Habari za muda huu wakuu? Poleni kwa msiba wa mzee wetu.
Naomba niende kwenye hoja yangu, kuna hii dawa ya kuua wadudu aina ya Rungu imekua kimeo sana sijui kama TBS wanaliona hili.
Nimekuwa mteja wa dawa hii kwa muda kidogo na pale mwanzo ilikuwa vizuri sana lakini kadri siku zinavyoenda hakuna kitu kabisa.
Unapuliza dawa mbu hata hawafi wala kulewa badala yake inakuwa kero kwa harufu yake kali na mbaya.
TBS na wote mnaohusika kusimamia hebu tusaidieni kwa hili pengine hawa ndugu zetu wamejisahau wanaangalia faida wamesahau kuangalia ubora wa bidhaa yao.
Naomba niende kwenye hoja yangu, kuna hii dawa ya kuua wadudu aina ya Rungu imekua kimeo sana sijui kama TBS wanaliona hili.
Nimekuwa mteja wa dawa hii kwa muda kidogo na pale mwanzo ilikuwa vizuri sana lakini kadri siku zinavyoenda hakuna kitu kabisa.
Unapuliza dawa mbu hata hawafi wala kulewa badala yake inakuwa kero kwa harufu yake kali na mbaya.
TBS na wote mnaohusika kusimamia hebu tusaidieni kwa hili pengine hawa ndugu zetu wamejisahau wanaangalia faida wamesahau kuangalia ubora wa bidhaa yao.