Jana jioni niliangalia taarifa ya habari ya TBC1 nakuona jinsi hii TV ya uma ilivyo chafu! Walitoa habari ya ukosefu wa maji katika mjini wa Karatu. Ni aibu sana TV ya uma inayoongozwa na mtu aliyepata "exposure" ya jinsi vyombo vya uma vya wenzetu vinavyoendeshwa, yeye anafanya kinyume!
Hii habari ilikuwa ni kumchafua Dr. Slaa na Chadema kwa ujumla. Hivi jamani ukosefu wa maji katika nchi hii ni habari kweli? haya ni maisha ya kila siku. Dar ni sehemu ngapi maji yanatoka muda wote, watu wasichote kwa madumu kutoka mbali? Kwa nini iwe habari kwa Karatu?
Ushauri wangu mafisadi wa nchi hii, mwisho wenu hauko mbali. Tumieni tu ulafi wa akina Tido Mhando na wengineo kwa maslahi yenu, lakini mjue wazalendo inatuuma na ipo siku tutaikomboa nchi yetu. Wakuu wa vyombo vya uma na wote wale wenye dhamana kama hizo, muogopeni Mungu----watanzania wamedhulumiwa sana kwa kitendo cha ninyi kuabudu mafisadi na kutumia dhamana hizo kwa maslahi yenu binafsi.
Nalaani kitendo hicho kiovu cha TBC1, kodi zetu mnatumia kwa manufaa ya mafisadi!
Mwanza kuna maeneo kibao maji yanatoka usiku tu kuanzia saa sita hadi saa kumi na moja, ziwa liko karibu! hilo ccm haliwanyimi usingizi isipokuwa wanataka kuonyesha watz hata karatu ni hovyo.
CCM toka ikulu wanazlendo tujenge nchi. Muone kama hatujaendelea mbele.
Mimi natumia king'amuzi chao lakini channel za TBC1 na TBC2 nimeweka ktk PG (parental Guide). hakuna ruhusa kuangalia na sijampa mtu password.
Jana jioni niliangalia taarifa ya habari ya TBC1 nakuona jinsi hii TV ya uma ilivyo chafu! Walitoa habari ya ukosefu wa maji katika mjini wa Karatu. Ni aibu sana TV ya uma inayoongozwa na mtu aliyepata "exposure" ya jinsi vyombo vya uma vya wenzetu vinavyoendeshwa, yeye anafanya kinyume!
Hii habari ilikuwa ni kumchafua Dr. Slaa na Chadema kwa ujumla[/B]
Mimi natumia king'amuzi chao lakini channel za TBC1 na TBC2 nimeweka ktk PG (parental Guide). hakuna ruhusa kuangalia na sijampa mtu password.