Elections 2010 TBC 1 na mbinu ya kuchakachua hoja za Slaa (PhD)

Mzito Kabwela

JF-Expert Member
Nov 28, 2009
18,857
7,615
Natazama TBC,

Wamemtafuta mwanzilishi wa kiwanda cha Tanga Cement ili ajibu kama Cement inaweza kuuzwa kwa shilingi elfu tano kwa mfuko mmoja kama asemavyo Wilbrod Slaa(PhD). Kwa mujibu wa mzungu huyo aliyehojiwa ni kuwa anachokisema Slaa(PhD) hakiwezekani kwa sababu kusafirisha mfuko mmoja hadi Mara ni shilingi 8,000/=.

Pia ikawepo habari nyingine kuwa GDP ya Tanzania imekuwa sana na changamoto pekee ni kuifanya ioane na hali halisi ya maisha ya mtanzania.

Nadhani lengo lao ni kuchakachua yale yote ambayo Slaa anayasema na ambayo yamempatia heshima kubwa.
 
Huyu mtaalam wauongo yaani wanatufanya sisi wajinga wanatuletea mzungu kichaa wanadai mwanzilishi wa simba cement,

na wanachokiongea hatukisikii huyu mzungu sio yule wapale Azam Takeaway.Huyu mwingine anasema pato la Tanzania

limepanda GDP alafu unashindwa kuonekana kwenye maisha ya mtanzania sasa sijui wanafanya nini hawa si waseme pato limeongezeka kwa mafisadi papa tu, Nawaomba TBC acheni kuonyesha habari zisizokuwa na tija kwa watanzania
 
Uyo mzungu ameandaliwa na CCM.

Alafu mbona wanakomaa na cement wakati alisema bati pia ni 5000 au wameona bati inawezekana ndo maana hawaifuatilii
Sasa uyo mtaalamu aambiwe kuwa cement inatoka all the way toka Pakistan na China na inauzwa Tz kwa tshs 9000 je why Tz ISHINDIKANE 5,000

Ukiboresha miundo Mbinu na kuwa na cheap source ya umeme ilo lawezekana
 
Wananchi wamechoshwa na mambo mengi,si makazi tu bali kila jambo linalogusa maisha yao.Watu wameshafanya maamuzi,hata kama angewekwa kikwete peke yake apigiwe ndiyo au hapana,angeshindwa tu.
 
Wanazungumzia kusafirisha cement ni gharama,hawajiulizi kwa nini ni gharama?Wavivu kufikiria ndio maana wana majibu mepesi.
Wakae pembeni wawaachie watu wanaojua kuzungusha vichwa.
 
Hivi wakuu mmekosa tv ya kuangalia hata muicheki hiyo biased tv? Bora hata uangalie kwaya ya atn au hata zile cartoons za tom and jerry!
 
Kama usafirishaji wa mfuko hapa mpaka shinyanga ni sh 8000 itakuwa je kuusafirisha kutoka china mpaka hapa? Mbona hiyo ya nje mapoja na umbali wa safari inayokaribia kuwa mara hamsini iliuzwa hapa Tz sh 9000?
Kwanza serikali inachukua ushuru wa bei gani kwenye diesel, vipuri, unit ya umeme, ushuru wa mauzo kwa huo mfuko, ushuru wa barabara nk? Hii serikali ndio muuaji namba moja wa raia zake.
Halafu nina wasiwasi na huyu mzungu, sii ndie huyu waliekuwa wanakula deal na EL kuiibia tanesco umeme?
 
Mzandiki mkubwa huyo. kwani Tanga kwenyewe Cement inauzwa shilingi ngapi?
 
huyo mzungu atafukuzwa kazi atawekwa mtanzania na bei itashuka mpaka shs.5000 kwani Wageni kazi yao ni kunyonya na sio kumnufaisha
Mtanzania.
 
mbona jibu ni rahisi jamani! anaposema 5,000 hana maana kwamba ni alfu tano kamili jamani, msikilizeni Dokta ana maana gani, kasema atafuta ushuru kwenye vifaa vya ujenzi. inaweza kufika 7,000 au 8,000 au any price. lakini nia yake ni kutoa kodi ya serikali.
 
natazama TBC,
wamemtafuta mwanzilishi wa kiwanda cha Tanga Cement ili ajibu kama Cement inaweza kuuzwa kwa shilingi elfu tano kwa mfuko mmoja kama asemavyo Wilbrod Slaa(PhD). Kwa mujibu wa mzungu huyo aliyehojiwa ni kuwa anachokisema Slaa(PhD) hakiwezekani kwa sababu kusafirisha mfuko mmoja hadi Mara ni shilingi 8,000/=.
Pia ikawepo habari nyingine kuwa GDP ya Tanzania imekuwa sana na changamoto pekee ni kuifanya ioane na hali halisi ya maisha ya mtanzania.

Nadhani lengo lao ni kuchakachua yale yote ambayo Slaa anayasema na ambayo yamempatia heshima kubwa.

Yani hiyo inaonesha jinsi gani CCM wamechoka hata kufikiria muda wote wao ni propaganda tu hata kwenye issue zinazohitaji utaaalam wao wanaleta propaganda tu, sasa kama wao hawawezi si wawaachie wenzao wanaoweza kushusha hiyo bei wanang'ang'ania nini???aiigrrrr
 
Hivi wakuu mmekosa tv ya kuangalia hata muicheki hiyo biased tv? Bora hata uangalie kwaya ya atn au hata zile cartoons za tom and jerry!

Hapo mkuu nakubaliana na wewe maana kuangalia TBC unaweza kuvunja TV yako mwenyewe
 
Ikitokea uchakachuaji wa kura za rais wetu by any mean ili asiende ikulu...wa kwanza kuchoma TBC nitakuwa mimi...natoa taarifa na aaliye na namba ya IGP Mwema anipatie nitoe taarifa rasmi. Nimekereka,nimechefuka, nimetapika na mpaka usawa huu ninia kichefuchefu na TBC Ziro. Pumbavu zao wote, hata huyo mkurugenzi nae paoja na kufanya kazi BBC kwa miaka yote hiyo bureeeeeeeeeee kabisa.
 
Ndo kazi yao kusema kila kitu hakiwezekani' wawapishe wanaoweza.. ambao tunaamini wataweza au watajaribu kubadilisha hali mbaya iliyopo
 
Wanatumia vyombo vya dola kujibu hoja za kampeni. si waseme wenyewe??

Huyo mzungu achunguzwe kama kiwanda chake kinatimiza masharti ya uwekezaji maana anajibu kama amewekewa bunduki makalioni
 
Kama inshu ni usafiri ndio unaifanya cement kuwa ghali basi tuangalie pale kiwandani cement inapozalishwa, Je cement inapatikana kwa bei nafuu zaidii!!?
Tanga: ........
Mbeya:........
Mbona hata palepale getini kiwandani cement haipatikani kwabei ya chini!!!!????? KUlikoni kuisingizia garama ya usafirishaji!!!? Nafikiri hapa TBC1 wametuona sisi watanzania ni mazuzu, wepesi wa kudanganyika, Watu tunaopapatika juu ya wazungu, wametuona sisi ni watu rahisirahisi tu, tusioweza kufikiri wala kuchanganua jambo. Huu ni upuuzi.


  • Tanzania ndiyo nchi pekee duniani inayoongoza kwa kuuza umeme kwa bei ghali....... [source: umoja wa mataifa, maendeleo ya makazi]
  • Viwanda vya cement ndio moja ya viwanda vinavyoongoza kwa kutumia umeme mwingi zaidi..........[source: Report ya serekali, wizara ya nishati na madini]
  • Ushuru............ [Source: Ufahamu wa kawaida]
  • Miundo mbinu mibovu............[Source: Huhitaji liko wazi]
Nafikiri hizo zingekuwa points katika kutetea uwepo wa bei kubwa kwa mfuko moja wa cement na si kumu_attack Dr SLAA kwa hoja zake na kizipinga bila hata ya kufanya analysis. Nafikiri kwa mtu yeyote akirekebisha hayo mambo kwenye hizo bullets hapo juu haina pingamizi kuwa cement itakuwa chini kwa vyovyote vile. Sasa suala lakutokuwezekana linatoka wapi????? Idiot.
 
Back
Top Bottom