Tanzia
Aliekuwa Mtangazaji maarufu wa radio Tanzania (TBC) mzee BEN KIKO amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo 31/10/2014 kwenye hospital ya jeshi mirambo Tabora.
R.I.P BEN
CHANZO: TBC
Aliekuwa Mtangazaji maarufu wa radio Tanzania (TBC) mzee BEN KIKO amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo 31/10/2014 kwenye hospital ya jeshi mirambo Tabora.
R.I.P BEN
Rais JAKAYA KIKWETE amemtumia Salamu za Rambirambi Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Dokta FENELA MUKANGARA kuomboleza kifo cha aliyekuwa Mtangazaji na Mwandishi Mkongwe na Mahiri hapa nchini wa iliyokuwa Radio Tanzania - RTD ambayo kwa sasa ni TBC Taifa, BEN HAMIS KIKOROMO maarufu kama BEN KIKO.
Katika salamu zake Rais KIKWETE amesema amehuzunishwa na kusikitishwa na taarifa za kifo cha BEN KIKO ambaye ametoa mchango mkubwa wa kihabari kwa Taifa.
Wakati wa vita dhidi ya Nduli IDI AMIN wa UGANDA mwaka 1978, BEN KIKO alifanya kazi kubwa kwa Taifa kwani aliweza kuripoti matukio mbalimbali kutoka katika uwanja wenyewe wa vita, na hivyo kuliwezesha Taifa na wananchi kwa ujumla kuhabarika vilivyo na matukio yaliyokuwa yakiendelea.
BEN KIKO amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Taifa ya MUHIMBILI ambako alikuwa amelazwa akipatiwa matibabu ya figo baada ya kuhamishiwa hapo akitokea Hospitali ya Jeshi ya MILAMBO Mkoani TABORA.
Katika hatua nyingine Rais JAKAYA KIKWETE amesaini kitabu cha Maombolezo kufuatia Kifo cha aliyekuwa Rais wa ZAMBIA, MICHAEL SATA.
CHANZO: TBC