Tatizo la maji Tanga mjini

Tatizo la maji Tanga mjini

Namche Bazar

Senior Member
Joined
Apr 8, 2019
Posts
122
Reaction score
179
Heshima kwenu wote.

Sisi wakazi wa kata ya Pongwe jijini Tanga yapata siku 10 sasa hatupati maji kabisa hasa katika maeneo ya Pongwe kusini (Sanawari) maji hayatoki hata tone moja.Hatujapata taarifa yeyote kuhusu tatizo la maji kama hapo nyuma ilivyokuwa na matengenezo nk

Tumeenda kwenye ofisi za mamlaka ya maji (Tanga uwasa) lakini majibu yao hayaridhishi.

Tumepata habari za kuaminika kuwa maji yote yamepelekwa vijiji vya wilaya ya Muheza ili kumtengenezea njia mbunge wa wilaya hiyo Adadi Rajabu aliyewaahidi wapiga kura wake watapata maji kabla ya 2020.

Tuonanyo sisi wananchi wa kata ya Pongwe huu ni ukatili mkubwa kwetu sisi ikiwa sisi ni wateja wa miaka mingi wa mamlaka ya maji ya Tanga,iweje leo sisi tunyimwe maji na kupelekea wateja wapya? Basi kama ni kutanua huduma za utoaji huduma ya maji kwanini kusiwepo na taarifa rasmi inayohusu mgao?

Tunamuamba waziri wa maji na naibu wake watufikirie na sisi katika kupata huduma hii muhimu ya maji hasa katika kipindi hiki cha Korona ambacho tunatakiwa kunawa maji tiririka kila wakati.

Tunaiomba ofisi ya TAKUKURU mkoa/taifa ije ichunguze huu mradi wa maji kwenda Muheza katika kipindi hiki cha uchaguzi mkuu,huenda meneja wa mamlaka ya maji Tanga mjini amepewa kitita cha fedha na kuruhusu maji yote yaende Muheza ili mbunge wa jimbo hilo apate kura?

Tunaomba tusaidiwe hivi sasa tunakunywa maji ya kwenye visima vifupi ambavyo vipo wazi na hatari kwa maisha yetu kwa ujumla wake.

Asanteni.

CC Prof Makame Mbarawa (waziri wa maji)
Juma Aweso (Naibu waziri wa maji)

Ummy Mwalimu (mtia nia ubunge Tanga mjini kupitia CCM.)
 
huenda meneja wa mamlaka ya maji Tanga mjini amepewa kitita cha fedha na kuruhusu maji yote yaende Muheza ili mbunge wa jimbo hilo apate kura?
Hapo hujatenda haki.. huenda amepata kitita??????
 
Hapo hujatenda haki.. huenda amepata kitita?
Sasa unataka tuseme nini, maana sio kawaida kuwanyima maji wateja waliopo na kuwapelekea maji wateja wapya.

Haiwezekani kwa hali ya kawaida bila kuwa na kiwezeshi, ndio maana tunaiomba taasisi ya kichunguzi TAKUKURU ifanye kazi hiyo ili ithibitike ni kweli au si kweli.
 
Sasa unataka tuseme nini,maana sio kawaida kuwanyima maji wateja waliopo na kuwapelekea maji wateja wapya.
Haiwezekani kwa hali ya kawaida bila kuwa na kiwezeshi,ndio maana tunaiomba taasisi ya kichunguzi TAKUKURU ifanye kazi hiyo ili ithibitike ni kweli au si kweli.
Nenda kwenye gruop la mlingano uwaulize viongozi wa wilaya ya Muheza, hasa diwani. Wana group lao la whatsapp , utapata jibu, then from there unaweza kwenda mbele. Uko wapi kwani? Pongwe au?
 
Hio itakuwa sio kawaida TANGA hakunaga shida za maji na moja Kati miji yenye maji na salama

Bila Shaka kutakuwa na uzembe au hujma
 
Naam mimi pia ni mkaazi wa Pongwe kusini, shida ni kubwa sana na hakuna taarifa yoyote rasmi kuhusu katizo hili. Ila kama alivyosema mtoa mada kuna tetesi kuwa maji yanapelekwa Muheza, si jambo baya, basi angalau wangeweka mgao tugawane baadhi ya siku.
 
Hio itakuwa sio kawaida TANGA hakunaga shida za maji na moja Kati miji yenye maji na salama

Bila Shaka kutakuwa na uzembe au hujma



Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa Tanzania hujuma Kama hii inawezekana, kumbuka wale watumishi wa tanesco walikuwa wanafungulia maji ya bwawa la mtera baada ya kupewa rushwa na wauza majenereta . Ningekuwa Nina madaraka ningenyonga wale watumishi walitutesa Sana na mgao wa umeme.
 
Huyo naibu waziri unayeshitaki kwake, kwenye jimbo lake maji yanatoka asubuhi na jioni kama dozi.
 
Tatizo ni sera mbovu za ccm kwa miaka 60 sasa. Tunahitaji kubadilisha watawala wa nchi hii.
 
Back
Top Bottom