Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
SHIRIKA la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), limesema Tanzania imeendelea kufanya vyema kiuchumi, licha ya changamoto kadhaa inazolikabili. Kwa mujibu wa ripoti ya Maendeleo Duniani ya mwaka 2011, iliyotolewa na UNDP jana mjini Dar es Salaam, Tanzania imeshika nafasi ya 152 kati ya 187, zilizofanyiwa utafiti, huku hali ya ukuaji wa uchumi wake ikielezwa kuendelea kukua kwa kasi.
Ripoti hiyo iliyozinduliwa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Servacius Likwelile, imeionyesha Tanzania ni miongoni mwa nchi 10 ambazo uchumi wake unakua kwa kasi katika kipindi cha miaka mitano mfululizo. Nchi zingine pamoja na viwango vya ukuaji wake katika mabano, Cuba (kati ya asilimia 10 hadi 51) Venezuela na Tanzania (kati ya asilimia 7 na 73).
Aidha, nchi 10 ambazo zinashikilia mkia katika ripoti hiyo ni Guinea, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Sierra Lione, Burkinafaso, Liberia, Chad, Msumbiji, Burundi, Niger na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo ni ya mwisho. Akizungumzia ripoti hiyo, Likwelile, alisema inatoa changamoto kwa Tanzania na kuhakikisha inaimarisha njia za kiuchumi ili kufika mbali zaidi na kustawisha maendeleo ya Watanzania.
Likwelile alisema licha ya mafanikio yanayoonekana, Tanzania bado inakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo ya miundombinu ambayo ni eneo muhimu katika kuimarisha sekta ya uchumi.
Hata hivyo, UNDP katika kaulimbiu yake ya mwaka huu ambayo ni "Uendelevu wa Usawa na Mustakabali Bora kwa Wote," inataka mafanikio ya kiuchumi yanayopatikana yaonyeshe athari kwa wananchi wote.
Katika ripoti nchi za Norway, Australia na Netherland, ziliongoza kwa kuwa na uchumi imara huku mataifa makubwa ikiwemo Marekani, Ujerumani, Canada, Ireland na Sweeden, yakitupwa nje kutoka katika orodha ya nchi 10 bora.
Mungu Ibariki Tanzania
Ripoti hiyo iliyozinduliwa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Servacius Likwelile, imeionyesha Tanzania ni miongoni mwa nchi 10 ambazo uchumi wake unakua kwa kasi katika kipindi cha miaka mitano mfululizo. Nchi zingine pamoja na viwango vya ukuaji wake katika mabano, Cuba (kati ya asilimia 10 hadi 51) Venezuela na Tanzania (kati ya asilimia 7 na 73).
Aidha, nchi 10 ambazo zinashikilia mkia katika ripoti hiyo ni Guinea, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Sierra Lione, Burkinafaso, Liberia, Chad, Msumbiji, Burundi, Niger na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo ni ya mwisho. Akizungumzia ripoti hiyo, Likwelile, alisema inatoa changamoto kwa Tanzania na kuhakikisha inaimarisha njia za kiuchumi ili kufika mbali zaidi na kustawisha maendeleo ya Watanzania.
Likwelile alisema licha ya mafanikio yanayoonekana, Tanzania bado inakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo ya miundombinu ambayo ni eneo muhimu katika kuimarisha sekta ya uchumi.
Hata hivyo, UNDP katika kaulimbiu yake ya mwaka huu ambayo ni "Uendelevu wa Usawa na Mustakabali Bora kwa Wote," inataka mafanikio ya kiuchumi yanayopatikana yaonyeshe athari kwa wananchi wote.
Katika ripoti nchi za Norway, Australia na Netherland, ziliongoza kwa kuwa na uchumi imara huku mataifa makubwa ikiwemo Marekani, Ujerumani, Canada, Ireland na Sweeden, yakitupwa nje kutoka katika orodha ya nchi 10 bora.
Mungu Ibariki Tanzania