TBC Mnakera sana!

TBC Mnakera sana!

edinajailos

Member
Joined
Oct 2, 2012
Posts
22
Reaction score
18
Jamani hiki Chombo cha utangazaji kinachojiita Cha Umma kimepoteza sifa ni bora kiitwe chombo cha CCM.Nasema hivyo kwa sababu hakitendi haki kwa watanzania kwa mfano vipindi vingi vya mahojiano kama Jambo asubuhi wanaohojiwa ni makada wa CCM hasa ktk Mchakato wa katiba mpya.Wanachokifanya wanachukua kada wa CCM na wajumbe wale 201 ambao ni makada wa CCM mfano Kingunge na kuanza kuendesha mdahalo juu ya katiba mpya.Jambo ambalo linakuwa limeegemea upande mmoja.

Mie Sina chama lkn kitendo hiki kinachofanywa na TBC hakikubaliki kwani hili shirika linaendeshwa kwa kodi zetu ikiwamo kodi yangu.Mfano mzuri ni hotuba ya Rais aliyoitoa wakati wa kufungua bunge imerudiwa zaidi ya mara kumi,cha kushangaza hotuba ya jaji warioba haikurudiwa kama ya rais,wakati ya warioba ndiyo ilibeba sauti kuu ya watanzania. Hata taarifa za habari ziko katika mlengo wa CCM.Sikatai kuwa hotuba ya rais isirushwe bali ninachokisema ni kuwa kuwe na msawazo ktk kurusha habari.Igeni mfano wa STAR TV na ITV wanajitahidi kuweka check and balance ktk midahalo yao.

Napendekeza hiki chombo kibadilishwe jina na kisiwe Shirika la Utangazaji la Taifa maana hakibebi maudhui ya watanzania bali kinabeba maudhui ya kisiasa zaidi.

-------------

Katika kipindi cha redio cha ‘Leo Katika Bunge' ambacho katika bunge hili maalumu la katiba kinaitwa ‘Katiba Tuitakayo', kinachorekodiwa na kurushwa na TBCCM kuanzia saa 3:00 hadi saa 4:00 usiku, mtangazaji wa TBCCM anayerekodi kipindi hiki kutoka bungeni Dodoma ameacha kwa makusudi kabisa kurekodi michango iliyotolewa na Juma Duni Haji, pamoja na Eng. Habibu Mnyaa waliotoa maoni ya kundi la watu wachache! Lakini maoni yote yaliyotolewa na wabunge wa CCM, hata kama ya kipuuzi, yamepewa airtime ya kutosha.

Haya ni makusudi kabisa yanayofanywa na chombo hiki kilichopo chini ya CCM ambacho huendeshwa kwa kodi za wananchi. Wanalenga kuwanyima wananchi habari sahihi juu ya watetezi wa maoni yao waliyoyatoa kwenye rasimu ya katiba hii inayojadiliwa. Inaonekana ripota wa kipindi hiki amepewa maelekezo maalumu na CCM kuhusu michango ya wabunge anyopaswa kuirekodi na kuirusha hewani, lengo likiwa kuwapumbaza na kuwahadaa wananchi juu ya usaliti unaofanywa na wabunge wa CCM katika kusigina maoni ya wananchi yaliyomo kwenye rasimu ya katiba.

Haiingii akilini kuona kwamba CCM wanafanya makusudi kuwanyima wananchi habari na kuwaacha wabakie mbumbumbu ili waendelee kuwatawala, kuwakandamiza, kuwanyonya na kuwamasikinisha. Raia wanakosa huduma muhimu za kijamii kama vile huduma za afya, shule, maji, barabara, nk kwa kisingizio kwamba hakuna fedha, kumbe fedha zinatumika kuendesha kituo cha redio ambacho hakina manufaa yoyote kwa wananchi. Ni bora vituo vya redio na tv vya TBCCM Taifa na TBCCM1 vifungwe kwani havina faida yoyote kwa wananchi.

habari wana jm f,nadhani Watanzania wengi sasa wanafatilia Bunge la Katiba, na kwa sasa ni TBC pekee ambao wanarusha matangazo ya bunge hili moja kwa moja (sijui kwa nini TV zingine hazirushi matangazo ya bunge hili live) ila ,kwa kitendo walichofanya jana cha kutukatia matangazo nadhani kwa watu makini hakikubaliki na si tu hakikubaliki bali hakivumiliki na si cha kukifumbia macho hata kidogo. Haiwezekani kituo ambacho kinajinasibu kuwa ni cha taifa kikawa kinafanya mambo ambao tunayaona kabisa yanamlengo tofauti, si kazi yake chombo hiki kuwafanya watanzania wamsikilize nani na nani wasimsikilize ,si kazi yake kuwachagulia watanzania kitu cha kusikiliza na si kazi yake kufanya siasa,kama ambavyo hakipaswi kuonekana kinaunga mkono chama au kikundi chochote hasa katika swala la kutunga katiba ya nchi. Cha kushangaza chombo hiki cha TBC moja kwa moja kinaonekana kuwa upande wa CCM kwa kila jambo,na kimefikia hatua ya kukata matangazo pale tu watu wanaotoa hoja zinazopingana na CCm wanapowakilisha hoja zao,hii inaonyesha kuwa mchezo huu si huru kama unavyopaswa kuwa.

TUKUMBUKE KUWA WALIMFUKUZA TIDO MHANDO KWA SABABU TU ALIENDELEA NA MPANGO WA KUENDESHA KIPINDI CHA MCHAKATO MAJIMBONI-kwake haikuwa rahisi kukisitisha kwa kuwa walishahafikiana na shirika la BBC ambao waliwezesha kipinde kile kiwe hewani lakini kwa kuwa watu wa chama flani waliona hakina masirahi kwao wakamkataza kukirusha japo kwa kuwa yeye ni msafi alikirusha na yaliyomkuta wote tunajua.

SASA WAKATI WA KULALAMA NADHANI UMEPITA..Watanzania ambao kodi zetu zinaendesaha kituo hiki tunapaswa kuchukua hatua stahiki ili waelewe kwa vitendo kuwa tumechoka na vitendo vyao vya KIZANDIKI,KISHENZI,KIJUHA NA MANENO YOTE MABAYA WANAYOLANDANA NAO. TUELEWE KUWA WANAJUA KUWA HATUPENDI, ILA WANAFANYA KWA KIBURI KUWA TUTAFANYA NINI ,SASA TUWAONYESHE KUWA TUNAWEZA FANYA KITU JUU YAO.

NINATOA WAZO HILI HILI KWA MTU ANAYEWEZA KUTUPA USHAURI NA ITAKUWA VIZURI KAMA UKIWA WA KISHERIA NA KAMA HAKUNA JAPO TUAMBIANE NINI CHA KUFANYA ..BINAFSI NAWAZA KUANDAMANA PAKA OFISI ZA tbc NA MABANGO YENYE JUMBE MBALIMBALI JUU YA KERO HII..HII ITASAIDIA KWA KUWA WAANDISHI WA TV MAKINI KAMA itv, star tv,na waandishi wa magazeti kama ----- na MwanaNchi na wengineo watarusha habari hii na hii itakuwa aibu kubwa kwao.
kisha maandamano hayo yataelekea vituo vya ITV na STAR TV kuwalaumu kwa nini wanatuacha watanzania katika kutupa habari za bunge la katiba wakati wao ndio tegemeo letu na wao ndio tunaowategemea kama vituo vya TAIFA.

Kama tunaweza kuwasiliana na vyombo vingine kama watu wa HAKI ZA BINADAMU katika kupigania hili kwani habari ni moja ya haki zetu za msingi.

JAMANI HAYA NI MAWAZO YANGU NAOMBA MICHANGO YA KUFANIKISHA HILI. NA KAMA KUNA MTU ANAWEZA NIPA NAMBA YA MTU NAYEWEZA KUWASILIANA NAE KATIKA KULIWEZESHA HILI TAFADHARI NAOMBA.

na kama una kitu muhimu juu la hili na ungependa hiwe siri basi ni PM

nawakilisha wana jamii f.

bajar musica gratis
 
TBC imejaaa kunguni na mende.. Ukiwa Professional kama Mhando unaonekana adui.. Siasa ilibidi ziwe kwa maslahi ya taifa mfano tatizo la Rwanda na Tanzania sasa wao wanaleta siasa zenye kufisha maslahi ya taifa.. ila maslahi ya kikundi flani. Halaf ndo tunaambiwa kauli mbiu iwe Tanzania kwanza.. Mbona wao wanafanya Tanzania baadae...?? Tunatengeneza taifa la wasaliti na watoto wetu watajifunza usaliti..
 
nakupa pole kwa kuwa na moyo wa kuendelea kuangalia icho kituo, mie nilishaacha kukiangalia siku nyingi, acha wale kodi yangu kwa upuuzi wao wa kuegemea upande mmoja ila nilishawatoa kwenye mawazo yangu, bora niangalie zangu vituo vingine vya habari, kuangalia TBC ni sawa na kusoma gazeti la habari leo hakuna jipya zaidi ya kujipendekeza kwa serikali hata kwenye mambo ya msingi ambayo watanzania wanataka waone mawazo ya aina zote ili kupima hoja za msingi na kufanya maamuzi sahihi.
 
Duh kumbe hili linagusa wengi, kwakweli TBC wanatuma kufanya kampeni za CCM kwenye mchakato wameenda mbali zaidi hata watu wanaojidai kuwahoji mitaani nao ni CCM. Kiukweli wanashindwa/kwa makusudi hawataki ku balance story. Hovyooo, tena bora yule cjui nani aliekuwepo mwanzoni kwenye kipindi cha jambo Dodoma alikuwa anahoji maswali ambayo CCM wanatakiwa kujibu.

Lakini huyu Mama ni kama sanamu kaletwa pale hana mbele wala nyuma, huu wizi wa kodi zetu kuna siku mtazilipa bila kupenda.
 
naipongeza sana tbc kwa vipindi vyake murwaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa, sio kama tv station zingine vipindi vyao ovyoooooo
 
Umechelewa kulibaini ndugu,ila afadhali umegundua.tukisema tunaonwa sisi ni cdm,hawajui kuwa tunataka kupata maoni ya upande mwingine pia
 
Jamani hiki Chombo cha utangazaji kinachojiita Cha Umma kimepoteza sifa ni bora kiitwe chombo cha CCM.Nasema hivyo kwa sababu hakitendi haki kwa watanzania kwa mfano vipindi vingi vya mahojiano kama Jambo asubuhi wanaohojiwa ni makada wa CCM hasa ktk Mchakato wa katiba mpya.Wanachokifanya wanachukua kada wa CCM na wajumbe wale 201 ambao ni makada wa CCM mfano Kingunge na kuanza kuendesha mdahalo juu ya katiba mpya.Jambo ambalo linakuwa limeegemea upande mmoja.
Mie Sina chama lkn kitendo hiki kinachofanywa na TBC hakikubaliki kwani hili shirika linaendeshwa kwa kodi zetu ikiwamo kodi yangu.Mfano mzuri ni hotuba ya Rais aliyoitoa wakati wa kufungua bunge imerudiwa zaidi ya mara kumi,cha kushangaza hotuba ya jaji warioba haikurudiwa kama ya rais,wakati ya warioba ndiyo ilibeba sauti kuu ya watanzania. Hata taarifa za habari ziko katika mlengo wa CCM.Sikatai kuwa hotuba ya rais isirushwe bali ninachokisema ni kuwa kuwe na msawazo ktk kurusha habari.Igeni mfano wa STAR TV na ITV wanajitahidi kuweka check and balance ktk midahalo yao.
Napendekeza hiki chombo kibadilishwe jina na kisiwe Shirika la Utangazaji la Taifa maana hakibebi maudhui ya watanzania bali kinabeba maudhui ya kisiasa zaidi.
huna hoja, zaidi unalalamika tu
 
Jamani hiki Chombo cha utangazaji kinachojiita Cha Umma kimepoteza sifa ni bora kiitwe chombo cha CCM.Nasema hivyo kwa sababu hakitendi haki kwa watanzania kwa mfano vipindi vingi vya mahojiano kama Jambo asubuhi wanaohojiwa ni makada wa CCM hasa ktk Mchakato wa katiba mpya.Wanachokifanya wanachukua kada wa CCM na wajumbe wale 201 ambao ni makada wa CCM mfano Kingunge na kuanza kuendesha mdahalo juu ya katiba mpya.Jambo ambalo linakuwa limeegemea upande mmoja.
Mie Sina chama lkn kitendo hiki kinachofanywa na TBC hakikubaliki kwani hili shirika linaendeshwa kwa kodi zetu ikiwamo kodi yangu.Mfano mzuri ni hotuba ya Rais aliyoitoa wakati wa kufungua bunge imerudiwa zaidi ya mara kumi,cha kushangaza hotuba ya jaji warioba haikurudiwa kama ya rais,wakati ya warioba ndiyo ilibeba sauti kuu ya watanzania. Hata taarifa za habari ziko katika mlengo wa CCM.Sikatai kuwa hotuba ya rais isirushwe bali ninachokisema ni kuwa kuwe na msawazo ktk kurusha habari.Igeni mfano wa STAR TV na ITV wanajitahidi kuweka check and balance ktk midahalo yao.
Napendekeza hiki chombo kibadilishwe jina na kisiwe Shirika la Utangazaji la Taifa maana hakibebi maudhui ya watanzania bali kinabeba maudhui ya kisiasa zaidi.

kwanzia hii siku niliwaogopa tbccm
 

Attachments

  • 954792_645536985501218_735193061_n.jpg
    954792_645536985501218_735193061_n.jpg
    10.1 KB · Views: 326
Pole ndg mimi nilishasau kama kuna chanel inaitwa TBC, tangu wasitishe mchakato majimboni kama wewe bado unaangalio uko ulimwengu wa giza totoro wajanja tunaamka na Tuongee asubuhi na star TV Baada ya hapo tuangalia taarifa motomoto na ITV daimad
 
Na nyie mmezidi uchokozi, mtu makini kama wewe unatafuta nini tbc? Mimi na familia yangu vipindi pekee tunavyo angalia tbc ni hivi hapa, Ze comedy, chereko na bunge basi kabla na baada ya hapo mwendo ni super brand, Channel 10 na Star Tv basi, vinginevyo maigizo toka Nigeria!
 
Pole ndugu,

Bado unaangalia TBC? Mm nilishaacha muda mrefu saana. tafuta vituo vya maana uangalie..


Jamani hiki Chombo cha utangazaji kinachojiita Cha Umma kimepoteza sifa ni bora kiitwe chombo cha CCM.Nasema hivyo kwa sababu hakitendi haki kwa watanzania kwa mfano vipindi vingi vya mahojiano kama Jambo asubuhi wanaohojiwa ni makada wa CCM hasa ktk Mchakato wa katiba mpya.Wanachokifanya wanachukua kada wa CCM na wajumbe wale 201 ambao ni makada wa CCM mfano Kingunge na kuanza kuendesha mdahalo juu ya katiba mpya.Jambo ambalo linakuwa limeegemea upande mmoja.
Mie Sina chama lkn kitendo hiki kinachofanywa na TBC hakikubaliki kwani hili shirika linaendeshwa kwa kodi zetu ikiwamo kodi yangu.Mfano mzuri ni hotuba ya Rais aliyoitoa wakati wa kufungua bunge imerudiwa zaidi ya mara kumi,cha kushangaza hotuba ya jaji warioba haikurudiwa kama ya rais,wakati ya warioba ndiyo ilibeba sauti kuu ya watanzania. Hata taarifa za habari ziko katika mlengo wa CCM.Sikatai kuwa hotuba ya rais isirushwe bali ninachokisema ni kuwa kuwe na msawazo ktk kurusha habari.Igeni mfano wa STAR TV na ITV wanajitahidi kuweka check and balance ktk midahalo yao.
Napendekeza hiki chombo kibadilishwe jina na kisiwe Shirika la Utangazaji la Taifa maana hakibebi maudhui ya watanzania bali kinabeba maudhui ya kisiasa zaidi.
 
Na nyie mmezidi uchokozi, mtu makini kama wewe unatafuta nini tbc? Mimi na familia yangu vipindi pekee tunavyo angalia tbc ni hivi hapa, Ze comedy, chereko na bunge basi kabla na baada ya hapo mwendo ni super brand, Channel 10 na Star Tv basi, vinginevyo maigizo toka Nigeria!
Wewe unaakili nyingi sana sana MUNGU akupe ujasili zaidi fata njia kuu acha tbccm
 
Back
Top Bottom