TCRA acheni uvivu na kutowajibika, fungieni hizi online TV's

Mugisher

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
411
360
Inanishangaza kuona kuwa msimamizi wa mawasiliano Tanzania, TCRA, yuko kimya na hachukui hatua zozote dhidi ya huduma za kiudanganyifu zinazotolewa na baadhi ya hizi online TVs.

Kuna udanganyifu mkubwa na kutokuwa na uweledi unaohusisha hizi online TVs, ambao kwa kweli, lazima hatua stahiki zichukuliwe.

Udanganyifu huu unahusisha uwekaji wa vichwa vya habari ya clips ambazo haziendani na story zenyewe kwenye habari husika kwa minajili tu ya kudanganya watu wafungue hizo clips. Huu ni uharamia na ugaidi wa habari ambao unabidi uchukuliwe hatua. Kama online TVs zimesajiliwa na TCRA zinatakiwa ziwe na weledi kama vile magazeti and radio zingine zinavyofanya kazi. Haiwezekani kichwa cha habari kiwe ni kuhusu 'mbuzi' lakini ukifungua hiyo clip story inayoongelewa ni ya 'ngombe'.

Pili online TVs zinachochea sana chuki na maadili mabovu kwa jamii. Natambua ya kwamba hiyo ndio content watanzania wanafurahia nayo, lakini lazimia kuwe na weledi wakuileta hiyo content kwa jamii. Mfano, haiwezekani habari zote za wasanii ni kuhusu ugomvi au kutukanana kama vile hamna habari zingine zozote za kurusha. Yaani mtu anapata nafasi yakupata story kama anamtukana msanii mwenzake.

Tatu online TVs zina 'waandishi' ambao ni mbumbumbu kweli kweli. Ni muda sasa, hata hawa 'waandishi' wawe na vigezo vya elimu ili kuruhusu wawe wanarusha habari niweledi zaidi. Basi hata cheti tu cha uandishi wa habari. Wengi wao hawana weledi kabisa wa kujua habari gani iletwe kwa jamii na ipi isiletwe au hata tu kuuliza maswali.

Kwa kweli TCRA acheni uvivu na fanyeni kazi yenu kama mtavyotakiwa kisheria. Upuuzi huu wa baadhi ya online TVs umefika mahali ambapo sasa hatua stahiki lazima zichukuliwe
 
Siku Watanzania tukianza Kuuana na pengine hata Staff wao ( TCRA ) nao labda wakifa au wakiwa Wahanga watazifungia Mkuu.
 
Kweli hili jambo la msingi sana; wanakuja na habari za uongo kila siku halafu hakuna wa kuwazuia, hao TCRA sijui wanafanya nini huko maofisini, hao matapeli kutwa wanakwambia ukitaka uongo mwingine kama huu subscribe!. sitaki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TCRA hawana uwezo wa kufunga Online TV....Online TV ni Youtube channel ambazo boss wao ni Google,na Google haipo Tanzania pia google wanamtaka mmiliki wa youtube channel awe mjanja na mbunifu ili aweze kupata views na apate kipato kizuri...

Narudi kwako kwa wewe mwenye roho mbaya ,ukitaka habari za uhakika angalia TBC ,CLOUDS ,WASAFI, ITV ,EATV na zinginezo...

Kuhusu Online TV achana nazo kwasababu wapo kimaslai zaidi hawana mda wa kukuretea unacho kitaka wewe wakati kwa upande wao hakina maslai

Sent using Jamii Forums mobile app
 
H
TCRA hawana uwezo wa kufunga Online TV....Online TV ni Youtube channel ambazo boss wao ni Google,na Google haipo Tanzania pia google wanamtaka mmiliki wa youtube channel awe mjanja na mbunifu ili aweze kupata views na apate kipato kizuri...

Narudi kwako kwa wewe mwenye roho mbaya ,ukitaka habari za uhakika angalia TBC ,CLOUDS ,WASAFI, ITV ,EATV na zinginezo...

Kuhusu Online TV achana nazo kwasababu wapo kimaslai zaidi hawana mda wa kukuretea unacho kitaka wewe wakati kwa upande wao hakina maslai

Sent using Jamii Forums mobile app
Hao Jamaa wa online ni wezi , haliwezekani kichwa Cha habari kiwe tofauti na habari husika , kufungia wanaweza si wanampa Amri mwenye nayo hasiiendeshe( aizime)
 
Wananilipa kodi... Ni kiwanda hicho.
Nawe anzisha yako.
 
Back
Top Bottom