TBS hizi nguo za kichina mnaziona?

TBS hizi nguo za kichina mnaziona?

Huku uswahilini kuna bidhaa sizani kama zinapitia TBS,mf hizi dawa za mbu za kuchoma,UFRESH (hizi watoto wanazipenda na sukari nyingi) ,kuna pipi zipo kwenye pakti ndondogo size ya punje ya mchele zina sikuri nyingi mno na watoto wanazipenda .
 
Mara nyingi bei ya kitu huendana na ubora wake, usitegemee shati ya 2500 ifanane na ya 25000.

Halafu Mtanzania ukimwambia hili shati bei yake 25000 kulingana na ubora wake atakwambia mbona kariakoo yapo mengi tu 2500 hajui kama ni kopi ya mwisho ya mchina.

Yote kwa yote umasikini wetu ndio chanjo, mahitaji mengi kuliko kipato.
 
Sie wavaa mitumba ya bei ghali mbona tunapeta tu.... Nguo zimesimama quality mpaka muonekano, na unaweza kuifua mwaka mzima bila matatizo yoyote...


Kweli kabisa. Mimi nimeachana na hizo special za kizushi nagonga used.Sema Tz tunakosea,tumediscourage mitumba kwa kuweka kodi kubwa, wenzetu Kenya biashara imeshamiri balaa.Sasa hivi vitu vikali vinatoka NBI, bei zake ni moto.
 
Mara nyingi bei ya kitu huendana na ubora wake, usitegemee shati ya 2500 ifanane na ya 25000.

Halafu Mtanzania ukimwambia hili shati bei yake 25000 kulingana na ubora wake atakwambia mbona kariakoo yapo mengi tu 2500 hajui kama ni kipi ya mwisho ya mchina.

Yote kwa yote umasikini wetu ndio chanjo, mahitaji mengi kuliko kipato.


Usemacho ni kweli lakini hali halisi haipo hivyo ndugu yangu.Mimi nishanunua mashati ya 80,000/=, suruali za 120,000/=, kwenye hizo malls unazozijua hapo Dar,hamna kitu.

Nilichogundua, miaka ya nyuma haya maduka ya ghali walijitahidi kuleta vitu safi,lakini, wakausoma mchezo kuwa Tz ni wapumbavu,unaweza kuwavalisha makaratasi wakavaa bila kelele. Wakageuza kibao. Amini usiamini,mavazi yanayouzwa leo pale Woolworths kwa mfano, siyo yale ya miaka ya 2000 mwanzoni.
 
Sure zaman nilikua nachukua shati kAriakoo kwny yale maduka ya nguo pale miaka ya 2007- 2010 shati hadi leo ninazo zipo safi ila now kila nkienda naishia kuondoka bila shati narudi karume kusagula yani mashati ya dukani hakuna mashati wala suruali nzuri tena kama kipindi kile....

Kuna viatu flan vinaitwa sebago miaka ya 2014 dukani vilikua quality ila leo cheche
 
Mnauziwa kulingana na uwezo wa soko. Mfano dukani kuwe na Levi's jeans OG bei £60 au Lacoste t-shirt £65 au Tims £160 wangapi wataweza kununua kiasi cha duka ku-sustain biashara? Hizo za Kariakoo ndio size za majority na kibiashara ndio zinafaa. Nunua nyingi fua mara moja kwa mwezi zitamudu ila ukitaka kufua kila wiki hamna rangi utaacha ona
 
Mnauziwa kulingana na uwezo wa soko. Mfano dukani kuwe na Levi's jeans OG bei £60 au Lacoste t-shirt £65 au Tims £160 wangapi wataweza kununua kiasi cha duka ku-sustain biashara? Hizo za Kariakoo ndio size za majority na kibiashara ndio zinafaa. Nunua nyingi fua mara moja kwa mwezi zitamudu ila ukitaka kufua kila wiki hamna rangi utaacha ona
Lakini sidhani hata huko nje ulaya kila mtu anaafford kununua t-shirt ya £60,lakini bado wanavaa nguo nzuri zenye quality..sisi tunakwama wapi??

Ni lazima tukubali hawa wachina wanatuletea vitu vya hovyo sana kwenye nguo..
 
Lakini sidhani hata huko nje ulaya kila mtu anaafford kununua t-shirt ya £60,lakini bado wanavaa nguo nzuri zenye quality..sisi tunakwama wapi??

Ni lazima tukubali hawa wachina wanatuletea vitu vya hovyo sana kwenye nguo..
Idadi ya hao wachache wanatosha kufanya maduka hayo kujiendesha,hapa idadi ni ndogo sana,tutafika baadae kidogo.

