The Invincible
JF-Expert Member
- May 6, 2006
- 6,003
- 3,269
Haya baba nimekusikia.Ndugu yangu Mkuu The Invincible, hakuna haja ya kutukanana "kenge wewe" na kuwahukumu marehemu wa watu, waachwe wapumzike, anayetoa huku ni Mungu mwenyewe, na hivi vitu ninavyowaambia hapa nyinyi wafia dini, usiviite vya kijinga, kwa sababu haya ninayoyazungumza humu ni mafundisho yake YEYE mwenyewe, ametufunza, "Tutaokolewa kwa neema na sio kwa matendo", hivyo hata mtu awe aliishi kihuni vipi na kanisa kugoma kumzika kwa heshima zote, wakovu haitokani na matendo yake bali ni neema tuu. Na wote wanaozikwa kwa sala na misa Takatifu, sio kigezo kuwa wao ndio wataenda mbinguni.
Mwacheni Ruge apumzike, tusinyooshe vidole na kumhukumu kwa maisha yake, yale ni maisha yake, ajuaye ya mbele ni Mungu pekee.
P