Tecno Mobile ndani ya GSM Arena

Mkuu mimi binafsi nafikiri ni brand tu.Nothing more nothing less.Binafsi sio brand conscious so huwa hata siwazagi kivile.Hesabu yangu huwa ni simpe:Requirements zangu-specification zangu= Price ambayo nitalipia ikiwa -ve I will pay less na ikiwa + I will pay more
 

Hapo unatumia simu gani kwanza.
 
Simu nzuri sio jina aisee jamaa, ni ubora wake, ubora wa tecno ni mdogo sana kwa sumsung , huawei, nokia, nk
Umeshawahi zitumia? Ipi na ipi?

Na vitu gani vimesababusha useme hazia ubora?
 
Short n clear


Watu wamekariri majina
 

Mkuu hujajua tu ! Jaribu kutumia high end phone utaona utofauti mkubwa , achana na camera achana na charge achana na processors , hivyo vyote achana navyo ila kuna vitu huwa havielezeki mfano uki scroll kwenye iphone na uka scroll kwenye tecno ni vitu viwili tofauti , yan ile response na smoothness ni tofauti kabisa . High end phones una click kwenye app mara moja , ila watu wa tecno kurudi nyuma naonaga wanabonyeza bonyeza ile back button mara kibao . Sasa tumia iphone one ni click moja tu na hamna issue za ku stack stack na kusubirishana. Fungua camera angalia inachukua mda gani ku focus kwenye subject ndo utajua nini maana ya ubora . Hata vitu mnavyoviita vya kawaida mfano wakati wa ku type ile speed ya response ni kitu muhimu sana na ni cha kila siku Ndo maana mtu akitumia high end kurudi chini lazima apate shida. Whatsap ya iphone siyo sawa na whatsap ya tecno na huu ndo ukweli ingawa zote zinatuma Picha na sms . Nimeona tecno wameweka animoji isee ni vituko !

Au simple zaidi labda endesha Swift na endesha Nissan Murano labda , kwenye swift unatumia nguvu nyingi, brake haziko on time yan ukitoka dar Moro uko hoi ila gari nzuri mzee huchoki.. huo ni mfano wa experience tunaoumaanisha

Swala la kusema tecno ni sub standard Kwa sababu haziko gsm arena tulikuwa sahihi 100% , sisi kaka watumiaji wa simu hatuwezi kumsikiliza tecno tu ndo atwambie ubora wa bidhaa zake , tunahitaji third party wa kudhibitisha huo ubora ili tumlinganishe na wengine tuone.

Pale unapokuta model ya simu dukani then ukaitafuta mtandaoni na usipate details za kutosha jua kwamba kuna tatizo ( kiufupi Mteja lazima ajue ananunua nini , ni muhimu sana) kama hujui unanunua nini unaanzia wapi ku negotiate? Yan una negotiate kitu ambacho hukijui? Mtu anakwambia camera Kali tu basi , serious? Unaona neno kamera kali linatosha kumwambia mteja anayejielewa?

GSM arena pale simu inapimwa na kulinganishwa kuangalia kama yaliyomo yamo.

Angalia hapo chini kwenye picha nimeweka 3D Touch ya iPhone ambavyo inaweza nisaidia natumia keyboard kama mouse pad , yan hiyo na move cursor popote Kwa kidole gumba in case nataka ku edit , space , highlight sehem yoyote wakati naandika n.k. Sasa vitu kama hivi kwenye tecno hamna lakini mkiambiwa mnakimbilia oooh hata sisi tunatuma whatsap , sijui fb tunaingia. Issue ni experience gani unaipata kwenye matumizi ya simu yako
 
Sijawahi kutamani kutumia tecno,nipo samsung tangu enzi za R220
 
Hivi bei ya bus la scania ni ghali sana?
Maana naona mabasi ya kichina ndio mengi na tunasafiria na tunafika safari salama.
 
Hivi bei ya bus la scania ni ghali sana?
Maana naona mabasi ya kichina ndio mengi na tunasafiria na tunafika safari salama.
Ila hayadumu [emoji3][emoji3][emoji3]

Angalia marcopolo za abood bado zipo vile vile miaka zaid ya 10, angalia BM yutong hata haijuilkan saiz ipo wapi [emoji3]
 
Sasa hio ndio shida ya Tz tunataka tutumie kitu mpaka mjukuu aone. Viwanda vitakufa jaman[emoji23]
Ila hayadumu [emoji3][emoji3][emoji3]

Angalia marcopolo za abood bado zipo vile vile miaka zaid ya 10, angalia BM yutong hata haijuilkan saiz ipo wapi [emoji3]
 

Asante kwa kushare experience yako.

Binafsi:

Hilo la kuscrol ndio nalisikia kwako
Hilo la kuclick mara mbili ndio nalisikia kwako.

Vitu kama 3d touch mouse havina umuhimu wowote kwa mtumiaji wa kawaida.

Aina nyingi, storage ya simu ikijaa hii ya kustact stack hutokea.

Turudi nyuma, je ni watz wangapia wana uwezo wa kutumia high end? Still Tecno ni chaguo sahihi na lenye kukidhi vigezo kwa mtumiaji wa kitanzania

Pia zingatia kuwa kitu kuwa cha bei rahisi haimaanishi ni sub-standard. Mfano mzuri wa kitu substandard ni kama zile note zilizokua zinalipuka na zile iphone zilizokua zikizibwa kwenye antena hazishiki network. Sub-standard ni sawa na amaps iliokua inapeleka watu chaka..
 

Mwafrica wa kawaida una maana gani ? Inaposema hali ya chini ni hali ya chini kiwango gani ?

Hiyo siyo mada nayoongelea hapa , issue ni tecno kutokuwa gsm arena na sasa kuingia huko , hii ndo issue . Me nimekwambia tulikuwa sahihi na bado tuko sahihi kuziita tecno simu za kikanjanja Kwa sababu hakukuwa na kipimo cha kuzipima sasa huo ndo ukanjanja tunauongelea. Siilingalishi tecno na IPhone maana hata havilingani Kwa hali yoyote ile ni mbingu na ardhi.

Labda nikwambie ukanjanja maana yake nini na hapa ntatumia camera maana ndo mojawapo ya app maarufu. Unakuta tecno ina 20 mp mpaka kwenye selfie camera, ila processor ndogo na sensor size ndogo ukiachana na mambo mengine , sasa hii maana yake ni kutokuwa na balance kwenye kupiga Picha ikiwemo speed , focus na adjustments (labda soma nini maana ya megapixel in relation to processor na sensor size katika determination ya ubora wa Picha) . Sasa wao wanachokifanya wanamuhadaa mteja Kwa kutaja megapixel kila sehem wanamtajia megapixel mtu ananunua akitegemea kitu kizuri mwisho ni frustrations . Sasa kwenda gsm arena kidogo mtu ataelewa!
 
Yah najua wanaiga simu nyengine ambazo ni brand maarufu ila ninachozungumzia ni kwamba hakuna haja ya kununua simu yenye specifications nyingi wakati hauzitumii, ndo mana nashauri watu wanunue simu za bei rahisi kulingana na matumizi yao jinsi yalivyo rahisi
 
Mbona lg hujataja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…