Tendwa aionya tena CHADEMA...

Tendwa aionya tena CHADEMA...

You know what is insernity...

Naona ameanza kuongeza maneno mengine kisha kujitafutia hukumu. This guy has completely lost any moral authority, if at all he ever had before. Matokeo yake, hata ofisi yake yote itaanza kutafsirika kama alivyo yeye mwenyewe.

Tamko la CHADEMA lililotokana na maazimio ya Kamati Kuu, lilisema hivi;


4:0. Uchaguzi wa Madiwani.

Kamati Kuu imepokea taarifa kuhusu ushiriki wa CHADEMA katika Uchaguzi wa Madiwani uliofanyika tarehe 16/06/2013 katika kata 22.

 Kamati Kuu imeipongeza Sekretarieti na uongozi wa Kanda mbalimbali za CHADEMA kwa maandalizi mazuri katika Uchagzuzi huo uliosababisha CHADEMA kuwapokonya CCM ushindi katika kata 4 ilizokuwa imeshinda katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010. Kamati Kuu imewapongeza wananchi kwa kuipatia CHADEMA kura asilimia (47.7%) dhidi ya CCM (49%) na (3.3%) za CUF.

 Kamati kuu imesikitishwa na vitendo vya fujo walivyofanyiwa viongozi, wagombea pamoja na Wanachama mbalimbali katika sehemu mbalimbali palipo fanyika Uchaguzi. Kamati Kuu imesikitshwa na kulaani vitendo hivyo vikiwemo vya watu kukatwa mapanga , kuchomwa visu na kubakwa kwa akina Mama na vijana wahuni walioandaliwa na Chama cha Mapinduzi
 Kamati Kuu imelaani vitendo hivyo vya kinyama vilivyofanywa mbele ya jeshi la polisi na Wakuu wa Wilaya.

 Ili kukabiliana na vitendo vya fujo vinavyofanywa na vijana wa CCM dhidi ya wagombea, Wanachama na viongozi wa CHADEMA, Kamati Kuu imeagiza kwamba kitengo cha ulinzi cha Chama “Red Brigade” kiimarishwe zaidi kwa kuhakikisha kuwa vijana wote wa Red Brigade Nchi nzima wanapewa mafunzo maalum ya UKAKAMAVU yatakayoandaliwa katika Makambi maalum katika mikoa yote.

@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@@

Aya ya mwisho hapo kwenye tamko, ndiyo inayowahangaisha.

Sasa unaweza kulinganisha na hicho kinachosemwa kwenye tamko eti la ofisi ya msajili wa vyama. Baada ya ushahidi mfululizo kutolewa na kuibana serikali, ofisa wa dawati la propaganda nje ya Lumumb! amekurupushwa tena kuja kuropoka lolote.

Ofisi zingine za umma zinadhalilishwa sana.

Halaf matamko meng yanasainiwa kwa niaba yake cjawah ona sain ya tendwa.
 
Amesema kuwa CHADEMA wanaruhusiwa kuanzisha vikundi vya kujilinda lakini hawaruhusiwi kuanzisha mafunzo ya kutumia nguvu kwaajili ya kujilinda kama walivyo tangaza katika mikutano yao ya hadhara kwani ni kinyume na Demokrasia na Katiba ya Jamuhuri ya Muungano. Sasa tunauliza, Je, upi ni msimamo wake juu ya uamuzi waliotangaza CHADEMA kwani anakubali hapo hapo anawakataza. Pia ni nguvu ipi iliyotumika hapo mpaka aone kama hiyo nguvu ni tishio kiasi hicho, au alitaka ifanyike chini ya kapeti kama ya magamba? akumbuke kuwa CDM ni chama cha demokrasia hivyo mambo yake huwa wazi wazi bila kificho.
Mbona huyu Babu hasomeki. Tiririka mdau unayeipenda Tanzania.
 
Vijana hebu muwe na huruma na huyu Kikongwe , kwa umri wake hastahili hata kuvuta sigara yenye kichungi bali anastahili KIKO .

