Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,211
- 113,520
Hapo zamani niliwahi kutoka na msichana mmoja aitwaye Crystal. Nilikutana naye akiwa pre-med student na lengo lake lilikuwa ni kwenda medical school na baadaye kuja kuwa daktari wa watoto.
Sijui hawa mademu wasomi wasomi nilikuwa nawapataje tu maana elimu yangu mwenzenu hapa ni ya ngumbaru.
Basi bana siku moja akanijia na wazo la kujichora tattoo. Mimi nikamhoji anataka kujichora tattoo ya nini na wapi. Akasema anataka kujichora tattoo ya mkuki moyoni halafu juu yake ajichore jina langu: Nyani Ngabu.
Nilimshangaa na nikabaki nimeduwaa. Binafsi siyahusudishi kabisa matattoo. Sielewi kwa nini watu wanajichora. Kwangu naona kama naharibu tu ngozi yangu na likitu ambalo halifutiki (well, siku hizi kuna teknolojia za kufuta hizo tattoo lakini ni bei mbaya sana). Ukija kulichoka hilo litattoo utafanya nini? Aaah kila mtu na maamuzi yake na sipingi wengine kujichora. Ni kwamba tu mimi hapana. Sitaki huo uchafu.
Basi siku moja mimi niko ndani naangalia telly naye Crystal huyo akaingia. Akanisalimia na kunikumbatia mimi asali wake. Akaniambia ametoka kuchorwa ile tattoo aliyoniambia anataka kuchora. Nikamwuliza iko wapi hiyo tattoo. Akafungua vifungo vya blauzi yake na akanionyesha katikati kwenye titi lake la kushoto.....mkuki moyoni na jina langu - Nyani Ngabu kwa juu yake.
Sikutaka kumhoji sana lakini kichwani nikawa najisemea mwenyewe hivi huyu anajua kweli anachokifanya? Kwanza umeenda kuharibu mwili wako na kitu ambacho hakifutiki, pili unaandika jina langu huku huna uhakika kama tutakuwa pamoja milele.....nikatikisa kichwa na nikajinyamazia nisije onekana mpinga maendeleo au mpinga vitu ambavyo wengine wanapenda.
Baadaye tukaja kuachana na kila mtu akaenda kivyake. Nina uhakika kabisa baada ya mimi alitoka na njemba zingine. Heheheheee....kila nikifikiria kuwa hizo njemba wakati zinatomasa tomasa matiti yake zilikuwa zinaona jina langu....basi kila nikifikiria hivyo kichwa changu kinaongezeka ukubwa na sijui kwa nini.
Nimekutana tena na Crystal wiki hii na tumeongelea mambo mengi ikiwamo hiyo tattoo. Kasema bado anayo na hajutii kujichora. Sasa sijui nielewe vipi?
Sijui hawa mademu wasomi wasomi nilikuwa nawapataje tu maana elimu yangu mwenzenu hapa ni ya ngumbaru.
Basi bana siku moja akanijia na wazo la kujichora tattoo. Mimi nikamhoji anataka kujichora tattoo ya nini na wapi. Akasema anataka kujichora tattoo ya mkuki moyoni halafu juu yake ajichore jina langu: Nyani Ngabu.
Nilimshangaa na nikabaki nimeduwaa. Binafsi siyahusudishi kabisa matattoo. Sielewi kwa nini watu wanajichora. Kwangu naona kama naharibu tu ngozi yangu na likitu ambalo halifutiki (well, siku hizi kuna teknolojia za kufuta hizo tattoo lakini ni bei mbaya sana). Ukija kulichoka hilo litattoo utafanya nini? Aaah kila mtu na maamuzi yake na sipingi wengine kujichora. Ni kwamba tu mimi hapana. Sitaki huo uchafu.
Basi siku moja mimi niko ndani naangalia telly naye Crystal huyo akaingia. Akanisalimia na kunikumbatia mimi asali wake. Akaniambia ametoka kuchorwa ile tattoo aliyoniambia anataka kuchora. Nikamwuliza iko wapi hiyo tattoo. Akafungua vifungo vya blauzi yake na akanionyesha katikati kwenye titi lake la kushoto.....mkuki moyoni na jina langu - Nyani Ngabu kwa juu yake.
Sikutaka kumhoji sana lakini kichwani nikawa najisemea mwenyewe hivi huyu anajua kweli anachokifanya? Kwanza umeenda kuharibu mwili wako na kitu ambacho hakifutiki, pili unaandika jina langu huku huna uhakika kama tutakuwa pamoja milele.....nikatikisa kichwa na nikajinyamazia nisije onekana mpinga maendeleo au mpinga vitu ambavyo wengine wanapenda.
Baadaye tukaja kuachana na kila mtu akaenda kivyake. Nina uhakika kabisa baada ya mimi alitoka na njemba zingine. Heheheheee....kila nikifikiria kuwa hizo njemba wakati zinatomasa tomasa matiti yake zilikuwa zinaona jina langu....basi kila nikifikiria hivyo kichwa changu kinaongezeka ukubwa na sijui kwa nini.
Nimekutana tena na Crystal wiki hii na tumeongelea mambo mengi ikiwamo hiyo tattoo. Kasema bado anayo na hajutii kujichora. Sasa sijui nielewe vipi?