technical college vs A-level

Kama umemaliza kibaha special xul na umepata A tatu na B nne(wani ya 11) basi utakua kilaza sana,wengine tumepiga Aza boy(One ya 9) tukaenda huko kibaha tukalamba one ya 3,jipange mkuu,achana na tek nenda mzumbe au ilboru ukapige tatu yako chuo ukachukua(UDSM) CIT au Telecomm Eng zen piga GPA yako above 4.5 ubakizwe pale ule maisha,tech hakuna kitu kuanzia DIT,MTC,ATC kote famba elimu rahisi sana na ukija chuo umetoka tek yani unakua mweupe sana! Soma dogo one ya 11 isikuchanganye max ndogo sana hizo!!!

Mkuu naona sasa hapa unatafuta kufanya mashindano yasiyokuwa na tija yoyote kwako, kwa huyo dogo na wanajf wote kwa ujumla.

Nataka nikuhakikishie kwamba usijaribu kui underate elimu ya FTC hata kidogo, ile kitu ni kiboko yake. Lakini kwakuwa unaamini kwamba A level ndio kiwango, basi baki ukiamini hivyo hivyo na sisi tuliopiga FTC tubaki tukiamini kwamba ndio kiwango. FTC anaingia aliyefaulu tu na unaanza kujengwa katika taaluma yako mapema na hata ukienda chuo kikuu unakuwa unaongezea tu ujuzi.

Kwani mwisho wa siku wote ni wahandisi right now, na maisha tunayasongesha bila matatizo hadi unaona sasa tuko hapa jf kubadilisha mawazo na kupigania ukombozi wa watanzania toka kwa mkoloni mweusi ccm.
 
Mkuu naona sasa hapa unatafuta kufanya mashindano yasiyokuwa na tija yoyote kwako, kwa huyo dogo na wanajf wote kwa ujumla.

Nataka nikuhakikishie kwamba usijaribu kui underate elimu ya FTC hata kidogo, ile kitu ni kiboko yake. Lakini kwakuwa unaamini kwamba A level ndio kiwango, basi baki ukiamini hivyo hivyo na sisi tuliopiga FTC tubaki tukiamini kwamba ndio kiwango. FTC anaingia aliyefaulu tu na unaanza kujengwa katika taaluma yako mapema na hata ukienda chuo kikuu unakuwa unaongezea tu ujuzi.

Kwani mwisho wa siku wote ni wahandisi right now, na maisha tunayasongesha bila matatizo hadi unaona sasa tuko hapa jf kubadilisha mawazo na kupigania ukombozi wa watanzania toka kwa mkoloni mweusi ccm.

Mkuu nimesoma na watu wengi UDSM waliotoka tek yani unawaonea huruma na waulize ma-tutor hapo UDSM watakwambia, yani aibu hadi unajiuliza kwanin asingebak huko huko alipotoka?
 
Labda nikusaidie tu kwamba hivi vyuo vya elimu ya juu tunavyovizungumzia hapa vya calibre ya DIT (Tertiary institutions) haviko chini ya TCU, hivi viko chini ya NACTE.

Jambo la pili, kama kweli TCU wanayo sheria ya kuwalazimisha waliomaliza diploma wafanye kazi walau mwaka mmoja kabla ya kuendelea na degree ningependa kuifahamu ni sheria namba ngapi na kama utanisaidia kuipata nitashukuru sana, lakini kuna watu ninawafahamu vizuri,labda niseme hata mdogo wangu amemaliza diploma na akaingia chuo kikuu moja kwa moja bila kufanya kazi mahali popote.

Kama itakuwepo sheria ama kanuni ya namna hiyo, basi TCU watalazimika kuwahakikishia ajira wahitimu wa diploma, kwakuwa suala la uhaba wa ajira nchi hii kila mtu analifahamu.

Ninachokumbuka ni serikali kuingiza kinyemela kigezo cha kutowapatia kipaumbele cha kupata mikopo kwa wanafunzi waliomaliza diploma kwa kisingizio kwamba wengi wanakuwa wameajiriwa kwahiyo watumie waajiri wao na mifuko ya pensheni kupata ufadhili, kitu ambacho si kweli na hiyo imepelekea wanafunzi wengi kukosa ufadhili kwa "umbumbumbu" huo wa watu wa wizara ya elimu.

Nafahamu kuwa DIT kipo chini ya Nacte lkn kwa 7bu kinatoa degree kinahucka kidogo na tcu ndo maana wanafunzi wanaoenda kusoma pale kwa level ya degree wanachaguliwa na tcu(kuanzia mwaka wa masomo 2010/2011)...kuhusu hiyo sheria ya kufanya kazi kwanza,matangazo yamebandikwa kwenye vyuo
 
dogo nenda a levell yanini kwenda kusoma miaka mitatu dit ili hali unaweza ku save mwaka mmoja.kumbuka time is money

Zamani ndio kulikuwa na kupoteza muda, sasahivi unapiga miaka mitatu unapata OD(FTC) kisha unaunga B.Eng miaka mitatu,jumla unakuwa mhandisi baada ya miaka 6, sawa na aliyekwenda A level miaka miwili kisha UDSM miaka minne, jumla miaka 6!!
 
