KALOKAGATHOS
Member
- Jul 9, 2013
- 38
- 6
TEKU bila TEKU HALL,LIBRARY,HEKIMA,AMANI na UZIMA HOSTEL ni majanga makubwa!,kumbi kama za SIMWANZA na MWAKASYUKA hazifai kwa maana kuna muingiliano wa mwangwi,wahadhiri wamegoma kutumia vipaza sauti kisa hawajazoea vitu kama hivyo,semina rooms zinavuja,kama mvua inanyesha mambo si mazuri,viti 90 kati ya 100 vimevunjika lakini utawala kimyaaaa! kuna ukumbi kama ule wa MWANGUKU umevamiwa na wadudu hatarishi kama vile mende,viroboto,kunguni,nyuki na nyoka.jamani kama jana kuna mwanachuo aligongwa na nyoka akiwa darasani.mazingira ni machafu na tayari cafteria hapaliki hapanyweki.wanajitahidi kujenga hostel za magorofa na kupanda nyasi uwanja wa mpira lakini madarasa na viti vya kutosha havionekani.si vibaya kujenga mabweni wala kupanda nyasi uwanjani,lakini madarasa na viti ni muhimu jamani duh!! jengeni basi hata magorofa mawili tu kama mnavyofanya kwenye kujenga mabweni ili heshima na mazingira ya kusomea yarudi! pale madegree wekeni paa maana mvua inavuruga kila kitu.ni hayo tu.
NI MIMI NYOKA MNYWA MAFUTA
NI MIMI NYOKA MNYWA MAFUTA