi kwa kutake advantage ya tatizo lako na baadae kukuacha katika hali mbaya zaidi. Uwe na taadhari kubwa na utumie akili zako vyema.

Ahsante sana. Changamoto za kiimani katika maswala ya tiba kias flan nazitambua kwa dini mbalimbali tukiwemo waislamu.

Mazingira ya kutegemea muujiza utendeke yanahitaji umakini sana. Naita muujiza maana nijuavyo dawa bado hakuna, na tunaambiwa 'viral diseases has no cure'.... loh! Akili kumkichwa maisha yaendelee 'positively'
Shukran!
 
Je ulikuwa kwenye mahusiano wakati unapima --just curious if you cared to hint your x? and kitu gani kilifanya upime , uliugua au routine checkup?

Mkuu siku hizi na madawa na vyakula unaweza kuishi miaka mingi sana 20+ so take it as a small challenge ila ukiwa mentally free u will win this battle. Hongera kwa uwazi.
 
Najaribu kujiweka kwenye viatu vyako, kwa kweli wewe ni jasiri. Kila kitu hutokea kwa makusudi maalum. Mungu aendelee kukuimarisha na akupatie haja ya moyo wako. Pole sn

Siamini kupata maambuki ni makusudi maalumu. Kama ni maalumu ni ya Mungu au vinginevyo?
 

Mungu akupe nguvu kaka na naamini utampata mwanamke bora
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…