๐—ง๐—ฎ๐—ป๐˜‡๐—ฎ๐—ป๐—ถ๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ๐—ป๐—ด๐—ฎ๐—ฟ๐—ฎ ๐—บ๐—ฎ๐˜€๐—ต๐—ถ๐—ป๐—ฑ๐—ฎ๐—ป๐—ผ ๐˜†๐—ฎ ๐—ง๐—ฒ๐—ต๐—ฎ๐—บ๐—ฎ ๐—–๐—ต๐—ถ๐—ป๐—ฎ

๐—ง๐—ฎ๐—ป๐˜‡๐—ฎ๐—ป๐—ถ๐—ฎ ๐˜†๐—ฎ๐—ป๐—ด๐—ฎ๐—ฟ๐—ฎ ๐—บ๐—ฎ๐˜€๐—ต๐—ถ๐—ป๐—ฑ๐—ฎ๐—ป๐—ผ ๐˜†๐—ฎ ๐—ง๐—ฒ๐—ต๐—ฎ๐—บ๐—ฎ ๐—–๐—ต๐—ถ๐—ป๐—ฎ

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
1,221
Reaction score
2,425
1_20250603_174233_0000.png


Wanafunzi na wakufunzi toka vyuo vikuu nchini Tanzania wameibuka washindi wakuu katika mashindano ya Masuala ya Teknolojia ya Huawei ICT ya mwaka 2024 - 2025 wakiwashinda washiriki wengine zaidi ya 210,000 toka Ulimwengu kote Duniani.

3_20250603_174234_0002.png
2_20250603_174233_0001.png


Ni fainal ambayo iliweza kufanyika Kwenye nchi ya China kupitia Jiji la Shenzhen ambapo wanafunzi Toka DIT, UDSM na UDOM wamefanikiwa kujishindia tuzo Baada ya kushika nafasi ya pili.

4_20250603_174234_0003.png


Ni mashindano ambayo yako chini ya Huawei Technologies yanayolenga kuwapa wanafunzi mafunzo ya ujuzi kwa vitendo kupitia Teknolojia ya akili bandia (AI) , Big data na cloud's storage.

5_20250603_174234_0004.png


Pamoja na kukuza ubunifu wa kutatua changamoto halisi kupitia sekta ya kilimo, afya na elimu.Washindi hao wameonyesha kuwa mafanikio hayo yanaonyesha uwezo wa Tanzania kushindana kimataifa katika sekta ya Teknolojia.
 
Alafu kuna wajinga wanadharau vyuo vyetu, mwisho unakuta vijana wanabaki kufanya kazi China
 
Tanzania yashika nafasi ya pili kati ya washiriki 210,000 toka ulimwengu kote duniani..๐Ÿ‘†

Hii mbona haieleweki, yalikuwa mashindano ya nchi na nchi? kama Tanzania imekuwa ya pili sema ni nchi ngapi ziliingia kwenyehayo mashindano.. labda Tanzania imekuwa ya pili kati ya nchi 30... sasa unasema Tanzania imekuwa ya pili kati ya washiriki 210,000 au mimi ndio sielewi...

Na huo ushindi wameshinda kwenye tech ipi au kitengo kipi?
 
Kwa uelewa wako hao UDOM, DIT na UDSM wana mtaala wa Tanzania au China?
Hao hua wanasoma course maalum za huawei. Hizo course hutolewa na huawei wenyewe kulingana na technolojia yao wanayotaka waijue. Tafuta mtandaoni huawei Talent au ICT Competition ujifunze zaidi. Hawasomi somi tu madesa ya bongo na kwenda huko. Ni course specific za huawei wenyewe. Na zaidi wamefingua center kwenye hivyo vyuo vyote na vifaaa wameweka๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ
 
Hao hua wanasoma course maalum za huawei. Hizo course hutolewa na huawei wenyewe kulingana na technolojia yao wanayotaka waijue. Tafuta mtandaoni huawei Talent au ICT Competition ujifunze zaidi. Hawasomi somi tu madesa ya bongo na kwenda huko. Ni course specific za huawei wenyewe. Na zaidi wamefingua center kwenye hivyo vyuo vyote na vifaaa wameweka๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ
Ongezea na mitihani wanafanya kuwapata wanaowataka tena inakua online ๐Ÿƒ๐Ÿƒ
 
Hao hua wanasoma course maalum za huawei. Hizo course hutolewa na huawei wenyewe kulingana na technolojia yao wanayotaka waijue. Tafuta mtandaoni huawei Talent au ICT Competition ujifunze zaidi. Hawasomi somi tu madesa ya bongo na kwenda huko. Ni course specific za huawei wenyewe. Na zaidi wamefingua center kwenye hivyo vyuo vyote na vifaaa wameweka๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ˜ƒ
Sawa mkuu. Kuna jamaa yangu anacho cheti cha Huawei ila alikipata baada ya kusoma Degree DIT. Hakutoka Form VI kwenda kusoma online Huawei, hao hakuna aliyetoka First year hajui chochote akaenda kusoma huo unaoita mtaala wa China wa Huawei. Bila UDSM, DIT na UDOM hao wasingefanya kitu kwa Huawei.

Hata kuna family friend mtu mzima alienda Japan kusomea mifumo ya Hitachi na akaenda Ujerumani kusomea mifumo ya Siemens kwenye vifaa tiba. Haimaanishi walimuokota vichochoroni akiwa kilaza wakamfundisha, alikuwa tiyari na elimu ya Biomedical Engineering ambayo hakusomea Ujerumani wala Japan.
 
Sawa mkuu. Kuna jamaa yangu anacho cheti cha Huawei ila alikipata baada ya kusoma Degree DIT. Hakutoka Form VI kwenda kusoma online Huawei, hao hakuna aliyetoka First year hajui chochote akaenda kusoma huo unaoita mtaala wa China wa Huawei. Bila UDSM, DIT na UDOM hao wasingefanya kitu kwa Huawei.

Hata kuna family friend mtu mzima alienda Japan kusomea mifumo ya Hitachi na akaenda Ujerumani kusomea mifumo ya Siemens kwenye vifaa tiba. Haimaanishi walimuokota vichochoroni akiwa kilaza wakamfundisha, alikuwa tiyari na elimu ya Biomedical Engineering ambayo hakusomea Ujerumani wala Japan.
Sawa mkuu. Kwahiyo ni ushirikiano wa wachina na sisi. Lakini elimu yetu bado inasuasua hasa upande wa elimu kwa vitendo, ndio maana hao huawei wametengeneza lab na kuweka vifaa wenyewe kwewnye hivyo vyuo. Unafikiri wangewaacha tu na hii ya kwetu ma madesa kwenye karatasi wangetoboa?
 
Back
Top Bottom