Tatizo la kula/kutafuna kucha

hata mm nakula sana kucha!! mpk zile nyamanyama kwenye kidole around kucha huwa nazila hasaa!! ila inasemekana mm nlipokuwa mdgo nilinyonya maziwa ya mama kwa miezi miwili tu baada ya hapo mwendo wa maziwa ya kopo na hii yote Ni kwa sababu mama yangu alikuwa akisumbuliwa na matatizo maziwa
 
Kama kichwa kinavyojitaja,

Nina swali juu ya hili swala kwa sababu cjui sababu ya kupelekea mtu kutafuna kucha na pia ningependa kujua tiba yake kwe sababu ni jambo ambalo limenikumba na nahitaji kuacha.

Naomba msaada wenu!!
 
kutafuna kucha ni moja ya bangi/alosto
Mimi siku moja nilijiuliza hivi huu upuuzi hadi lini?
ntakuwa mke wa MTU siku moja. na watoto bado natafuna kucha watanielewaje..?
maana ukianza kutafuna unakua Kama zezeta husikilizi unachoambiwa hufanyi unachofanya mpaka umalize...
halafu hata kumpa MTU mkono unaona aibu umetafuna na ngozi vidole vibayaaa...
nikasema sasa nafuga mkono wa kushoto kulia natafuna..
nikakaza hadi leo.. mkono wa kushoto Una kucha nzuriii...
nikahamia kulia nikasema nakula vidole vwili tu... vitatu nikafuga ndo had I Leo

huwezi kuacha kabisa tena vidole vya kutafuna co vyote
 
kutafuna kucha ni moja ya bangi/alosto
Mimi siku moja nilijiuliza hivi huu upuuzi hadi lini?
ntakuwa mke wa MTU siku moja. na watoto bado natafuna kucha watanielewaje..?
maana ukianza kutafuna unakua Kama zezeta husikilizi unachoambiwa hufanyi unachofanya mpaka umalize...
halafu hata kumpa MTU mkono unaona aibu umetafuna na ngozi vidole vibayaaa...
nikasema sasa nafuga mkono wa kushoto kulia natafuna..
nikakaza hadi leo.. mkono wa kushoto Una kucha nzuriii...
nikahamia kulia nikasema nakula vidole vwili tu... vitatu nikafuga ndo had I Leo

huwezi kuacha kabisa tena vidole vya kutafuna co vyote
Mbinu nzur sana hii
 
Unaweza ukaacha kutafuna kucha "kama utataka". Hakuna aliezaliwa akitafuna kucha isipokuwa hayo ni matokeo ya kimazingira.

Tatizo la kutafuna kucha tena "mpaka kuitwa tatizo" si kidogo. Kwa wenzetu wanasaikolojia wanaliita "tatizo la kitabia" na kwa watafunaji wengi, huwa kuna mazingira linatokea; mfn. Unapokuwa na stress, huna kazi ya kufanya, una matatizo ya ulaji n.k.

Katika umri mkubwa hali hii huwa ni mbaya sana kwa muathirika kwani unakuta mtu hawezi kupitisha dk 5 bila kuweka kidole aama vidole mdomoni na kuanza kung'ata kucha hata kaama ni fupi mno.

Ni kweli hali hii huleta fedhesha kwa mtafunaji hasa pale anapokuwa mbele za watu wa kuheshimika ama anapofanya presentation ya kitu fulani.
UNAWEZAJE KUACHA.
Kuacha si rahisi kama "hutatia nia ya kufanya hivyo". Utafunaji wa kucha ni tabia na mtu hujifunza tabia fulani na huamua kuiacha pia (a behavior can be learnt or unlearnt).

Kama alivyosema msemaji mmoja hapo juu njia moja wapo ni KUPAKA VITU VICHUNGU KWENYE KUCHA ZAKO ambavyo vitakufanya ushinde kuzitafuna kucha zako

Pili, kuviwekea "nail clip" vidole vyako.

Kuweka kitu kwenye meno ya upande wa juu mbele ambavyo vitasaidia kuzuia ukataji wa kucha.

Tatu, kujitahidi kujiepusha na vitu vinavyoweza pelekea kutafuna kucha (najua utakuwa unajua ni mazingira gani huwa unatafuna kucha zako)

Kutafuta kitu mbadala ambacho kitakufanya uwe bize nacho (kama gums) hivyo kutojishughulisha na kucha zako, ingawa nazo si nzuri.

Jitahidi kujizuia hata kwa kuvifunika vidole vyako kwa vitambaa ama gause kwani ukiweze kufanya moja ya mambo hayo kwa muda wa miezi miwili ama zaidi, hakika utaondokana na tatizo la kutaka kutafuna kucha'zo.

Dawa ya kuondoa tatizo linalokusumbua kwanza ni kama ulivyofanya "kuliona tatizo na kulikubali" na pili "kuchukua hatua" kwa kudhamiria kufaaanya hivyo.

All the best dear!
 
Mnao tafuna kucha mnaupungufu wa madini ya chuma mwilini...ivo basi jitahdini kula vyakula vyenye madini ya chuma mtaacha kula kucha......
 
Anayetafuna kucha ana tabia ya aibu, ana mawazo/stress ama ni mwoga.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom