Tendwa aionya tena CHADEMA...

Tendwa aionya tena CHADEMA...

Mzee wa watu lazima ajikombe kwa maccm,vinginevyo watasitisha mkataba wake wa kibarua maana muda wake umekwisha.Tanzania ya leo hata kama umesoma ili maccm yakupenda lazima uwe mnafiki kama maccm.
 
Ameshikwa pabaya anaweweseka kwani anaona giza mbele ktk maisha yake yanayoelekea kukoma siku za karibuni hapa duniani.ROHO YA MAREHEMU MTARAJIWA JONI WA KUTENDWA IPATE REHEMA KWA SHETANI IPUMZIKE KWA MISUKOSUKO.
 
Na Jennifer Chamila, MAELEZO

Msajili wa vyama vya Siasa nchini amewaasa wanachama na viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutumia muda wao kufanya shughuli za siasa ili kuchangia maendeleo ya nchi badala ya kutumia uwezo na muda wao kubuni mambo yanayoleta mtafaruku na kuhatarisha amani ya nchi.

Pia amepinga tamko la chama hicho la kuanzisha mafunzo ya kujilinda kwa vijana wake nchi nzima.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo jijini Dar es Salaam na kusainiwa kwa niaba ya Msajili wa vyama vya siasa Sisty Nyahoza alisema kuwa hajawahi kuruhusu CHADEMA au chama chochote cha siasa kufanya mafunzo ya ukakamavu au mafunzo ya kutumia nguvu ya aina yoyote kwa wanachama wake au mtu yeyote yule.

Anaongeza kuwa CHADEMA wanaruhusiwa kuanzisha vikundi vya kujilinda lakini hawaruhusiwi kuanzisha mafunzo ya kutumia nguvu kwaajili ya kujilinda kama walivyotangaza katika mikutano yao ya hadhara kwani ni kinyume na Demokrasia na Katiba ya Jamuhuri ya Muungano.

Nyahozo ametoa ufafanuzi kuhusu vikundi vya ulinzi na usalama vilivyopo katika Katiba ya Vyama vya Siasa kwamba vikundi hivyo haviruhusiwi kufanya mafunzo ya kutumia nguvu ya aina yoyote katika kutekeleza majukumu yao.

Bali wajibu wao ni kutoa taarifa wa vyombo vya Dola pale wanapo sikia au kuona uhalifu ukitokea na wala sio kupambana na wahalifu au watu wanaotaka kuwadhuru kama tamko la CHADEMA la tarehe 9 mwezi huu linavyo sema.

"Hakuna maelezo yoyote katika Katiba ya CHADEMA yanayoruhusu kutumia nguvu kufanikisha shughuli za kulinda mali na Viongozi wa Chama. Ni vyema wananchi wote waelewe kuwa Sheria za Nchi zimeweka masharti maalumu kwa Vyama Vya Siasa kutokana na umuhimu wa vyama hivi katika kudumisha aman utulivu na umoja wa Kitaifa", alisema Nyahoza.

Alisema kuwa kutokana na Ibara ya20(2)C ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1997 inasema kuwa "Bila kujali masharti ya ibara ya (1) na (4),haitakuwa halali kwa chama chochote cha siasa kuandikishwa ambapo kutokana na katiba au sera yake:-kinakubali au kunapigani matumizi ya nguvu au mapambano kama njia za kufikia malengo yake ya kisiasa.

Nyahoza alimaliza kwa kuwataka CHADEMA kuacha kutekeleza mpango walio tangaza wa kuanzisha makambi ya kufanya mafunzo ya kujilinda kwa vijana wao nchi nzima,kwani kufanya hivyo ni kukiuka sheria za nchi na endapo watashindwa kutii agizo hilo hatua za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

××××××××××××××

NIMEMEPITIA TAMKO LA TENDWA HILO HAPO JUU NA NIKAPATA TAFAKURI IFUATAYO:
1. KUMBE TENDWA ANARUHUSU VIKUNDI VYA KUJILINDA KATIKA VYAMA NA NDIYO MAANA ALISAJILI KATIBA ZA VYAMA INCLUSIVE CHADEMA AMBAYO MSAJILI AMEKUWA AKITOA MATAMKO YASIYO NA TIJA.
2. TENDWA KARUHUSU VIKUNDI HIVI KWA AJILI YA KULINDA VIONGOZI WA CHAMA NA MALI ZA CHAMA,

UJINGA UPO HAPA
A) Tendwa ameshindwa kufafanua nini maana pana ya neno "nguvu" na je utajilinda bila nguvu? na je kama ni vikundi kwa ajili ya kujilinda Chadema walitamka lini kuwa watatumia " nguvu" kujilinda na kuwalinda viongozi wa chama"
Naomba tendwa atoe ufaafaunizi mpana kama mwanasheria juu ya nini maana ya neno "nguvu" (Broader interpretation of the word " nguvu") na je nini tofauti kati ya "ukakamavu" na "nguvu"

Ofisi imepwaya ya msajili kwa hili inadhihirisha namna gani nchi ina viongozi vilaza kama mbunge wa kipindi kile pale temeke.....KIHI......

Nimesoma weeee..... nimekarudiarudia weeee..... naona madudu tu.
 
Wakati mwingine unajiuliza kwa nini watanzania ni mabingwa wa kukwepa kodi....sababu ni matumizi mabaya ya kodi yenyewe kama inavyotumika vibaya ktk ofisi ya huyu mzee.
 
Hiki ni kizazi cha dotcom ukimwaga mboga namwaga ugali na kama ni mbwai mbwai unatakiwa kujitetea mwenyewe kabla ya kutafuta mtetezi wako.hapo busara za babu Tendwa hakuna hata Taifa ambalo halina jeshi ni rahisi kuvamiwa lakini adui anapofahamu kuna jeshi inakuwa vigumu kukuchokoza. Babu acha kutumika na sisiemu
 
Tendwa kama Tendwa ameshaona aibu kuzungumzia mambo ya Red Brigade baada ya kupewa ushahidi wa kujitosheleza juu ya kikundi cha green guard na uharamia wanaoufanya.

Sasa kwakuwa watu wa lumumba ndio wanaoandaa haya matamko na kumpelekea ayasome bila shaka ameona aibu kuendelea kuletewa matamko kutoka lumumba na hivyo ameamua kuwaachia wasaidizi wake kuyatoa kwa niaba ya ofisi yake. Matamko mawili ya mwisho kutoka ofisi ya msajili yametolewa/yamesainiwa na watu wengine/wasaidizi wake. Nadhani ameona aibu kuyasaini yeye kwakuwa aibu inazidi kumuandama yeye na familia yake kwa kukubali kujigeuza kuwa dekio la ccm.


Tendwa amekubali kutumika ndani ya siasa ya ccm acha avue aibu
 
...
Anaongeza kuwa CHADEMA wanaruhusiwa kuanzisha vikundi vya kujilinda lakini hawaruhusiwi kuanzisha mafunzo ya kutumia nguvu kwaajili ya kujilinda kama walivyotangaza katika mikutano yao ya hadhara kwani ni kinyume na Demokrasia na Katiba ya Jamuhuri ya Muungano.....
Wazazi ya zamani nachanganya, walimu dasarani nachanganya, kwa uzushi, na maneno mbofu mbofu! 01-Mr. Ebbo - Maneno Bofu Bofu - YouTube
 
Haha ha bora angekaa kimya tu.Amechanganyikiwa.Haturudi nyuma

Nashauri Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa ialikwe kwenye makambi ya mafunzo kusudi ijiridhishe na yanayoendelea huko.

No research no right to speak. Tendwa anatunga maneno halafu anayatolea matamko. Namna hii hatuwezi kufika

cb
 
Kawaida watu hatuangalii mtu alianzaje bali alimalizaje, huyu mzee anamalizia vibaya uzee wake. Hata -------- hawezi kuwekewa ushahidi wa wazi kama picha na vielelezo mbalimbali jinsi Green Guard wanavyofanya akajifanya havioni na kang'ang'ania mawazo au maoni ambayo hata hayajaanza kufanyiwa kazi!

