Elections 2010 TBC1 ni wachafu!

Uzoefu, mazoezi na umbo langu nililo nalo ccm mkianzisha zogo mtakiona hata viefuefu vyenu tutavikwida!Hata mkitutisha na hivyo vigwaride vya kuvishana vyeo. Hasira zikisha panda mtakoma
 
wajami ni mojawapo ya mipango mingi ya kumdhoofisha DR slaaaaa.
1. TBC 1 inatumika, pamoja na kuweka coverage za CUF zadi wakati inajulikana wazi kwamba libumba anapoteza muda tu
2. Mipango zaidi yaandaliwa kuwachafua

tupambane kuuelimisha umma---popote utakapokuwa kuweni watetezi wa kweli wa Dr Slaaaaa
 
Jana jioni niliangalia taarifa ya habari ya TBC1 nakuona jinsi hii TV ya uma ilivyo chafu! Walitoa habari ya ukosefu wa maji katika mjini wa Karatu. Ni aibu sana TV ya uma inayoongozwa na mtu aliyepata "exposure" ya jinsi vyombo vya uma vya wenzetu vinavyoendeshwa, yeye anafanya kinyume!
Hii habari ilikuwa ni kumchafua Dr. Slaa na Chadema kwa ujumla. Hivi jamani ukosefu wa maji katika nchi hii ni habari kweli? haya ni maisha ya kila siku. Dar ni sehemu ngapi maji yanatoka muda wote, watu wasichote kwa madumu kutoka mbali? Kwa nini iwe habari kwa Karatu?
Ushauri wangu mafisadi wa nchi hii, mwisho wenu hauko mbali. Tumieni tu ulafi wa akina Tido Mhando na wengineo kwa maslahi yenu, lakini mjue wazalendo inatuuma na ipo siku tutaikomboa nchi yetu. Wakuu wa vyombo vya uma na wote wale wenye dhamana kama hizo, muogopeni Mungu----watanzania wamedhulumiwa sana kwa kitendo cha ninyi kuabudu mafisadi na kutumia dhamana hizo kwa maslahi yenu binafsi.

Nalaani kitendo hicho kiovu cha TBC1, kodi zetu mnatumia kwa manufaa ya mafisadi!

Naungana na Kiraia kuwa hiyo ni aibu ya JK na wala sio Dr. Slaa. Kwani kazi ya mbunge kikatiba sio kutekeleza mipango ya serikali bali ni kuwakilisha wananchi kwenye kusimamia, kuiwajibisha serikali na kutunga sheria.
 
Waanze kutuma applications kwenda vituo tofauti vya binafsi kama kile cha ITV na hicho cha Clouds au Radio Uhuru maana hawana sifa tena kufanya kazi katika kituo cha habari kinachomilikiwa na Umma.
 
Watuonyeje makazi ya watu wa mkoa wa pwani wilaya zote na maisha yao kwa ujumla ampabo jike wa ccm anazaliwa
 
Mwanza kuna maeneo kibao maji yanatoka usiku tu kuanzia saa sita hadi saa kumi na moja, ziwa liko karibu! hilo ccm haliwanyimi usingizi isipokuwa wanataka kuonyesha watz hata karatu ni hovyo.

CCM toka ikulu wanazlendo tujenge nchi. Muone kama hatujaendelea mbele.

avatar26464_3.gif

safi sana
 
Mimi natumia king'amuzi chao lakini channel za TBC1 na TBC2 nimeweka ktk PG (parental Guide). hakuna ruhusa kuangalia na sijampa mtu password.


Hivi hawajagundua kwamba kila watakachotangaza kwa hila kitajulikana? Hawachoki? Maana Watanzania wa leo sio wa mwaka 2005.. Hata mimi huwa siwapi nafasi ya kunichafulia mood kabisa siku hizi, sina haja na taarifa zao zilizochakachuliwa!!!
 
Wachafu sana ni wakuwapiga mawe,haswa TIDO MHANDO mzee mstaafu wa BBC hana akili kabisa anataka nchi yetu ingie kwenye mauaji anavyokandamiza demokrasia nitamchukia sana mpaka siku ya kufa kwangu kwa vitendo anavyofanya sasa hivi bora ITV na Star TV ambazo ni mali ya watu lakini hawana ghiriba kama ilivyo TV ya walipa kodi taarifa ilichukua dakika nne mkutano wake wa KIlombero ulionyweshwa kwa sekunde sitini tuu.
 
Unajua Tido Mhando kwa kimombo anaitwa "boot licker!" anatia kichefuchefu ndio maana hata Marin Hassan alikoswakoswa mkongoto kwenye uzinduzi wa kampeni ya Chadema
 
Tido Mhando kakosa kabisa uzalendo bado anawaabudu watu wanaotafuna fedha zetu za umma na kula rushwa hadi wanajitapikia.
 
Hivi tatizo la Maji maeneo ya Kimara n aibu ya nani? Na Wilaya nzima ya Bagamoyo?
 
Tido Mhando na wafanyakazi wengine wa TBC ni waelevu, tatizo ni kwamba wamekubali kupewa amri na wapumbavu na kwa hofu yao wanakubali amri za wapumbavu ili mkono wao uingie kinywani. Hapo wafanyakazi wana nafsi mbili, nafsi ya kwanza inamwambia kwamba what they are doing is wrong na nyingine inamwambia akubali amri za wapumbavu ili maisha yasogee. Watu wenye nafsi mbili God has already reserved a prominent place in hell for them.
 
Jana jioni niliangalia taarifa ya habari ya TBC1 nakuona jinsi hii TV ya uma ilivyo chafu! Walitoa habari ya ukosefu wa maji katika mjini wa Karatu. Ni aibu sana TV ya uma inayoongozwa na mtu aliyepata "exposure" ya jinsi vyombo vya uma vya wenzetu vinavyoendeshwa, yeye anafanya kinyume!
Hii habari ilikuwa ni kumchafua Dr. Slaa na Chadema kwa ujumla
[/B]

sasa mkulu sasa ulitaka wadanganye !! wafuasi wa chadema acheni kujistukia hivo! hahaha
 
Back
Top Bottom