Kitimoto
JF-Expert Member
- Aug 25, 2012
- 5,045
- 4,701
Chama cha Wafugaji Nguruwe Tanzania (TAFIPA) kimesema wastani wa tani 52,000 za nyama ya nguruwe huingizwa nchini kila mwaka kutoka nje ya nchi, huku Tanzania ikizalisha tani 27,000 pekee.
Katibu wa chama hicho, Collins Ritenga amesema leo Jumamosi Mei 6, 2023 kwenye mkutano ulioratibiwa na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) ukihusisha wafugaji na wafanyabishara wanyama hao kutoka Mikoa ya Mbeya, Iringa, Katavi na Rukwa.
Kikao hicho kimelenga kujadili na kuweka mikakati ya pamoja ya kuthibiti na kukabiliana na ugonjwa wa homa kali ya mafuta ya nguruwe ambao umekuwa ni changamoto katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
“Licha ya jitihada kubwa za wananchi kujihusisha na ufugaji wa nguruwe, bado kuna changamoto ya kutofikia malengo ya uzalishaji wa kibiashara kama mataifa mengine, ikiwepo ufugaji wa mazoea unaochangia kupata changamoto za ugonjwa wa homa ya mafuta ya nguruwe,” amesema.
Ameongeza kuwa ujio wa FAO huenda ukawa mwarobaini kwa wafugaji kuondokana na ufugaji wa mazoea ikiwepo changamoto za kukabiliana na ugonjwa hho ambao umekuwa ukiathiri sana sekta ndogo ya ufugaji nguruwe nchini.
Mwananchi