ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 79,084
- 84,978
My Take
Nafasi ya kwanza ni Uganda baada ya Kuipita Ethiopia.
Bajeti ya Kilimo iliyoongezwa na Serikali ya Samia kutoka Bilioni 250 Hadi Trilioni 1.2 imeanza kuzaa matunda Kwa Tanzania kuzipiku Kenya na Ivory Coast kuwa namba 3 wa Kuzalisha Kawaha Afrika nzima.
Hongera sana SSH Kwa utashi wa Kisiasa, hongera Waziri Bashe na hongera wakulima hata kama Chadomo Watachukia 😂
Tuna kazi ya kufanya kuwapita Uganda & Ethiopia
View: https://www.threads.com/@statsfrica/post/DL43rrOtze2?xmt=AQF0ylHZJJdF7ncGFuEAgqtm5KtFVUNDuW3_rbJkheL4Tg
==============
Tanzania inashika nafasi ya tatu barani Afrika kwa uzalishaji wa zao la Kahawa hapa nchini, ikizipiku nchi za Kenya na Ivory Coast zilizokuwa nafasi za juu kwa uzalishaji wa zao hilo Afrika.
Hayo yalibainishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Ushirika na Umwagiliaji, Dkt. Stephen Nindi wakati akifunga Mkutano Mkuu wa 15 wa Bodi ya Kahawa nchini kwa niaba ya waziri wa kilimo, uliofanyika jana jijini Dodoma.
Dkt. Nindi amesema serikali itaendelea kutafuta masoko ya zao la Kahawa katika nchi mbalimbali barani Afrika na nje ya bara la Afrika, ili kuhakikisha inawainua kiuchumi wakulima mbalimbali hapa nchini lakini pia kuongeza mapato.
Aidha amesema lengo la serikali ni kuona kahawa ya hapa nchini inazidi kupata soko katika nchi tofauti ili wazidi kupanua wigo wa soko la zao la Kahawa duniani kote na kuongeza kuwa lengo ni kuona Kahawa ya Tanzania inatumika sehemu mbalimbali.
Kutokana na hilo, ameviagiza vyama vya Ushirika hapa nchini kuhakikisha vinashirikiana na Bodi ya Kahawa kuhakikisha wanasonga mbele ikiwemo kutatua changamoto ndogo ambazo wanakutana nazo wakulima ili kuendeleza tasnia ya kahawa.
Amesema pia serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa kahawa ili kuhakikisha zao hilo linakuwa na mchango mkubwa katika uchumi wa nchi hii ikiwemo kuongeza kuchangia pato la taifa kupitia mauzo ya ndani na nje ya nchi.
Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Kahawa nchini Primus Kimaryo amesema Bodi hiyo inaendelea kuweka mikakati ya kuimarisha kilimo cha zao hilo ili kufikia malengo ya kuongeza uzalishaji katika maeneo mbalimbali.
Kimaryo amesema Bodi hiyo ilijiwekea kufikia tani 300,000 ndani ya miaka mitano lakini hazijafika na kuongeza wanarudi kujipanga upya ili waweze kufikia mkakati wa kuzalisha tani hizo.
Nafasi ya kwanza ni Uganda baada ya Kuipita Ethiopia.
Bajeti ya Kilimo iliyoongezwa na Serikali ya Samia kutoka Bilioni 250 Hadi Trilioni 1.2 imeanza kuzaa matunda Kwa Tanzania kuzipiku Kenya na Ivory Coast kuwa namba 3 wa Kuzalisha Kawaha Afrika nzima.
Hongera sana SSH Kwa utashi wa Kisiasa, hongera Waziri Bashe na hongera wakulima hata kama Chadomo Watachukia 😂
Tuna kazi ya kufanya kuwapita Uganda & Ethiopia
View: https://www.threads.com/@statsfrica/post/DL43rrOtze2?xmt=AQF0ylHZJJdF7ncGFuEAgqtm5KtFVUNDuW3_rbJkheL4Tg
==============
Tanzania inashika nafasi ya tatu barani Afrika kwa uzalishaji wa zao la Kahawa hapa nchini, ikizipiku nchi za Kenya na Ivory Coast zilizokuwa nafasi za juu kwa uzalishaji wa zao hilo Afrika.
Hayo yalibainishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayeshughulikia Ushirika na Umwagiliaji, Dkt. Stephen Nindi wakati akifunga Mkutano Mkuu wa 15 wa Bodi ya Kahawa nchini kwa niaba ya waziri wa kilimo, uliofanyika jana jijini Dodoma.
Dkt. Nindi amesema serikali itaendelea kutafuta masoko ya zao la Kahawa katika nchi mbalimbali barani Afrika na nje ya bara la Afrika, ili kuhakikisha inawainua kiuchumi wakulima mbalimbali hapa nchini lakini pia kuongeza mapato.
Aidha amesema lengo la serikali ni kuona kahawa ya hapa nchini inazidi kupata soko katika nchi tofauti ili wazidi kupanua wigo wa soko la zao la Kahawa duniani kote na kuongeza kuwa lengo ni kuona Kahawa ya Tanzania inatumika sehemu mbalimbali.
Kutokana na hilo, ameviagiza vyama vya Ushirika hapa nchini kuhakikisha vinashirikiana na Bodi ya Kahawa kuhakikisha wanasonga mbele ikiwemo kutatua changamoto ndogo ambazo wanakutana nazo wakulima ili kuendeleza tasnia ya kahawa.
Amesema pia serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa kahawa ili kuhakikisha zao hilo linakuwa na mchango mkubwa katika uchumi wa nchi hii ikiwemo kuongeza kuchangia pato la taifa kupitia mauzo ya ndani na nje ya nchi.
Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Kahawa nchini Primus Kimaryo amesema Bodi hiyo inaendelea kuweka mikakati ya kuimarisha kilimo cha zao hilo ili kufikia malengo ya kuongeza uzalishaji katika maeneo mbalimbali.
Kimaryo amesema Bodi hiyo ilijiwekea kufikia tani 300,000 ndani ya miaka mitano lakini hazijafika na kuongeza wanarudi kujipanga upya ili waweze kufikia mkakati wa kuzalisha tani hizo.