Tatizo la kutokwa na damu kwenye fizi: Fahamu chanzo na namna ya kutatua tatizo hili

Naombeni msaada wenu katika hili. Nina miaka sasa natokwa damu kwenye fizi. Sijui tatizo ni nini. Ninapokuwa napiga mswaki tatizo huwa kubwa zaidi, lakini nimegundua hata niamkapo asubuhi hujikuta kinywa kina damu. Nimezunguka haspitali mbalimbali na kwanza nilipewa vidonge vya vitamini C, haikusaidia, Muhimbili wakanisafisha (kwangua) meno, bado haikusaidia. Nikaambiwa nipige mswaki mara tatu au zaidi....kila baada ya mlo, nalitimiza kwa ukamilifu bila mafanikio. Aidha, nikaambiwa nihakikishe napiga mswaki kwa sio chini ya dakika mbili na ikiwezekana hata kuongeza dawa mara mbili...natimiza, na tatizo liko palepale. Wajuzi nisaidieni, what next should I do?
 
Kama kwenye kuta za meno ile hali ya weusi/njano imerudi basi ni vema ukarudi wasafishe tena pia inabidi unywe na antibiotic za kutibu anaerobics angalau kwa wiki mbili pia ni vizur wakajua hali ya kuganda damu yako
 
habari,naomba msaada wa kitaalamu niweze kutatua tatizo la kutoka damu wakati wa kupiga mswaki,pia ni aina gani ya toothpaste nitumie kuondoa tatizo au kama mtu anafahamu professional hospital that naweza kwenda wakanisaidia...tatizo limeanza ghafla tu,naomba msaada jmn,naboreka sana...Thanks.
 
Mkuu, inaoenekana una too much cavity ambayo imejichimbia katika ufidhi (ufizi). Kabla ya yote unatakiwa usafishe meno yako kwa dentish. Huko, utanyonywa hiyo cavity na kupewaushauri nasaha. Kusema kwamba upige mswaki sijuwi mara ngapi kwa siku au sijuwi utumie toothpaste gani ni upuuzi tu, kwani tatizo lako ni cavity. You have too much.
 
Mkuu, inaoenekana
una too much cavity ambayo imejichimbia katika ufidhi (ufizi). Kabla ya
yote unatakiwa usafishe meno yako kwa dentish. Huko, utanyonywa hiyo
cavity na kupewaushauri nasaha. Kusema kwamba upige mswaki sijuwi mara
ngapi kwa siku au sijuwi utumie toothpaste gani ni upuuzi tu, kwani
tatizo lako ni cavity. You have too much.

Thanks Mkereketwa..
 
Kaka. Pole daaa kwanza nimecheka MKEREKETWA kanichekesha!! Kwanza kabisa kutoa damu katika fizi kunaweza tokea kama ! Kuna upungufu wa vitamin c ambazo zitafanya fizi kutokuwa na afya tosherevu

2: inaweza kuwa kwenye meno yako kuna vitu vinavyoitwa calculus , huu ni uchavu ambao hugandamana hasa sehemu ya shingo ya jino , na kuweka vitu vigumu vigumu na hata ukipisha ulimi vitu hvy huleta mikwaruzo,

Uchafu huo unapokuwa sehemu ya jino husababisha ( inflamation ) kuvimba kwa fizi kwani eneo hili huwa na damu nyingi ili kuilinda fizi kutokana na huo uchafu,

Na mara nyingi kunapotokea hali hii, mara upigapo mswaki damu hutoka kwa kiasi fulani , na si mswaki tu hata unapotafuna aina fulani ya vyakula vigumu damu huweza kutoka pia.

TIBA
Kama ni upungufu wa vitamin , utashauliwa kutumia matunda hasa ya vitamin c
2. :Na mara nyingine utapewa vitamic c vidonge ( ASCOBIC ACID)
3:Usafishwe fizi kama unauchafu huo ( calculus ) ugaga , pamoja na kupewa antiseptic mouth wash , eg hydrogen peroxide , linsterin, au medi oral .
4: Mwisho oral hygine instructions namna ya kuswaki , aina ya mswaki !!!!
 
Sorry hydrogen peroxide ya kutumia inatakiwa iwe 3% maana kuna ya 6% pia ambayo inatumiwa kwa vidonda.
 
naomba msaada kwa anayejua tatizo la kutokwa na damu kwenye fizi hasa napopiga mswaki,,
 
Wakuu mimi nina tatizo limeanza juzi tu,fizi zimevimba na meno yanauma hata kutafuna chakula siwezi,nifanye nini?naomba ushauri
 
Habari wana JF. Ninatatizo la muda mrefu la kutokwa na damu kwenye fizi hasa wakati wa kupiga mswaki au hata kama sipigi mswaki. Wakati mwingine hata kama ninaongea na mtu ananiambia damu kwenye meno.
Tatizo hilo lipo toka nikiwa mdogo mpaka sasa nina zaidi ya miaka 30.
Kama ni mswaki napiga ×2 kwa siku.
Msaada tafadhali.
 
Back
Top Bottom