Taratibu za kufuata ili kupata TIN Number

Chuck j

JF-Expert Member
Jun 17, 2011
2,358
815
Naombeni kwa mwenye kujua jinsi ya kupata TIN Number.
Asanteni

HABAR WAKUUU,

Nnaomba msaada kwa anaejua ni njia zipi nizitumie kupata Tin number ya TRA kwa ajili ya kampuni, nmesajili kampuni brela la usambazaji wa vifaaa, nnahitaj nipate TIN ya mlipa kodi ndo nianze operation,,, msaada kwa mwenye ujuza tafadhar

====================================
Nenda kasajili jina la biashara Brela kwanza wakishakupa Cheti, unakipeleka TRA ukiwa na nakala ya mkataba wa ulipopanga ofisi ya biashara yako na vitu vingine kadhaa wanavyovihitaji. Watakupatia TIN

Kisha unaambatanisha Copy ya TIN, Cheti Cha Usajili ( Brela ), Mkataba wa eneo la ofisi, Copy ya kitambulisho Nk. vyote hivi unaenda navyo kwa afisa biasha katika wilaya husika huyu ndiye atakayekupatia Leseni ya Biashara.

Nimejaribu kukumbuka kumbuka, ila uwe tayari na usumbufu wa kipuuzi kutoka kwa watumishi wa umma.

USITOE WALA KUPOKEA RUSHWA TAFADHARI.

Kama ni kampuni ni hivi,
1. MOA
2. Registration
3. Extract
4. Mkataba wa mahala pa biashara ulioshuhudiwa na wakili
5. Utambulisho wa shareholders
6. Barua ya utambulisho wa serikali za mitaa pale unapofungua biashara, yaani ulipopanga
7. Kama ni pako uwe na uthibitisho
8 Picha mbili zilizogongwa mhuri wa mwenyekiti wa serikali za mitaa
9. Jiandae kulipa kodi ya mwaka huu yaani unaweza kukadiriwa 150K na kutakiwa kulipa nusu.
10. Usumbufu wa hapa na pale


ACHENI KUDANGANYA WATU!!!!!
Si dhani kama ni lugha sahihi kutumia na hasa hasa tunapojiita GTs. Lkn naamini ungeji-homework-isha kidogo tu ungegundua TIN ni BURE. Tunalipa withoholding tax(10%) on rent sbb tumelipa kodi, vp kama ofisi/fremu ni yako mwenyewe, utalipa w/tax 10% based on what amount?

Gharama uliyojengea ofisi? Mimi nilitakiwa kulipa hiyo w/tax nikawaambia silipi kodi ya pango sbb ni family premise na nilitakiwa kuthibitisha kwa kupeleka docs. Ishu ni kwamba huwez kupewa TIN wkt umekwepesha kodi yetu, w/tax lazima ilipwe kwa kila kodi ya pango utakayolipa.

Ila unaweza kutumia ujanja wa kuipunguza kwa muda lkn end of the day utatakiwa kuilipa tu. Kama pango ni 200,000/= kwa mwez so it is 2,400,000/=kwa mwaka. therefore w/tax(10%) utakayolipa ni 240,000/=

Tafuta mkataba mwengine(utajua mwenyewe utakapo upata) utakao onyesha kodi ya pango ni 200,000/= lkn umelipa miezi miwili au mitatu yaani 600,000/= kwahiyo w/tax(10% ya 600,000) ni 60,000/=kwahiyo utakua umeipunguza kwa muda kutoka 240,000/= mpaka 60,000/= kwakweli inakera kulipa kodi kabla ujaanza biashara na kidogo ina leta saikolojiko satisfaksheni kuona badala ya kulipa 240,000 umelipa 60,000 na kuokoa 180,000/=ni nyingi sana kibiashara.

Kimsingi w/tax inabidi ilipwe na mwenye nyumba sbb yeye ndio mnufaikaji wa kodi ya nyumba lkn fanya hivyo TZ uone kama utapata hiyo nyumba au fremu yenyewe. Mpangaji ndio mwenye wajibu wa kuikata na kuiwakilisha TRA kisha receipt lazima apelekewe mwenye nyumba kama proof of payment of w/tax.
 
