Wadau, tumshukuru Mungu uchaguzi umeisha kwa 'amani' ingawa hatua ya NEC kushindwa kutoa matokeo kwa muda unaotakiwa ni aibu na dosari kubwa. Wananchi sasa wamefikia hatua ya kuona kuwa chaguo lao haliwezi kuthibitishwa na Tume hadi walazimishe. Sote tu mashahidi kuwa pale ambapo CCM inapokuwa imeshinda Ubunge, Msimamizi wa Uchaguzi (kw aniaba ya NEC) anatangaza matokeo haraka, lakini pale ambapo wapinzani wa CCM wameshinda inachukua muda sana kuthibitisha matokeo hadi amani inakuwa inatishiwa.
Arusha, maduka yote yalifungwa mjini kwa sababu Msimamizi wa Uchaguzi alichelewa kutangaza matokeo hali iliyofanya mji uwe tete na maduka yote mjini kufungwa kwa ajili ya umma uliokusanyika Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi tangu aalfajiri! Umma unajua mshindi mapema maana matokeo yote ya Uunge na Udiwani hubandikwa kwenye kuta za vituo vya kupigia kura. Sehemu zote ambazo Wapinzani wameshinda, matokeo yameshinikizwa na Umma na kushuhudia uvunjifu wa amani (kama ilivyodaiwa na CCM wakati wa Kampeni, je, kuna kitu gani nyuma yake kama sio NEC na CCM/ Serikali kuwa kinyume na maamuzi ya umma? Uliona wapi na lini pale ambapo wananchi waliridhika na matokeo kukawa na vurugu? Zanzibar mwaka huu kulikuwa na fujo gani? Kwa nini hali ya fujo itokee Bara ambapo kuna vyama vikuu zaidi ya viwili vinanvyopingana? NEC, CCM na Dola wanasababisha hali hii, NDIYO!
Idadi ya Wapiga kura waliosajiliwa kwenye daftari ni tata na kuna uwezekano mkubwa kuwa na mahoka wengi sana na watu waliojiandikisha zaidi ya mara moja. Tuchunguze trend ya Wapiga kura tangu kuanzishwa kwa daftri, kwa nini idadi ya wanaojitokeza inakuwa ndogo? Hivi ni kweli wananchi hawajahamasika kupiga kura?
Mwaka 2005 (wakati daftari lilipotumika kwa mara ya kwanza) idadi ya waliojitokeza ilikuwa kubwa kulinganisha na chaguzi zilizofuatia, hii inawezekana kabisa kuwa idadai iliandaliwa maalumu kwa ajili ya matokea ya kishindo kwa CCM!
Tujiulize, kwa nini wakati idadi ya wanaojiandikisha inaongezeka kila daftri linapofunguliwa inaongezeka sana lakini ukifika uchaguzi idadi ya wapiga kura inapungua kuliko ya awamu ya uchaguzi ulopita? Hapo kuna jambo!
SHUKRANI KWA POLISI
Kama mwaka huu Polisi wetu wangekuwa wanongozwa na IGP Mstaafu Mahita, naamini kabisa Bara ingekumbwa na umwagaji mkubwa wa damu. Shukrani za pekee kwa IGP mwema ambaye amejitahidi kuachana na fikra za ukandamizaji.
LAkini pia inawezekana hata jeshi letu la Polisi limechoshwa na uvurugaji wa matokeo ya uchaguzi na kutumiwa na Wanasiasa (hasa CCM) kwa gharama ya maisha ya umma na kwa kupakwa matope kwa kutumia maguvu bila sbabu za msingi huku wao wakishutumiwa kwa rushwa wakati Wanasiasa wakishiriki kwenye rushwa kubwa zaidi.