Tanzia: Msanii Jebby afariki dunia kwao Dodoma

Papaa Mobimba

JF-Expert Member
Jan 27, 2018
754
3,097
Msanii-Jebby.jpg

Msanii Jebby amefariki dunia leo akiwa nyumbani kwao Dodoma. Imeelezwa kwamba siku kadhaa zilizopita Jebby aliomba kurudi kwa Dodoma baada ya hali yake kuwa mbaya. Taarifa za awali zinasema alikuwa anasumbuliwa na uvimbe kwenye bandama.

Msanii Jebby atakumbukwa kwa wimbo wake wa 'Swahiba' aliomshirikisha Afande Sele. Wimbo huo umekuwa ukisikika kunapotokea msiba mkubwa na hata Masogange umauti ulipomkuta wimbo wa ''Swahiba'' umegongwa sana.

RIP Jebby.

Wimbo wa Swahiba
 
Back
Top Bottom