Nenda TRA,TIN hutolewa bure,ingawaje watakusumbua ili wapate kitu kidogo lakin komaa,usikubali kutoa rushwa,narudia tena usikubari kutoa rushwa,mtoa rushwa na mpokea rushwa wote ni watuhumiwa.TIN ni bure hata ukifika TRA utakuta matangazo ya kumwaga kukujulisha kuwa TIN hutolewa bure.Nakutakia mchakato mwema
 
TIN ni bure ila maagent wengi hukukamua hasa kama ukiwaachia wao wafanye. Kama unataka kutoa gari unaenda na kopi ya B/L pale TRA kodi za ndani pale jirani na TTCL posta. Utajaza application form na kusajiliwa katika computer then utapigwa picha na itaingizwa katika computer pia. Baada ya dakika kadhaa utapewa TIN yako. Jaza kitabu na potea hapo ni bure. Wakikuona kama haujui utaratibu watakuingiza katika mtego wa rushwa. Otherwise kama unataka TIN kwa ajili ya kubadili leseni then utaelekezwa uende TRA ya wilaya unayotoka ie Kino, Temeke au Ilala. Good luck
 
Duh ,,,,mi nataka kwa ajili ya kubadili renew lesen ya biashara ya mazao ya misitu,,umenisaidia sana,,Kama kuna kiachohitajika zaidi let me know pls,,Mungu akubarriki''
 
Kwa anayejua utaratibu anifahamishe na gharama zake pia...

Natanguliza shukrani

TIN number hutolewa bure lakini hupewi mpaka wakukadirie kodi kulingana na biashara yako ilivyo then baada ya kulipa kodi ya awamu ya kwanza ndio wanakupa TIN number kuhusu leseni nenda manispaa ya kinondoni for more details au wadau watajazia.
 
TIN number hutolewa bure lakini hupewi mpaka wakukadirie kodi kulingana na biashara yako ilivyo then baada ya kulipa kodi ya awamu ya kwanza ndio wanakupa TIN number kuhusu leseni nenda manispaa ya kinondoni for more details au wadau watajazia.

nashukuru mkuu...
 
umeshajisajiri jina la biashara yako,? kama bado nenda brela kajisajiri na TIN no wanatoa bure ila mpaka wafanye installment ya biashara yako ndiopo wakupe, hiyo na kuhusu leseni ya biashara mpaka uwe na TIN no ndipo waweza jaza fomu za leseni ndipo waje kukagua eneo au biashara yako iilipo wakupe leseni? una jingine la kusema?
 
umeshajisajiri jina la biashara yako,? kama bado nenda brela kajisajiri na TIN no wanatoa bure ila mpaka wafanye installment ya biashara yako ndiopo wakupe, hiyo na kuhusu leseni ya biashara mpaka uwe na TIN no ndipo waweza jaza fomu za leseni ndipo waje kukagua eneo au biashara yako iilipo wakupe leseni? una jingine la kusema?

Hapo kwenye blue sijaelewa vizuri.
TRA mpaka wafanye nini ndio wakupe TIN ?
Ina maana TIN inatolewa kwa masharti fulani ?

Naomba msaada wa kueleweshwa.
 
kwani aliyeuliza ni tindikalikali au ni mu-israel mtoa roho za watu?
Hapo kwenye blue sijaelewa vizuri.
TRA mpaka wafanye nini ndio wakupe TIN ?
Ina maana TIN inatolewa kwa masharti fulani ?

Naomba msaada wa kueleweshwa.
 
kwani aliyeuliza ni tindikalikali au ni mu-israel mtoa roho za watu?

Nimeona mada nikaona kuna jambo sijaelewa vizuri nami labda naweza kuelimishwa.
Ndio maana nikauliza tu hapo.
Nitafurahi kama nitaelimishwa zaidi kwenye mada hii ingawa sio mimi nilioanzisha mada hii.
 
oky kama umejisajiri jina la kampuni/biashara yako unayotaka kufanya, nenda TRA watakupa fomu za TIN utajaza na watakupa maelekezo yote waoo namna ya kufanya utapataa maelekezo na mambo mengine palepale ni hayo mkuu
Nimeona mada nikaona kuna jambo sijaelewa vizuri nami labda naweza kuelimishwa.
Ndio maana nikauliza tu hapo.
Nitafurahi kama nitaelimishwa zaidi kwenye mada hii ingawa sio mimi nilioanzisha mada hii.
 
Ingia tovuti ya tra, nenda ujazaji online wa tin, fuata maelekezo, ukimaliza nenda tra kuweka dole gumba. Maelezo mengine ya upatikanaji wa tin utapata tra bila wasiwasi kabisa. Ukipata tin nenda halmashauri yako kitengo cha biashara watakuelekeza ujazaji wa fomu na mengineyo, ila si bure tena ni fedha, gharama yake itategemea kule tra walikufanyia makadirio kiasi gani ya biashara yako kwa mwaka. ( wakati mwingine tra wanakwambia uende kwa tax consultant akufanyie makadirio ya mapato yako kwa mwaka, then consultant ataandika report utakayopeleka tra ili ufungue file na ulipie tax in advance).
 
Nawashukuru sana wachangiaji wote katika mada hii...hakika itanisaidia sana.
 
Tafadhali check me asap kama unaweza kunitolea TIN number maana kwa sasa sipo karibu na mji na inahitajika sana a muhimu...
 
Back
Top Bottom