Mhurumieni inawezekana ana matatizo ya kifamilia ambayo yanaathiri utendaji wake pamoja na reasoning capacity yake.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Tendwa anafanya kazi kwa mkataba, Kwa kuwa yupo pale kwa mkataba, amekosa sifa za kisheria kusajiri au kufuta chama chochote cha siasa

Kisheria Tendwa anatakiwa Kuwa ameshastaafu utumishi, Tena siyo kustaafu tu , ni kustaafu utumishi USIOTUKUKA,

Hivyo basi mtu anapofikia hatua ya kustaafu maana yake Mwili pamoja na Akili huwa vimechoka, japo wengine huchoka akili zaidi kuliko Mwili watu hawa ni hatari sana ktkt jamii.

Mcha Mungu anapofikia hatua Hiyo huamua kupumzika kwa heshima badala ya kun'gan'gania usichoweza mwishowe unaweza kusababisha maafa mkubwa ktk nchi.

Nasckia sasa anafanya kazi kwa mkataba pengine wanataka aivushe ccm kwanza 2015 ndo aondoke salama.

Utu wa MTZ sasa umedhihakiwa hadi hatua ya mwisho police wameambiwa wapige tu badala ya kukamata na kupeleka Mbele ya Sheria.

CHADEMA wapoamua sasa ni heri na bora wakajilinda wenyewe coz jeshi halina msaada tena Kwao anaibuka mtu mchovu na kusema jilinde lakini usitumie Nguvu. Wendawazimu huu! Nini maana ya kujilinda bila kutumia Nguvu. Msaada Jamani.
 
Hiyo yote ni Aibu.
Ukweli ni kwamba hoja ya cdm imepita bila kupingwa.

Chadema ni Kisiki cha Mpingo.
 
Kujilinda bila kutumia nguvu ndo kujilinda vipi tena...? Maana ukitaka usitumie nguvu sana...inabidi utumie bunduki.. au
 
Nasubiri siku Tendwa atakapoipongeza Chadema ndipo nami nitatoa dukuduku langu kwa Tendwa
 
Pamoja na mapenzi ya tendwa kwa ccm, lakini pia tukumbuke huyu jamaa anakaribia kustaafu na anamatarajio ya kuteuliwa katika wadhifa fulani ndio maana ameamua kujitoa ufahamu na kutoa kauli zinazo gongana na kumuaibisha yeye na aliye mteua kuwa msajili.....MAJANGA!
 
Chadema haifi tena. Wasira

Chadema inachanja mbuga. S. Simba

Chadema kisiki cha mpingo. Mrema

Chadema ni wajanja sana. Ole medeye.

Chadema ni watani wetu. Nape

Chadema wanatukaba koo ila tumeshinda. Mwigulu.

Kinachotukera ccm na Tendwa ni
Kauli hizi

Pipoz powa

Tulianza na Mungu Tunamaliza na Mungu

Kula ccm Kura chadema

Wao wana pesa sisi tuna Mungu

Ccmkwa Mafisadi cdm kwa Wanyonge.

Hakuna kulala mpaka kieleweke

Ukipiga kura rudi hatua 103 nyuma linda kura yako.

Ccm Analogia cdm digitali

Hakuna dhambi kubwa kama WOGA.
 
Vijana hebu muwe na huruma na huyu Kikongwe , kwa umri wake hastahili hata kuvuta sigara yenye kichungi bali anastahili KIKO .

Wazee si wamekwisha kustaafu? Yeye anasubiri nini?
 
Namini kuwa tendwa keshatendwa na sasa anfikiri kwa kutumia ma------.
 
Nchi GANI DUNIANI VIONGOZI wa kuandikisha VYAMA wana NGUVU zaidi ya Wabunge... NCHI YETU CCM inawapa NGUVU yoyote atakayeipa MCHECHETO CHADEMA

Hiyo ni moja kati ya ishara ya kushindwa kwa serikali husika
 
Hapa mimi nimechoka kabisa. Msajiri anasema vyama vinaruhusiwa kuanzisha vikundi ila visitumie nguvu kujilinda bali wajibu wao ni kutoa taarifa. Kuna haja ya kuwa na kikundi kwa ajiri ya taarifa tu?

Nao ccm wanatoa taarifa ama wanafanya kusulubu kama walivyoagizo polic?
 
Back
Top Bottom