TANZIA Wakili mtetezi wa ICTR Prof. Jwani Mwaikusa auawa Tanzania

kmp

Member
Jun 18, 2009
39
0



Habari nilizozipata zinasema Prof. Mwaikusa Mwalimu wa Sheria na Mwanasheria aliyebobea wa Chuo Kikuu cha DSM amefariki dunia baada ya kuvamiwa na watu wanaosemekana kuwa ni majambazi alipokuwa akirejea nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo.

Prof. Mwaikusa pia alikuwa rafiki wa mahakama ambaye alitetea vizuri hoja alizowakilisha kuhusu mgombea binafsi. mwenye data zaidi atujuze. rip prof.mwaikusa.
---

1713088394724.png

Wakili mwandamizi wa utetezi nchini Tanzania wa mahakama inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa inayoshughulikia kesi za washukiwa wa mauaji ya kimbari ya Rwanda amepigwa risasi na kufa nje ya nyumba yake mjini Dar es Salaam.

Profesa Jwani Mwaikusa, ambaye pia alikuwa mkufunzi katika chuo kikuu cha Dar es Salaam, aliuawa wakati akitaka kuingia nyumbani kwake nje kidogo ya mji huo.

Polisi wanasema mpwa wake pamoja na jirani yake waliuawa pia.

Imearifiwa kuwa wahalifu hao walilipekua gari la marehemu na kuondoka na mkoba wake wa kazi pamoja na hati kadhaa.

Bw Mwaikusa alikuwa wakili mtetezi wa mfanyabiashara wa Rwanda Yussuf Munyakazi anayekabiliwa na tuhuma za kuhusika katika mauaji ya kimbari kwenye mahakama ya kimataifa mjini Arusha.

Wakati akimtetea, alifanikiwa kuzuia Munyakazi asirejeshwe nchini Rwanda, kwa hoja kuwa asingeweza kutendewa haki na mahakama za huko.

Gazeti la Citizen nchini Tanzania limesema kumekuwepo na ongezeko la matukio ya uhalifu mjini Dar es Salaam katika siku za hivi karibuni.

Watu watano wameuawa kwa risasi na wahalifu wenye silaha katika kipindi cha miezi mwili iliyopita.
---

Viongozi na Wanasiasa wengine waliowahi kupigwa riasasi
- Utata kifo cha hayati Abeid Karume

- DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

- Simulizi: Kisa na Mkasa wa Mauaji ya Jenerali Imran Kombe (Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa-TISS)

- TANZIA - John Mwankenja auawa kwa risasi

- Dr. Wilbert Kleruu - Utata wa kifo chake, historia na maisha yake

- TANZIA - Waziri Salome Mbatia afariki dunia, maswali yaibuka!

- Iringa: Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA

- Maandamano ya CHADEMA: Aqulina Akwilini Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza NIT apigwa risasi na kufariki; Polisi wakiri kuhusika

- Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka ashambuliwa kwa risasi na Watu wasiojulikana

- Askari polisi aliyepigwa risasi na majambazi Tanga afariki
 
Last edited by a moderator:
Mhhh, hii ni habari mbaya na ya kutisha. Poleni sana wafiwa.

Hii nchi sasa inatisha. Majambazi wanatamba utadhani wanaishi ikulu?

RIP Prof. Mwaikusa.
 
Poleni sana wanafamilia na wale wote wanaotetea demokrasia ya kweli katika nchi hii. Lakini moto wa mgombea binafsi hauta zimika labda watumalize watanzania wote wenye mitazamo kama ya prof. Mwaikusa

RIP Prof. Mwaikusa
 
Sad News...R.I.P prof.

Prof. Jwani T. Mwaikusa

mwaikusa.jpg



Career:
  • Professor of Law, Faculty of Law, University of Dar es Salaam 1999
  • Mkono & Co Advocates since 1998
  • Advocate, High Court of Tanzania since 1988
  • Managing Editor of the Tanzania Law Reports.
Qualifications:

  • Ph.D., School of Oriental & African Studies, University of London, UK, 1995
  • LL.M, University of Birmingham, UK, 1985
  • LL.B (Hons), University of Dar es Salaam, Tanzania, 1981.
 
