Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,978
- 30,327
TATIZO LA MAJINA YA KIISLAM KATIKA HISTORIA YA VITA VYA MAJI MAJI
Ukisoma historia ya Vita Vya Maji Maji utakutana na jina Mkomanile.
Linaandikwa jina moja tu, ''Mkomanile.''
Kwa nini liandikwe jina moja tu?
Huyu ndiye mwanamke pekee katika majina karibu 67 ya mashujaa wa Vita Vya Maji Maji aliyenyongwa na kuzikwa katika kaburi la halaiki Mahenge Songea.
Huyu mwanamke jina lake ni Khadija Mkomanile.
Kwa nini jina la Khadija halikuandikwa?
Tuseme hawakulijua?
Ukisoma historia ya Maji Maji utasoma jina Chinyalanyala jina moja tu.
Kwa nini liandikwe jina moja tu?
Jina lake ni Omar Chinyalanyala.
Inawezekana kuwa jina la Omar hawakuifahamu?
Ukisoma historia ya Vita Vya Maji maji utasoma jina la Songea Mbano.
Hapa unasoma majina mawili jina moja halikutajwa.
Kwa nini jina lake la kwanza halikuandikwa lifahamike?
Huyu jina lake lake la kwanza ni Abdulraufu.
Hili jina Abdulraufu hawakulijua?
Kuna ''Kazembe'' lakini jina lakini la kwanza halipo.
Haya yanashangaza sana.
Kipande hicho hapo chini kinatoka katika kitabu cha Abdul Sykes:
''Kuelewa hali ya Uislam wakati ule, unahitaji kusoma barua iliyoandikwa na Chifu Songea bin Ruuf wakati alipokuwa akikusanya nguvu za raia wake dhidi ya majeshi ya Wajerumani na huku akijaribu kupata ushirika wa machifu wengine katika sehemu za kusini ya Tanganyika na ng'ambo ya Mto Ruvuma katika Msumbiji.
Barua hii aliyoandikiwa Sheikh, Sultan Mataka bin Hamin Massaninga anaandika (barua hii ipo katika herufi za Kiarabu):
Sultan Songea bin Ruuf anasema:
''Kwa Sheikh Sultan Mataka bin Hamin Massaninga.
Asalaam Aleikum,
Ninakuletea barua kupitia Kazembe.
Tumepata amri kutoka kwa Mwenyezi Mungu kuwa Wazungu lazima waondoke nchini.
Tupo katika kupigananao hapa.
Naamini tumeshapatana muda mrefu, (kwa hiyo) niletee wanao, ili tufanye ushirikiano.
Nilitaka kukuletea mifugo kama zawadi, lakini sipo katika hali ya kuweza kufanya hivyo, kwa kuwa vita ambavyo Mwenyezi Mungu amevitaka vinaendelea.
Niletee watumiaji bunduki mia moja, na niunge mkono katika kulivamia Boma (Songea).
Ninakuletea chupa ya Mtume Muhammad, ambayo ndani yake ipo nguvu ya kuwashinda Wazungu.
Usiwe na shaka nayo, ina uwezo mkubwa.
Tutakapoliteka Boma (Songea), tutakwenda kwenye vituo katika Nyasa pamoja, mimi na wewe.
Hivi sasa tusahau ugomvi wetu wa zamani.
Chupa hii, na dawa, imeletwa na Chinyalanyala mwenyewe, kiongozi wa vita.
Ameleta vilevile kombe, na anakupa salamu nyingi.
Endapo watu wako watakuja, Chinyalanyala mwenyewe atafika na atakupa vitu vingi vilivyo vitukufu.
Hassan bin Ismail anakusalimu.
Salam nyingi,
Sultan Songea bin Ruuf.''
Msikilize Mwalimu Hussein Bashir mwandishi wa vitabu kadhaa vya historia akizungumza:
Ukisoma historia ya Vita Vya Maji Maji utakutana na jina Mkomanile.
Linaandikwa jina moja tu, ''Mkomanile.''
Kwa nini liandikwe jina moja tu?
Huyu ndiye mwanamke pekee katika majina karibu 67 ya mashujaa wa Vita Vya Maji Maji aliyenyongwa na kuzikwa katika kaburi la halaiki Mahenge Songea.
Huyu mwanamke jina lake ni Khadija Mkomanile.
Kwa nini jina la Khadija halikuandikwa?
Tuseme hawakulijua?
Ukisoma historia ya Maji Maji utasoma jina Chinyalanyala jina moja tu.
Kwa nini liandikwe jina moja tu?
Jina lake ni Omar Chinyalanyala.
Inawezekana kuwa jina la Omar hawakuifahamu?
Ukisoma historia ya Vita Vya Maji maji utasoma jina la Songea Mbano.
Hapa unasoma majina mawili jina moja halikutajwa.
Kwa nini jina lake la kwanza halikuandikwa lifahamike?
Huyu jina lake lake la kwanza ni Abdulraufu.
Hili jina Abdulraufu hawakulijua?
Kuna ''Kazembe'' lakini jina lakini la kwanza halipo.
Haya yanashangaza sana.
Kipande hicho hapo chini kinatoka katika kitabu cha Abdul Sykes:
''Kuelewa hali ya Uislam wakati ule, unahitaji kusoma barua iliyoandikwa na Chifu Songea bin Ruuf wakati alipokuwa akikusanya nguvu za raia wake dhidi ya majeshi ya Wajerumani na huku akijaribu kupata ushirika wa machifu wengine katika sehemu za kusini ya Tanganyika na ng'ambo ya Mto Ruvuma katika Msumbiji.
Barua hii aliyoandikiwa Sheikh, Sultan Mataka bin Hamin Massaninga anaandika (barua hii ipo katika herufi za Kiarabu):
Sultan Songea bin Ruuf anasema:
''Kwa Sheikh Sultan Mataka bin Hamin Massaninga.
Asalaam Aleikum,
Ninakuletea barua kupitia Kazembe.
Tumepata amri kutoka kwa Mwenyezi Mungu kuwa Wazungu lazima waondoke nchini.
Tupo katika kupigananao hapa.
Naamini tumeshapatana muda mrefu, (kwa hiyo) niletee wanao, ili tufanye ushirikiano.
Nilitaka kukuletea mifugo kama zawadi, lakini sipo katika hali ya kuweza kufanya hivyo, kwa kuwa vita ambavyo Mwenyezi Mungu amevitaka vinaendelea.
Niletee watumiaji bunduki mia moja, na niunge mkono katika kulivamia Boma (Songea).
Ninakuletea chupa ya Mtume Muhammad, ambayo ndani yake ipo nguvu ya kuwashinda Wazungu.
Usiwe na shaka nayo, ina uwezo mkubwa.
Tutakapoliteka Boma (Songea), tutakwenda kwenye vituo katika Nyasa pamoja, mimi na wewe.
Hivi sasa tusahau ugomvi wetu wa zamani.
Chupa hii, na dawa, imeletwa na Chinyalanyala mwenyewe, kiongozi wa vita.
Ameleta vilevile kombe, na anakupa salamu nyingi.
Endapo watu wako watakuja, Chinyalanyala mwenyewe atafika na atakupa vitu vingi vilivyo vitukufu.
Hassan bin Ismail anakusalimu.
Salam nyingi,
Sultan Songea bin Ruuf.''
Msikilize Mwalimu Hussein Bashir mwandishi wa vitabu kadhaa vya historia akizungumza:
Google Photos
photos.google.com