Mkuu nimesoma na watu wengi UDSM waliotoka tek yani unawaonea huruma na waulize ma-tutor hapo UDSM watakwambia, yani aibu hadi unajiuliza kwanin asingebak huko huko alipotoka?

Hao unaowazungumzia ni isolated cases, huwezi kuthibitisha kwamba wote waliopita technical colleges ni weupe. Na hata waliomaliza A level wengi tu wanapata shida wakiwa vyuo vikuu.

Na mifano hai ipo watu waliopita technical colleges na waliperform vizuri sana udsm na vyuo vikuu vingine.
 
Nafahamu kuwa DIT kipo chini ya Nacte lkn kwa 7bu kinatoa degree kinahucka kidogo na tcu ndo maana wanafunzi wanaoenda kusoma pale kwa level ya degree wanachaguliwa na tcu(kuanzia mwaka wa masomo 2010/2011)...kuhusu hiyo sheria ya kufanya kazi kwanza,matangazo yamebandikwa kwenye vyuo

Mdogo wangu ameanza kusoma degree mwaka wa masomo 2011/1012 na alikuwa hajafanya kazi mahali popote, ameunganisha baada ya kumaliza diploma, kwahiyo hilo tangazo hadi nilione ili nijiridhishe na ukweli wake.

Vyuo vya calibre ya DIT kama TCA, MIST, RWI (Technical Colleges) havihusiki na TCU, isipokuwa kuna baadhi ya vyuo ambavyo viko chini ya NACTE kama IFM, CBE, TIA, USTAWI, MWALIMU NYERERE na vingine vya aina hiyo ambavyo vinapokea wanafunzi waliomaliza A level kwa ajili ya kusoma degree, na hawa wahitimu wa A level wanapofanya application za kujiunga na vyuo hivyo wanaomba kupitia TCU, na hapo ndipo unakutana na uhusiano mdogo uliopo kati ya vyuo hivyo na TCU. Lakini taratibu nyengine za uendeshaji wa hivyo vyuo unabaki kwenye mamlaka ya NACTE.

Sina uhakika kama vyuo vya ufundi navyo vimeanza kupokea wanafunzi waliohitimu kidato cha sita kusoma degree, kama vinawapokea basi uhusiano uliopo ndio huo. Nina uhakika NACTE haiwezi kukubali hicho kigezo cha kufanya kazi mwaka mmoja kwanza, na kwakuwa wao ndio wanaohusika katika kuchagua wanafunzi wenye diploma/FTC wanao join vyuo vilivyo chini ya mamlaka yake na wengi wanaunganisha bila kutakiwa kufanya kazi kwanza, hapo ndipo bado napata shaka na sheria hiyo unayoitaja.
 
rafiki yangu ni heri uende technical college....mimi mwenzio csee nilipataga divion one ya point 17......nikaenda a--level miinaki nikapiga pgm.....mwisho wa siku form six.....nilipata four ya 19......hivyo nikajikuta narudi nyuma naanza na certifikate kama mtoto wa form 4
 
rafiki yangu ni heri uende technical college....mimi mwenzio csee nilipataga divion one ya point 17......nikaenda a--level miinaki nikapiga pgm.....mwisho wa siku form six.....nilipata four ya 19......hivyo nikajikuta narudi nyuma naanza na certifikate kama mtoto wa form 4

aisee,pole sana mkuu,ts ol bout lyf.
 
Mdogo wangu ameanza kusoma degree mwaka wa masomo 2011/1012 na alikuwa hajafanya kazi mahali popote, ameunganisha baada ya kumaliza diploma, kwahiyo hilo tangazo hadi nilione ili nijiridhishe na ukweli wake.

Vyuo vya calibre ya DIT kama TCA, MIST, RWI (Technical Colleges) havihusiki na TCU, isipokuwa kuna baadhi ya vyuo ambavyo viko chini ya NACTE kama IFM, CBE, TIA, USTAWI, MWALIMU NYERERE na vingine vya aina hiyo ambavyo vinapokea wanafunzi waliomaliza A level kwa ajili ya kusoma degree, na hawa wahitimu wa A level wanapofanya application za kujiunga na vyuo hivyo wanaomba kupitia TCU, na hapo ndipo unakutana na uhusiano mdogo uliopo kati ya vyuo hivyo na TCU. Lakini taratibu nyengine za uendeshaji wa hivyo vyuo unabaki kwenye mamlaka ya NACTE.