Majambazi kazi zao kuharibu/kubomoa/kusambaratisha miundombinu/ hazina iliyokwisha tengemaa bila kujali gharama zilizotumika hapo na taifa waitegemea vipi. RIP Mwaikusa
 
mwaikusa.jpg
Habari ambazo zimeingia sasa hivi ni kuwa Prof. Jwani Mwaikusa ameuawa. Pamoja naye taarifa zinadokeza kuwa mwanae pia ameuawa. Tunaendelea kufuatilia taarifa hizo kwa karibu ili kuweza kupata taarifa za uhakika zaidi.

Wengi tunamfahamu hivi karibuni katika kesi ya wagombea binafsi akiwa mmoja wa walioitwa kuwa "marafiki wa mahakama" yeye akitetea haki ya wagombea binafsi na kusisitiza kuwa mahakama ina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo. Siku za karibuni amekuwa ni mwanasheria katika Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Rwanda na mmoja wa wanasheria waliobobea wa Katiba amefariki duniani.

Taarifa zinadokeza kuwa mauaji hayo yametokea nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo.

Taarifa bado zina kiza kuna uwezekano wa zaidi ya watu wawili kuwa wameuawa kwenye tukio hilo..



sina details zaidi.. vyanzo vyetu vinafuatilia..
 
Oh no!
How convenient? If it's true, one can't rule out a politically motivated assassination.
 
habari nilizozipata zinasema prof.mwaikusa mwalimu wa sheria na mwanasheria aliyebobea wa chuo kikuu cha dsm amefariki dunia baada ya kuvamiwa na watu wanaosemekana kuwa ni majambazi alipokuwa akirejea nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo. prof.mwaikusa pia alikuwa rafiki wa mahakama ambaye alitetea vizuri hoja alizowakilisha kuhusu mgombea binafsi. mwenye data zaidi atujuze. rip prof.mwaikusa.

..what a sad news! Mwe...MUNGU wape moyo wa matumaini familia na ndugu wa mpendwa wetu JWANI!

Usalama katika nchi hii ni ZERO, majambazi wanatamba na kupoteza roho za watu kadri wapendavyo. Hii si ajabu kwani baadhi ya Police yasemekana wamo kwenye payroll za majambazi:embarrassed1:

Ndugu yake kanielezea kwa simu mazingira ya kifo: Prof Jwani alikua anarudi nyumbani kwake alipoingia getini, majambazi wawili unknowingly waliingia naye. Wakamlazimisha kushuka kwenyee gari yake, hakushuka na ndipo walipoanza kummiminia risasi na kumuua. Mtoto wake akaja ili atoe msaada (bila shaka baada ya kusikia milio ya risasi) nae pia kamiminiwa risasi na kufa. Pia inasemekana jirani yake naye katika jitihada za kutaka kuja kutoa msaada naye kauwawa!!! :embarrassed1: UKAGONE MALAFYALE!

MUNGU MWENYE REHEMA NA NEEMA NYINGI, WASAMEHE WALIOFANYA KITENDO HIKI CHA KIKATILI NA KUTOA ROHO YA MPENDWA WETU!!!!
 
Inawezekana klakini acha imani hizo kwa sasa. Dhana hii ndio inayowapa nafuu Askari wlale na majambazi wazidi kuangamiza baba na mama za watu na kusabababisha mateso makubwa kwa wale waliokuwa wanaomtegemea.
Oh no!
How convenient? If it's true, one can't rule out a politically motivated assassination.
 
"Mungu aziweke Roho za Marehemu Mahala pema peponi"

----

Kuna kila dalili za kuonyesha Ujambazi umerudi tena kwa kasi na nguvu zaidi Tanzania. Tofauti ndogo ni kuwa ujambazi wa kwenye mabenki umepungua na sasa ni raia na mali zao ndio wanataabika.
 
Mmh! Hii inatisha jamani, sasa hao majambazi walifanikiwa kuchukua kitu? au ilikuwa ni chuki tu?
Nina wasiwasi kama kweli ni majambazi, sasa kwanini waue mtoto na jirani pia!!
Mungu tusaidie.
 
Back
Top Bottom