Pia kama watalaamu wa majina na wanazuoni wa dini mbalimbali wanavyosema, jina huwa linaweza kutafsiri tabia ya mtu! Hivyo CCM wametumia mwanya huo wa kuweza kumtenda John ili awe msemaji wake. Huyu ametendwa kirahisi kwa sababu jina lake lina ruhusu kufanyiwa hivyo! Sasa sishangai anapokosa busara na kuanza kuitisha CDM ambayo haijaanza kutekeleza mipango yake ya kujilinda na kuwaacha Green Guard (Mungiki ya Tanzania) wanao ua na kuumiza watu! Kila mara vyombo vya habari vianatangaza Mh. Mbunge Nassari alipigwa na kujeruhiwa na Green Guard, kwanini hili halikemei?
 
Tendwa ni kati ya wazee ambao bila shaka ameshaingiliwa na magonjwa ya uzee, na ni mwana-CCM hai kwa hivyo ukimuuliza kambi za CCM zilizokuwa zinaonyeshwa dhahiri na green guard kubeba silaha kubwa, bunduki na nyinginezo atasema hakuambiwa!! au atasema CCM hawazitumii, walikuwa wamebeba kama geresha tu! akiulizwa kwanini Green Guard wanatumia nguvu kuteka kupiga, kung'a kucha na meno na kuua wanaharakati na wanachama wa vyama vingine atasema hajawahi kusikia??

Tendwa ni kati ya viongozi hovyo..wanaojilamba-lamba, na wasio na direction ya kusimamia hali na maendeleo ya demokrasia kwa tanzania au taifa lolote changa...! hii siyo mara ya kwanza kwa Tendwa kujiuma-uma, anaona taifa ni kama kambi ya kuku au mifugo ya kuswaga bila kufikiria! Kwa kawaida huyu jamaa ni mwoga, mnafiki na mla-kuwili (double std), ndio maana kampa msaidizi wake kuwasilisha tamko, maana alijua wana-habari wasio makanjanja wangemuuliza maswali mengi, angeanza kutetema!

Chadema inatakiwa kumpuuza Tendwa kwa kila asemalo dhidi yao hadi apate akili mpya, na ikiwa hapati akili, awekwe ktk agenda ya watu ambao wanaua demokrasia, 'anailea' CCM na magaidi wao waliojaa ktk kambi za mafunzo ya Green Guard. "Demokrasia Tz bila Tendwa -- inawezekana vyema sana", kama ilivyo "Tanganyika mpya bila CCM inawezekana mapema sana!"
 
nimesikia anaendeshwa na nguvu ya whisky
Labda kama amehamia huko ila huyu mzee ni noma kwa viroba,umri huo anaendekeza ulevi ovyo kabisa halafu anapewa kazi nyeti kama hiyo na njaa nayo inamnyemelea akitoka tu kwa hiyo ofisi kwishney,atabaki historia tu.
 
huyu babu kavurugwa sasa kama mtu anamfanyia fujo ataenda polisi kwanza bila kujitetea? na kwa dunia ya sasa huwezi kujitetea bila kuwa fiti babu kwa ujumla wake kavurugwa. VIVA CDM VIVA M4C

Huyu John Tendwa anasumbuliwa na Bingo ya Lukuvi ya Milioni 100!
Alivoshupalia swala la Red Brigade inaonyesha kabisa kuwa kuna msukumo nyuma yake wa Serikali ya CCM!

Huwezi kuwa Msajili wa Vyama vya siasa na ukawa unafanya kazi kwa mtindo wa "Double standard"! Kusema kuwa sheria hairuhusu vikundi vya ukakamavu na wakti huohuo CCM wana kikundi cha Greenguard kinacholinda Vigogo wa CCM ni unafiki na ushabiki wa kipumbaf uliopitiliza mipaka.

Ni bora Tendwa akanyamaza kimya na kuachana kabisa na hoja hii inayozidi kumdhalilisha!
 
Back
Top Bottom