Msaada maumivu ya meno/fizi

Msaada maumivu ya meno/fizi

Ngurukia

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2023
Posts
6,044
Reaction score
22,610
Hali zenu waungwana,

Kwa atakaekuwa na ujuzi/msaada juu ya maumivu ya meno na fizi nitamshukuru mno.

Ninasumbuliwa na meno kuuma hasa ya upande mmoja wa kinywa (kulia), yanavuta mpaka kwenye fizi na midomo ya chini.

Hakuna jino lililoharibika ila maumivu yake yanakithiri hasa yakiguswa na ubaridi.

Nilienda hospitali ya meno jibu nilililopewa ni kuwa mafizi yangu yamelika kupelekea kuwa na meno sensitive.

Nimekuwa natumia sensodyne sensitive na sensodyne rapid relief lakini huwa napeta ahueni kwa siku chache tu kisha huanza tena.

Nimejaribu kufuatilia chakula ninachokula kuona kuwa kama kuna trigger lakini sijaona cha mno ninachokula kuweza kuleta athari/maumivu.

kwa yeyote mwenye tiba nitashukuru mno.

Natanguliza shukran zangu za dhati.
 
Hali zenu waungwana,

Kwa atakaekuwa na ujuzi/msaada juu ya maumivu ya meno na fizi nitamshukuru mno.

Ninasumbuliwa na meno kuuma hasa ya upande mmoja wa kinywa (kulia), yanavuta mpaka kwenye fizi na midomo ya chini.

Hakuna jino lililoharibika ila maumivu yake yanakithiri hasa yakiguswa na ubaridi.

Nilienda hospitali ya meno jibu nilililopewa ni kuwa mafizi yangu yamelika kupelekea kuwa na meno sensitive.

Nimekuwa natumia sensodyne sensitive na sensodyne rapid relief lakini huwa napeta ahueni kwa siku chache tu kisha huanza tena.

Nimejaribu kufuatilia chakula ninachokula kuona kuwa kama kuna trigger lakini sijaona cha mno ninachokula kuweza kuleta athari/maumivu.

kwa yeyote mwenye tiba nitashukuru mno.

Natanguliza shukran zangu za dhati.
Rudi tena hospitali. Mbali na kutumia hizo sensodyne, kuna matibabu ya kufanya coating ya hayo meno kwa dawa(material) inayoitwa composite utafanyiwa, ambayo ndio itakuwa mwarobaini ya hiyo sensitivity.
 
Kuna mti mmoja unaitwa "mkuyu"
fanya uutafute na
hakikisha unapakaa utomvu wake kwenye jino linalokuuma.
jino likiacha kuuma nitafute nikupe maelekezo mengine.
 
Ngurukia ulipata tiba ya hili tatizo maana mimi pia linanisumbua
Nilipona kwa dawa za kawaida kabisa.

Kuna daktari aliniandikia dose ya Metronidazole (Flagyl) na Amoxillin. Nilipomaliza dose na tatizo liliisha mpaka leo.
 
Nilipona kwa dawa za kawaida kabisa.

Kuna daktari aliniandikia dose ya Metronidazole (Flagyl) na Amoxillin. Nilipomaliza dose na tatizo liliisha mpaka leo.
Weeeh maana hali niliyonayo ni kama uliyonayo wewe kwa wakati huo kulingana na maelezo yako ni hiii amoxilin ya vidonda kama sikosei na hizo dawa ni vidonge au kimiminika
 
Weeeh maana hali niliyonayo ni kama uliyonayo wewe kwa wakati huo kulingana na maelezo yako ni hiii amoxilin ya vidonda kama sikosei na hizo dawa ni vidonge au kimiminika
zote vidonge. Ni antibiotics lakini nilipewa kutumia kama combo
 
Back
Top Bottom