Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Katika tukio la mauaji yaliyotokea Tarime (North Mara Mine) shirika la utangazaji la taifa limeonyesha mapungufu makubwa na kupoteza kabisa umuhimu wa kuwepo kwake, kwa siku mbili mfululizo wametoa kwenye taarifa zao za habari (prime time) za saa mbili kuhusu tukio hili lakini cha ajabu hakuna hata sehemu moja ambapo wamewapa fursa waathirika kueleza upande wao wa habari, kwa siku zote wamemnukuu Kagasheki na Kamanda wa polisi lakini hakuna sehemu yoyote ambapo wamewanukuu wanaotuhumiwa kuvamia mgodi ili nao watupe upande wao lakini hilo halijatokea.
Kwa mtazamo wangu TBC imegeuka kuwa chombo cha wanasiasa walioko madarakani (CCM) na si cha watanzania kama ambavyo sababu za kuundwa kwake zinaeleza, kwa hiyo uendeshaji wa chombo hiki kuendelea kugharimiwa na watanzania wote ni UFISADI, ni bora basi CCM wakakichukua na kulipia uendeshaji wake kwa sababu kinaendeshwa kwa matakwa ya CCM siyo watanzania wote!
Kwa mtazamo wangu TBC imegeuka kuwa chombo cha wanasiasa walioko madarakani (CCM) na si cha watanzania kama ambavyo sababu za kuundwa kwake zinaeleza, kwa hiyo uendeshaji wa chombo hiki kuendelea kugharimiwa na watanzania wote ni UFISADI, ni bora basi CCM wakakichukua na kulipia uendeshaji wake kwa sababu kinaendeshwa kwa matakwa ya CCM siyo watanzania wote!