Kirikou Wa Kwanza
JF-Expert Member
- May 24, 2013
- 3,564
- 1,989
Guys, kama kichwa cha habari kinavyosema; Tecno Spark ni toleo jipya la simu kutoka kampuni ya Tecno. Hawa jamaa wamekuja tena. Nimepitia baadhi ya maoni kwenye mitandao yanasema, body ya Tecno Spark ni copy ya iPhone 7; na ukiiangalia hii simu ya Tecno Spark kweli inavutia sana kwa muonekano wa nje. Hii simu inashawishi kuinunua, lakini sisi kina yahe wenye pesa za kuungaunga tumesita kidogo kwenda kuinunua kichwa kichwa kutokana na historia ya simu za Tecno kutokuwa imara, mfano simu kuzimazima kama ina ugonjwa wa kifafa. Hizi Tecno Spark K7 na Plus K9 zote ni non-removable battery na zote zina fingerprint. This time jamaa wamekuja kivingine upande wa software, au ndiyo yaleyale? Msaada kama umeinunua unaweza kutuelezea uzuri na ubaya wake... Thanks.