Sina uhakika kama vyuo vya ufundi navyo vimeanza kupokea wanafunzi waliohitimu kidato cha sita kusoma degree, kama vinawapokea basi uhusiano uliopo ndio huo. Nina uhakika NACTE haiwezi kukubali hicho kigezo cha kufanya kazi mwaka mmoja kwanza, na kwakuwa wao ndio wanaohusika katika kuchagua wanafunzi wenye diploma/FTC wanao join vyuo vilivyo chini ya mamlaka yake na wengi wanaunganisha bila kutakiwa kufanya kazi kwanza, hapo ndipo bado napata shaka na sheria hiyo unayoitaja.

Hiyo sheria imebandikwa kwenye vyuo mwaka huu(muulize huyo mdogo wako kama ameisoma atakuambia) na kuhusu wahitimu wa kidato cha sita kwenda kusoma degree kwenye hivyo vyuo,wanaenda kusoma lkn wanachaguliwa na tcu(hapo ndo upo uhusiano kati ya hivyo vyuo na tcu)
 
Dogo... Nenda Technical College(DIT) Kuna faida kuu mbili ambazo ni quaranteed. Mosi , Siku ya kwanza unapoingia DIT, shule unayopata ni kukufanya mtaalamu wa either Umeme, Mechanics, Computer, Ujenzi, Maabara, Madini nk nk nk. Yule wa form6 si hivyo...Yeye Utaalamu anaufukuzia atapofika Chuo..kama ataweza!!


Pili..Wakati ukifundishwa kuwa professional kama Electrical Technician, or Lab.Tech...Pia unaaandaa mazingira ya kuendelea na professional yako chuo kama yule jamaa wa form6...Tofauti ni kwamba kama wote mambo yatawaendea kombo kwa level hiyo..Hebu niambie nami atakayejutia muda wake?? Nani atamwajiri form6 asiye na profession? Ni rahisi sana kwa mtu mwenye OD(FTC) kuajiriwa au kujiajiri kuliko yule wa form6 failure.....


Kwa ujumla Elimu ya Ufundi ni nzuri sana...Na mtu aliyekwambia wanaokwenda Tech ni failure, nadhani alikupotosha..Mimi enzi zetu kweli sheria ilikuwa ngumu kuunganisha chuo moja kwa moja baada ya FTC..Wengi hawakwenda moja kwa moja Chuo..Lakini nikwambia wazi kuwa wengi wao sasa hivi wana masters, CPA na PhD za fani nyingine zaidi ya engineering....Kwa mtu aliyepitia FTC ataungana nami kuwa hakuna elimu yoyote atakayoamua kuisoma akashindwa....Wengi wamesoma Uhasibu, sheria, Biashara nknk na wanatesa kimaisha vile vile...Technical Education is the best..Japokuwa sysytem ya elimu TZ inatupiga vita sana!!! Uchumi wa ujerumani umejengwa na Ma technicians na Engineers...Wizara ya elimu badilikeni jamani!!!!
 
hello wana jf.
mimi nimemaliza form 4 mwaka jana.
matokeo yangu ni mazuri nna dvn 1.11 na AAA PCM.
nilichagua tech colleg(DIT) first choice.nadhani engineer aliyesoma diploma halafu BA ni safi zidi ya alietoka A-level halafu akachukua BA.tatizo watu wengi wananikatisha tamaa na kusema huko colleg si kwa watu wenye ufaulu kama wangu wanasema huko ni kwa waliofaulu kwa kiwango kidogo.....yaani wengi wananiona wa ajabu wanasema kupitia huko ni kujiharibia kwani ajira zinasumbua kwa waliopitia huko.
najisikia vibaya naona kama nibadilishe baada ya matokeo kutoka.sio kwamba siwezi A-level bali nahisi njia ya ttech colg kwa engineerig ni nzuri zidi.

kwa hiyo naomba anayefahamu zaigi anielezee hili swala la A level na tech colg.je mimi nipo sawa au wao wapo sawa


Siku zote shikamana na unachokiamini mdogo wangu usifuate maneno ya watu!!Samahani kidogo,hapo palipokuwa bolded juu unamaanisha Bachelor of Arts au?Kama lengo lako ni kusoma diploma ya engineering halafu university ukasomee Arts (BA) nakushauri bora uende form 5 usomee masomo ya Arts tu moja kwa moja kuliko kupoteza muda na diploma ambayo hautajiendeleza nayo level ya shahada ya kwanza!
 
Jaman mm pia nimemaliza kidato cha nne nimepata points sita za PCM na nimechagua technical college lakn bado napata upinzani kutoka kwa ndugu zangu wanataka niende A level
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom