wapendwa, mimi ni mtanzania nimekaa nje ya nchi(ulaya) kwa muongo mmoja. nimeona hapalipi. nataka kurudi kwetu nije kujenga nchi yangu, kwani naamini mcheza kwao hutunzwa. ninataka kusafirisha mizigo yangu kwa njia ya container, lakini ninataka kuwa na uhakika haswa ni vitu gani ambavyo nitasamehewa kodi nisije nikabeba mauchafu halafu yakaniletea balaa. kiukweli nimechacha haswaa, ulaya noma, miaka yote hiyo nimefanya kazi lakini bills nazo zinakula pesa yote! sikuzamia, bali nilikuja na ninaondoka kiustaarabu!