Taswira ya Mbagala

Taswira ya Mbagala

.......kati ya maeneo ya dar yalionikalia kushoto kujenga au hata kuishi ni mbagala, sijui kwa nini? Sinaga mzuka hata wa kununua kiwanja hata kama ni bei rahisi. Wilaya ya temeke yote huwa siipendi.

Mkuu kwa ile kazi yako itakuruhusu kwel kupata hela ya kununua kiwanja Mbagala? vip mkuu bado upo kwa sista au ulishapata chumba chako mwenyewe? teh wabongo bhana
 
Mimi nisipokuta ile foleni ya pale bandari nafika mjini kwa dk 20, ikiwepo dk 30-45 honestly nafaidi usingizi maana sina haja ya kuamka sa11 kwenda kazini. Sasa wewe toka huko unakoish njoo tukutane posta tuone kama tutafika sawa? Huyu vp? We huijui mbagala kaa kimya.

Nakaa huko watu hawaijui Mbagala. Ni raha sana kwa usafiri. tena asubuhi kama unatoka mbagala gari za toka mjini huwa wanazizuia watu waweze kuwahi kazini kuanzia darajani
 
Mbagala nayoishi mimi hatujui shida ya maji, chumba bei rahisi, vigodoro ni shughuli za kawaida tushazoea, chakula ni bei rahisi naipenda mbagala

Na wao vigodoro vyao ni akina FM academia twanga.....etc ... Kuanzia Jumatano usiku kuchwa Ndombolooooo
 
Mbagala hawachangii nyembe tu hata kondomu hufuliwa na kuazimwa kwa mtu mwingine.

Inaweza ikawa afadhari ya hiyoo... Huko kwenu mnachangia mademu bila kondomu... Na mademu wenyewe hao wanalia kwa script ... oooshhh bebii... ooosh shiiiit..... mwanzo mwisho .......kila mmoja anaona yupo peke yake na anapendwa sana
 
Mbagala hakuna taby ya maji kama ubungo kwa mnyika.

Mbagala na temeke kwa ujumla ni eneo ambalo kuna viwanja vingi vya wazi na michezo ambavyo havijauzwa kama kinondoni.

Mbagala watu wanaishi kwa umoja ustaarabu na kusaidiana wakati wanatatizo kuliko ubungo kwa mnyika ambao ni wabinafsi na wachoyo ambao wako ladhi. Kukata mabomba ili wauze maji.
 
wanajeshi wengi waliostaafu na police wameenda kujenga mbagala, usafiri sio shida kama mbezi, kimara, bidhaa bei rahisi.
 
Wiki hii nilipata fursa ya kupita mbagala na kuzungukia mitaa michache na hiki ndio nilichokiona;

1.Kwa wenyeji Mbagala hujulikana zaid kama "Mbajala"
2.Mbagala ina watu wengi sana na pilikapilika ni nyingi sana.
3.Nyumba nyingi zimetenganishwa na njia na vipenyo finyu sana lakini ndani kuna sofa! sijui hata hizo sofa zinapitaje
4.Kuna ujamaa sana watu bado wanachangia matumiz ya vitu mbalimbali nimekuta jamaa watano wamejipanga kwa kinyozi wanahudumiwa kwa wembe mmoja!
5.Kuna ukaribu baina ya watu kiasi kwamba watu wanafahamiana, kama ni mgeni utajulikana tu.
6.Kuna biashara kubwa ya vitu feki / pirated hasa cd, tv n.k
7.Ofisi ya imamu ni moja ya ofisi muhimu sana pengine kuliko hata ya mjumbe wa mtaa
8.Kuna uwingi wa ofisi za wataalam wa tiba asili pengine kuliko hata maduka ya madawa.
9.Wakazi wa huko hupendelea sana sherehe zinazokwenda kwa majina mbalimbali kama kumtoa mwali, maulidi n.k, sherehe husherekewa kwa shangwe na vigelegele na akina dada na akina mama ambao wengi wao huvalia nguo nyepesi za kuangaza almuradi kila kitu burudani!

Jaman hii ndio Mbagala niliyoiona mimi, Je Mbagala yako ikoje?

noma sna
 
Back
Top Bottom