TUJITEGEMEE
Platinum Member
- Nov 6, 2010
- 27,504
- 28,436
Msanii huyu amefariki leo asubuhi baada ya kujifungua. Mungu alilaze mahali pema peponi.
Source: M/kiti wa CCM taifa kupitia TBC/ITV
Source: M/kiti wa CCM taifa kupitia TBC/ITV
Pole nyingi kwa Baba wa mtoto aliyeachwa, kwa mtoto mwenyewe, wazazi, ndugu na marafiki wa "Paka Mapepe". Hakika inauma sana. Kweli hakuna kifo kizuri hata kimoja. Lakini kuna uchungu mwingine huzidiiiii! Hembu fikiria, mtoto hajanyonya, hatamjua mama yake maisha!!! Malengo ya dada huyu katika maisha yamesimama ghafla!!! Lakini sasa utashangaa kusikia "Kazi ya Mungu haina makosa", "Mungu amechukua kiumbe chake" ; "Mungu kachuma ua lake" ; "Kama uliandikiwa...." n.k. n.k. Jamani, hembu wana JF tutafakari kidogo. Huyu Mungu, ambaye tunajua ni Mungu wa Upendo na Rehema na Fadhili, amemchukua mama mara baada ya kujifungua!!!! Kichanga kiteseke? HAKIKA, SI MUNGU KACHUKUA KIUMBE CHAKE. Hii ni kazi ya IBILISI. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo wa wanadamu, na ameendelea kuua, halafu ni mwongo, na anaendeleza uongo wake.Yohana 8:44. Tumlaani Ibilisi na malaika zake. Mungu atakikomesha kabisa kifo kisiwepo milele. Ufunuo 21:3,4. Nawatakia siku njema.
Msanii huyu amefariki leo asubuhi baada ya kujifungua. Mungu alilaze mahali pema peponi.
Source: M/kiti wa CCM taifa kupitia TBC/ITV