TBC Inachakachua Mpaka Taarifa za kiSerikali

TBC Inachakachua Mpaka Taarifa za kiSerikali

Dar_Millionaire

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2008
Posts
227
Reaction score
89
Sasa hivi katika majumuisho ya bajeti ya wizara ya ujenzi Mh. Aden Rage ameuliza, "Jana nilisikia TBC kwenye taarifa ya habari ya saa mbili usiku kuwa makandarasi wa barabara mkoani Tabora wamegoma kwa sababu ya kucheleweshewa malipo. Namuomba mheshimiwa waziri au naibu waziri [wa ujenzi] atoe kauli kuhusu hilo"

Naibu waziri akaeleza kuwa hata yeye aliona taarifa hiyo kwenye TV ya TBC jana usiku. Hata hivyo alishangaa kuona Meneja wa Mkoa wa Tabora wa TANROADS akinukuliwa laivu kwenye hiyo taarifa ilhali meneja huyo yupo Dodoma na amekuwepo hapo Dodoma kwenye kikao cha Bunge kwa wiki mbili zilizopita.

Baada ya kuwasiliana na meneja wake huyo, ndipo ikabainika kuwa hiyo video ya kauli ya meneja ni ya miezi mitano iliyopita, TBC wame-cut na kupaste ili kutengeneza habari.

Waziri akamalizia kwa kutoa onyo kwa TBC waache ubabaishaji na kuipaka tope serikali.
 
Akiwa akimjibu mbunge wa tabora mjini naibu waziri wa ujenzi mwakyembe ameonya tbc 1 kuacha mara moja kuchakachua habari kama chombo cha serikali,tbc 1 jana walichakachua taarifa kwamba wakandarasi wamegoma kumbe ukweli wenyewe hiyo ilikuwa ni habari ya mwezi mei na kwamba hata mkandarasi waliyemuonyesha kwamba alikuwa anaelezea ugomaji wa wakandarasi hao alikuwepo dodoma kwa wiki nzima

my take kama tbc1 inawazushia wana ccm na serikali yao jee mangapi wametengeneza kuwaharibia watanzania walioko upinzani
tbc 1 ni kituo mfu hakifai kuendelea kuwepo kwa uongozi uliopo sasa
 
.............Mzimu wa Tido unaendelea kuwaandama....
 
Amewachana live waache taarifa za uongo kama vyombo vingine vya habari,aibu sana kwa chombo cha serikali kuumbuliwa bungeni
 
Wengine wakipakwa matope wao wanachekelea sasa kibao kikiwageukia wanapiga kelele.
 
Amewachana live waache taarifa za uongo kama vyombo vingine vya habari,aibu sana kwa chombo cha serikali kuumbuliwa bungeni
Yaani ni aibu tupu hembu fikiria habari wana cut and paste habari ya mwezi mei wanaifanya ya leo ,ukiangalia TBC1 wanatumika kwa propaganda walikuwa wanawasgusga hadhi mawaziri wa wizara hiyo huko CCM kunamgawanyiko wa ajabu sijapata kuiona chombo cha serikali kinatumika kuangusha bajeti ya wizara fulani,CCM lazima waondoke watatumbkiza nchi yetu kwenye janga kubwa sana tusipokuwa makini
 
tbc ni chombo cha serikali kama vyombo vingine vya serikali kinachosumbuliwa na utawala mbovu,tbc ya tildo ni tofauti na ya sasa.ushauri wa bure ni kubadili uongozi mzima wa tbc ili tuwe na shirika la habari la umma makini la linalo heshimu ueledi wa wafanyakazi wake.pamoja tunajenga taifa.
 
Nchi hii sio rahisi kubadili uongozi Wa tbc1 ndo maana Tido aliondolewa Hilo shirika si la umma bali ni la ccmagamba.
 
Hebu ngoja nisubiri taarifa ya habari ya saa2 ya TBC1 kama watairusha hiyo habari ya Mwakyeme.
 
TBC habari zao zinatia shaka katika umakini...
TBC cjui mnatumia vigezo gani katika kumchagua mtu wa kufanya nae mahojiano..?

Sasa cjui ni kwa faida ya Taifa au CCM...?

Daniel Mshana upo wapi?
ulipokabidhiwa kiti kw mbwembwe nyingu ulituahidi utayaendeleza yote mazuri aliyoyaanzisha Tido Mhando.... but now mambo ni kuelekea kuyumba...! ni ovyooo... tatizo nn ndg yetu mshana?

mifano:
leo mchana ktk taarifa yao ya habari baada ya bunge kuhairishwa, walimwonyesha mh mrema anazungumzia siasa majitaka badala
ya kuchangia hoja muhimu ktk wizara ya ujenzi!
TBC haikuonyesha wabunge wengine wa CCM na CDM waliotoa michango ya hoja nzuri, wananchi wapiga kura wao wakapata kuona kuliko kupoteza muda na mh mrema...!

Jioni hii Mjengoni Mhe Dr Mwakyembe amewa mind TBC kutokana na Taarifa ya Habari ya jana usiku ya Upotoshaji kuhusu kusema uongo
kuwa Contractors wote wa barabara wamegoma kufanya kazi zao mkoani Tabora! Mh N/Waziri alikuwa anajaribu kutoa ufafanuzi ktk swali aliloulizwa na Mh Rage Mb wa Tabora mjini....!

Katika hiyo Taarifa yao TBC wanadai walifanya mahojiano na Tan Roads Manager wa Tabora huko mjini Tabora... wakati Mh N/Waziri anajibu
swali la mb rage, amesema huyo Tanroad manager wa Tobara yupo Dodoma zaidi ya 2 weeks, ktk hiki kipindi cha bunge akihusika kuitayarisha bajeti ya Wizara husika!!!
Mh N/waziri alikanusha hilo.

TIDO MHANDO tunakukumbuka sana kwa ujuzi na uhodari wako enzi zako ulipokuwa TBC DG.....!
 
Mimi nilishaacha kuangalia tbc siku nyini
 
Tbc ya Tido ndo ilikua ya uma ya sasa ipo kwa ajili ya tabaka tawala yaani magamba.hvyo hapo hakuna cha ajabu sn kwani ni sawa na baba kumrekebisha mwanae anapokosea.sikilizia sasa watakavyokua na waoga kurepoti matukio.
 
Wana JF,

TBC imeingiliwa na Si Ha Sa siwaelewi hawa Serikali inataka nini hivi hawaoni haya mashirika yakiingiliwa na propaganda za si ha sa za CCM yanakufa mumeona viwanda vingi na uzembe wa utendaji kazi ndio hayo sasa yanaikuta TBC wasipo hangali utasikia TBC imebinafsishwa na itakuja kuwa kama ATCL haina hata ndege na Rwanda inawashinda kanchi kadogo kama mkoa wa Kagera kama alivyo sema kafulila
 
tbc habari zao zinatia shaka katika umakini...
Tbc cjui mnatumia vigezo gani katika kumchagua mtu wa kufanya nae mahojiano..?

Sasa cjui ni kwa faida ya taifa au ccm...?

Daniel mshana upo wapi?
Ulipokabidhiwa kiti kw mbwembwe nyingu ulituahidi utayaendeleza yote mazuri aliyoyaanzisha tido mhando.... But now mambo ni kuelekea kuyumba...! Ni ovyooo... Tatizo nn ndg yetu mshana?

Mifano:
Leo mchana ktk taarifa yao ya habari baada ya bunge kuhairishwa, walimwonyesha mh mrema anazungumzia siasa majitaka badala
ya kuchangia hoja muhimu ktk wizara ya ujenzi!
Tbc haikuonyesha wabunge wengine wa ccm na cdm waliotoa michango ya hoja nzuri, wananchi wapiga kura wao wakapata kuona kuliko kupoteza muda na mh mrema...!

Jioni hii mjengoni mhe dr mwakyembe amewa mind tbc kutokana na taarifa ya habari ya jana usiku ya upotoshaji kuhusu kusema uongo
kuwa contractors wote wa barabara wamegoma kufanya kazi zao mkoani tabora! Mh n/waziri alikuwa anajaribu kutoa ufafanuzi ktk swali aliloulizwa na mh rage mb wa tabora mjini....!

Katika hiyo taarifa yao tbc wanadai walifanya mahojiano na tan roads manager wa tabora huko mjini tabora... Wakati mh n/waziri anajibu
swali la mb rage, amesema huyo tanroad manager wa tobara yupo dodoma zaidi ya 2 weeks, ktk hiki kipindi cha bunge akihusika kuitayarisha bajeti ya wizara husika!!!
Mh n/waziri alikanusha hilo.

Tido mhando tunakukumbuka sana kwa ujuzi na uhodari wako enzi zako ulipokuwa tbc dg.....!

hii ndo serikali ya wachakachuzi usishsangae. Tunaambiwa nec ya magamba imeiamuru serikali ya magamba ishushe bei ya kerosiioni. Menyewe kwa menyewe. Ni kichekesho.
 
Kujipendekeza kwingi ndo kumewafikisha hapa mpaka wanakuwa kama mbwa koko...tbc is a corpse!!
 
TBC1 hawana wataalamu wa habari wamejaza yaleyale magalasha ya redio tanzania unategemea nini hapo? unakuta wanajipodoa mpaka wanaume mara wamevaa vitenge mara sijui hakuna lolote.
 
Sasa hivi katika majumuisho ya bajeti ya wizara ya ujenzi Mh. Aden Rage ameuliza, &quot;Jana nilisikia TBC kwenye taarifa ya habari ya saa mbili usiku kuwa makandarasi wa barabara mkoani Tabora wamegoma kwa sababu ya kucheleweshewa malipo. Namuomba mheshimiwa waziri au naibu waziri [wa ujenzi] atoe kauli kuhusu hilo&quot;<br />
<br />
Naibu waziri akaeleza kuwa hata yeye aliona taarifa hiyo kwenye TV ya TBC jana usiku. Hata hivyo alishangaa kuona Meneja wa Mkoa wa Tabora wa TANROADS akinukuliwa laivu kwenye hiyo taarifa ilhali meneja huyo yupo Dodoma na amekuwepo hapo Dodoma kwenye kikao cha Bunge kwa wiki mbili zilizopita.<br />
<br />
Baada ya kuwasiliana na meneja wake huyo, ndipo ikabainika kuwa hiyo video ya kauli ya meneja ni ya miezi mitano iliyopita, TBC wame-cut na kupaste ili kutengeneza habari.<br />
<br />
Waziri akamalizia kwa kutoa onyo kwa TBC waache ubabaishaji na kuipaka tope serikali.
<br />
<br />



mi coni tatzo, kwani "TUNAVUNA TULICHOPANDA" Ila Tanzania one day itakuja kuwa nchi bora!! Tutarudisha nyara zetu!
 
mbona saa mbili tbc hawajaitoa hii!lazima wajisafishe ili tujue nani mwongo,wao au n/waziri!maana hata mwakyembe anaweza aliktwa anajinasua!
 
Back
Top Bottom