Ni kweli huko Ulaya nguo ya £10/15/20 ni nzuri sana tofauti na nguo ya tzs 50,000-100,000. Tatizo sio Wachina ni watu wetu ndio wanatupiga kwasababu vitu vizuri vya Ulaya na Marekani vinatengenezwa China.
 
Nadhani tatizo linaweza kuwa pande zote. Kwa upande wa wanunuzi wanapaswa kuangalia specifications na instruction za nguo, kuna nguo ambazo zinahitaji zifuliwe kwa machine, na zingine ni dry cleaning tu. Sasa nguo inayohitaji dry cleaning ukiifua kwa maji hata uinyoonshe vipi haitokaa sawa. Na hata nguo za kufua kwa machine pia zina specification za maji unakuta umeambiwa ufue kwa maji baridi tu au moto tu au vuguvugu, sisi tunafua tunavyojua sisi, haiwezi kuwa sawa. Kuna nguo hazi nyooshwi kwa pasi zinanyooshwa kwa mfuke wa moto, sisi tunanyoosha.
Jingine ni maji yetu, huko zitokako maji yana kuwa treated kupunguza mineral contents, hapa kwetu hilo halifanyiki, na kuna wengine hutumia maji ya visima au yakuvuna ya mvua, yoote haya yana athari zake kwenye fabrics.
Sabuni, kuna za unga, vipande, na za maji. Hapa kwetu sabuni nyingi ni kali sana, kwasababu nahisi maji yetu ni hard water na sio soft water hivyo watengenezaji wa sabuni kwa kuzingatia hilo huziongezea kemikali na kuzifanya kali sana, sasa na ufuaji wetu mtu analoweka nguo 24hrs kwenye sabuni kali, anategemea fabrics za hiyo nguo ziwe sawa, hapana.
Huko wanakozitengeneza, hawalengi soko la Afrika, ila kwasababu za kibiashara wanaleta tu au kuchepusha na hapo ndio sisi tusio treat maji, na kutumia sabuni kiasi maalumu na kwa muda maalumu, na tusio tumia washing machines na kupikicha yanatukuta yote haya.
Na nguo zinazofuliwa kwa dry cleaning sisi tuna fua kwa maji tena mtu anailoweka 24hrs, kwanza haihitaji maji kabisa, lakini umeifua, mbaya zaidi umeiloweka 24 hrs huwezi kutegemea iwe au irudie ubora wake.
Hivyo tujifunze kuangalia label zinasemaje kabla ya kununua, na kama hukuangalia label basi angalia kabla ya kuifua, unaweza kuta haifuliwi ni dry cleaning fabrics, na unapo nyoosha angalia label, inahitaji dry heat, au mvuke, ukifuata masharti ya manufacturer hutojuta, na huto lalamika. Sisi tunajisahau, au hatujali kabisa manufacturer instructions, sio nguo tu, hili liko kwenye vitu vyote. Tukijifunza kutafiti na kuangalia mahitaji ya kitu, kwa case hii nguo, na kujali hatuta juta, lakini ukiangalia mahitaji yako tu bila kujali mahitaji ya nguo uliyoinunua bei ghali hutoisha kulalamika kila siku.
Hata mitumba inazo instructions of care, tuwe waangalifu tusijiumize ki uchumi.
Waswahili tunasema, " cheap is expensive" hahaha, any way mmeelewa nadhani.
Kila la kheri.
 
Mchina anatabia ya kumridhisha mfanyabiashara kwa kutengeneza kitu cha bei anayotaka mfanyabiashara.
Wanaotuteza ni Wafanyabiashara wa kwetu ambao hutafuta utajiri wa haraka haraka kwa kununua vitu vya ovyo vyenye muonekano mzuri kwa bei ndogo na kuviuza kwa bei ya juu.
Kwa mfano kuna wakati ma contena ya Kinywaji aina ya Red bull toka China lilikamatwa na baada ya kukaguliwa ubora wake kinywaji hiki kilionekana ni fake kabisa.
Waliosababisha hiki kinywaaji kikamatwe si wanywaji mbali ni wafanyabiashara halali wa red bull.
Mchina yeye anachotaka ni fedha, ukitaka gari aina ya saloon la bei ya shilingi 4m atakutengenezea.
Gari hili litakuwa na mapungufu mengi sana na huwezi kusafiri nalo mwendo mrefu. Kwa muonekano, mfanyabiashara anaweza kuliuza hata kwa shilingi 12m.
 
Idadi ya hao wachache wanatosha kufanya maduka hayo kujiendesha,hapa idadi ni ndogo sana,tutafika baadae kidogo.

