Mkuu hii ni siku ya ngapi tangu vurugu hizo zitokee, kwa nini imemchukua muda mrefu kukemea mambo ambayo yanalitia Taifa letu aibu kubwa kimataifa - yeye kama mdhamini wa vyama kwa nini hakuwaita siku ya tukio na kuwapa karipio kali. Mpaka sasa hivi nimelitunza gazeti la mwananchi linalo onyesha vizuri watu wazima/wamakamo wamebeba matofali ya kujengea nyumba na wawe wakipania kumuua mtanzania mwenzao - kisa kasimika bendera sijui wapi, mambo ya kitoto kabisa na hatarishi!!
Swala hili wangeweza kuelewana tu, au kutumia vyombo vya DORA kwa kuwakalisha chini wakaelewana - haya mambo ya kujichukulia sheria mkononi tunawafundisha nini raia baki - ukija na matra ya kusema Taifa letu ni la amani na utulivu nani atakuelewa??