edinajailos
Member
- Oct 2, 2012
- 22
- 18
Jamani hiki Chombo cha utangazaji kinachojiita Cha Umma kimepoteza sifa ni bora kiitwe chombo cha CCM.Nasema hivyo kwa sababu hakitendi haki kwa watanzania kwa mfano vipindi vingi vya mahojiano kama Jambo asubuhi wanaohojiwa ni makada wa CCM hasa ktk Mchakato wa katiba mpya.Wanachokifanya wanachukua kada wa CCM na wajumbe wale 201 ambao ni makada wa CCM mfano Kingunge na kuanza kuendesha mdahalo juu ya katiba mpya.Jambo ambalo linakuwa limeegemea upande mmoja.
Mie Sina chama lkn kitendo hiki kinachofanywa na TBC hakikubaliki kwani hili shirika linaendeshwa kwa kodi zetu ikiwamo kodi yangu.Mfano mzuri ni hotuba ya Rais aliyoitoa wakati wa kufungua bunge imerudiwa zaidi ya mara kumi,cha kushangaza hotuba ya jaji warioba haikurudiwa kama ya rais,wakati ya warioba ndiyo ilibeba sauti kuu ya watanzania. Hata taarifa za habari ziko katika mlengo wa CCM.Sikatai kuwa hotuba ya rais isirushwe bali ninachokisema ni kuwa kuwe na msawazo ktk kurusha habari.Igeni mfano wa STAR TV na ITV wanajitahidi kuweka check and balance ktk midahalo yao.
Napendekeza hiki chombo kibadilishwe jina na kisiwe Shirika la Utangazaji la Taifa maana hakibebi maudhui ya watanzania bali kinabeba maudhui ya kisiasa zaidi.
-------------
Mie Sina chama lkn kitendo hiki kinachofanywa na TBC hakikubaliki kwani hili shirika linaendeshwa kwa kodi zetu ikiwamo kodi yangu.Mfano mzuri ni hotuba ya Rais aliyoitoa wakati wa kufungua bunge imerudiwa zaidi ya mara kumi,cha kushangaza hotuba ya jaji warioba haikurudiwa kama ya rais,wakati ya warioba ndiyo ilibeba sauti kuu ya watanzania. Hata taarifa za habari ziko katika mlengo wa CCM.Sikatai kuwa hotuba ya rais isirushwe bali ninachokisema ni kuwa kuwe na msawazo ktk kurusha habari.Igeni mfano wa STAR TV na ITV wanajitahidi kuweka check and balance ktk midahalo yao.
Napendekeza hiki chombo kibadilishwe jina na kisiwe Shirika la Utangazaji la Taifa maana hakibebi maudhui ya watanzania bali kinabeba maudhui ya kisiasa zaidi.
-------------
Katika kipindi cha redio cha ‘Leo Katika Bunge' ambacho katika bunge hili maalumu la katiba kinaitwa ‘Katiba Tuitakayo', kinachorekodiwa na kurushwa na TBCCM kuanzia saa 3:00 hadi saa 4:00 usiku, mtangazaji wa TBCCM anayerekodi kipindi hiki kutoka bungeni Dodoma ameacha kwa makusudi kabisa kurekodi michango iliyotolewa na Juma Duni Haji, pamoja na Eng. Habibu Mnyaa waliotoa maoni ya kundi la watu wachache! Lakini maoni yote yaliyotolewa na wabunge wa CCM, hata kama ya kipuuzi, yamepewa airtime ya kutosha.
Haya ni makusudi kabisa yanayofanywa na chombo hiki kilichopo chini ya CCM ambacho huendeshwa kwa kodi za wananchi. Wanalenga kuwanyima wananchi habari sahihi juu ya watetezi wa maoni yao waliyoyatoa kwenye rasimu ya katiba hii inayojadiliwa. Inaonekana ripota wa kipindi hiki amepewa maelekezo maalumu na CCM kuhusu michango ya wabunge anyopaswa kuirekodi na kuirusha hewani, lengo likiwa kuwapumbaza na kuwahadaa wananchi juu ya usaliti unaofanywa na wabunge wa CCM katika kusigina maoni ya wananchi yaliyomo kwenye rasimu ya katiba.
Haiingii akilini kuona kwamba CCM wanafanya makusudi kuwanyima wananchi habari na kuwaacha wabakie mbumbumbu ili waendelee kuwatawala, kuwakandamiza, kuwanyonya na kuwamasikinisha. Raia wanakosa huduma muhimu za kijamii kama vile huduma za afya, shule, maji, barabara, nk kwa kisingizio kwamba hakuna fedha, kumbe fedha zinatumika kuendesha kituo cha redio ambacho hakina manufaa yoyote kwa wananchi. Ni bora vituo vya redio na tv vya TBCCM Taifa na TBCCM1 vifungwe kwani havina faida yoyote kwa wananchi.
habari wana jm f,nadhani Watanzania wengi sasa wanafatilia Bunge la Katiba, na kwa sasa ni TBC pekee ambao wanarusha matangazo ya bunge hili moja kwa moja (sijui kwa nini TV zingine hazirushi matangazo ya bunge hili live) ila ,kwa kitendo walichofanya jana cha kutukatia matangazo nadhani kwa watu makini hakikubaliki na si tu hakikubaliki bali hakivumiliki na si cha kukifumbia macho hata kidogo. Haiwezekani kituo ambacho kinajinasibu kuwa ni cha taifa kikawa kinafanya mambo ambao tunayaona kabisa yanamlengo tofauti, si kazi yake chombo hiki kuwafanya watanzania wamsikilize nani na nani wasimsikilize ,si kazi yake kuwachagulia watanzania kitu cha kusikiliza na si kazi yake kufanya siasa,kama ambavyo hakipaswi kuonekana kinaunga mkono chama au kikundi chochote hasa katika swala la kutunga katiba ya nchi. Cha kushangaza chombo hiki cha TBC moja kwa moja kinaonekana kuwa upande wa CCM kwa kila jambo,na kimefikia hatua ya kukata matangazo pale tu watu wanaotoa hoja zinazopingana na CCm wanapowakilisha hoja zao,hii inaonyesha kuwa mchezo huu si huru kama unavyopaswa kuwa.
TUKUMBUKE KUWA WALIMFUKUZA TIDO MHANDO KWA SABABU TU ALIENDELEA NA MPANGO WA KUENDESHA KIPINDI CHA MCHAKATO MAJIMBONI-kwake haikuwa rahisi kukisitisha kwa kuwa walishahafikiana na shirika la BBC ambao waliwezesha kipinde kile kiwe hewani lakini kwa kuwa watu wa chama flani waliona hakina masirahi kwao wakamkataza kukirusha japo kwa kuwa yeye ni msafi alikirusha na yaliyomkuta wote tunajua.
SASA WAKATI WA KULALAMA NADHANI UMEPITA..Watanzania ambao kodi zetu zinaendesaha kituo hiki tunapaswa kuchukua hatua stahiki ili waelewe kwa vitendo kuwa tumechoka na vitendo vyao vya KIZANDIKI,KISHENZI,KIJUHA NA MANENO YOTE MABAYA WANAYOLANDANA NAO. TUELEWE KUWA WANAJUA KUWA HATUPENDI, ILA WANAFANYA KWA KIBURI KUWA TUTAFANYA NINI ,SASA TUWAONYESHE KUWA TUNAWEZA FANYA KITU JUU YAO.
NINATOA WAZO HILI HILI KWA MTU ANAYEWEZA KUTUPA USHAURI NA ITAKUWA VIZURI KAMA UKIWA WA KISHERIA NA KAMA HAKUNA JAPO TUAMBIANE NINI CHA KUFANYA ..BINAFSI NAWAZA KUANDAMANA PAKA OFISI ZA tbc NA MABANGO YENYE JUMBE MBALIMBALI JUU YA KERO HII..HII ITASAIDIA KWA KUWA WAANDISHI WA TV MAKINI KAMA itv, star tv,na waandishi wa magazeti kama ----- na MwanaNchi na wengineo watarusha habari hii na hii itakuwa aibu kubwa kwao.
kisha maandamano hayo yataelekea vituo vya ITV na STAR TV kuwalaumu kwa nini wanatuacha watanzania katika kutupa habari za bunge la katiba wakati wao ndio tegemeo letu na wao ndio tunaowategemea kama vituo vya TAIFA.
Kama tunaweza kuwasiliana na vyombo vingine kama watu wa HAKI ZA BINADAMU katika kupigania hili kwani habari ni moja ya haki zetu za msingi.
JAMANI HAYA NI MAWAZO YANGU NAOMBA MICHANGO YA KUFANIKISHA HILI. NA KAMA KUNA MTU ANAWEZA NIPA NAMBA YA MTU NAYEWEZA KUWASILIANA NAE KATIKA KULIWEZESHA HILI TAFADHARI NAOMBA.
na kama una kitu muhimu juu la hili na ungependa hiwe siri basi ni PM
nawakilisha wana jamii f.
bajar musica gratis