Ni kweli huko Ulaya nguo ya £10/15/20 ni nzuri sana tofauti na nguo ya tzs 50,000-100,000. Tatizo sio Wachina ni watu wetu ndio wanatupiga kwasababu vitu vizuri vya Ulaya na Marekani vinatengenezwa China.
Hahaha hatupigwi, hatufuati maelekezo ya jinsi ya ku care hizi nguo. Tatizo siyo bei, tatizo ni kukosa tools, au maarifa ya ku care nguo hizi. Hatuna washing machines, hatufuati kiasi cha sabuni, aina ya sabuni, hatuangalii contents.
Nguo inahitaji dry cleaning tunafua tena tuna pikicha. Nguo inahitaji maji vuguvugu tunatumia baridi, nguo isiyo nyooshwa tunanyoosha.
Lazima tuwalaumu wachina na wazungu, kwa sababu hatufuati maelekezo.
 
Mchina anatabia ya kumridhisha mfanyabiashara kwa kutengeneza kitu cha bei anayotaka mfanyabiashara.
Wanaotuteza ni Wafanyabiashara wa kwetu ambao hutafuta utajiri wa haraka haraka kwa kununua vitu vya ovyo vyenye muonekano mzuri kwa bei ndogo na kuviuza kwa bei ya juu.
Kwa mfano kuna wakati ma contena ya Kinywaji aina ya Red bull toka China lilikamatwa na baada ya kukaguliwa ubora wake kinywaji hiki kilionekana ni fake kabisa.
Waliosababisha hiki kinywaaji kikamatwe si wanywaji mbali ni wafanyabiashara halali wa red bull.
Mchina yeye anachotaka ni fedha, ukitaka gari aina ya saloon la bei ya shilingi 4m atakutengenezea.
Gari hili litakuwa na mapungufu mengi sana na huwezi kusafiri nalo mwendo mrefu. Kwa muonekano, mfanyabiashara anaweza kuliuza hata kwa shilingi 12m.
Hahaha ndugu kila kitu kabla hujanunua tafiti mazingira yako,otherwise hutoisha kulalamika. Kila kitu kina operate kwenye specified environmental conditions. Usipofuata maelekezo utalalamika tu.
 
Mimi kinachonishangaza siku hizi ni size za hizi nguo zilizo dukani. Yaan zinabana kiasi kwamba huwez vaaa kama ni fashion jamani sio kwa style hii ya siku hz. Unakuta mtu unavaa suruali kiuno size 34 lkn uende dukani upate suruali ya size hy nakuambia paja halipitiiii.. hivi hii imekaaje..???
 
Mara nyingi bei ya kitu huendana na ubora wake, usitegemee shati ya 2500 ifanane na ya 25000.

Halafu Mtanzania ukimwambia hili shati bei yake 25000 kulingana na ubora wake atakwambia mbona kariakoo yapo mengi tu 2500 hajui kama ni kipi ya mwisho ya mchina.

Yote kwa yote umasikini wetu ndio chanjo, mahitaji mengi kuliko kipato.

Acha kuongea ww, ata ayo ya 25k matatizo yake ni yaleyale
Infact mashati mengi congo ni 18 mpaka 27k
Apo ni kuibiwa tu otherwise uwe mtaalam sana
Mengi mazuri ni ya ovyo ukikaa nayo mwezi
 
Hahaha hatupigwi, hatufuati maelekezo ya jinsi ya ku care hizi nguo. Tatizo siyo bei, tatizo ni kukosa tools, au maarifa ya ku care nguo hizi. Hatuna washing machines, hatufuati kiasi cha sabuni, aina ya sabuni, hatuangalii contents.
Nguo inahitaji dry cleaning tunafua tena tuna pikicha. Nguo inahitaji maji vuguvugu tunatumia baridi, nguo isiyo nyooshwa tunanyoosha.
Lazima tuwalaumu wachina na wazungu, kwa sababu hatufuati maelekezo.
Hili nalo ni tatizo. Lakini nguo nyingi za Kariakoo hazina labels zenye maelekezo hayo
 
Hili nalo ni tatizo. Lakini nguo nyingi za Kariakoo hazina labels zenye maelekezo hayo
Hahaha hivyo tatizo sio nguo ni nguo zinazouzwa kariakoo?! Label zipo, I bet hata nguo uliyovaa ina label, ila ni kitu sisi hatukijali kabisa tuna angalia kila kitu lakini siyo label, kwasababu ni kadogo sana au hatujui umuhimu wake, halafu tunalalamika.
Ni nguo za kariakoo tu, vipi za Mwenge, Ubungo, Tegeta, au Tazara?!
Hahaha sisi hatuishiwi malakamiko hata kwa matatizo yetu wenyewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom