Tanzania tumenufaika nini kwa uwekezaji huko Loliondo na Ngorongoro?

Ileje

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,801
12,247
Nimekuwa nikijiuliza: Tanzania kama Taifa huru tunanufaika nini na uwekezaji unaofanyika Loliondo na Ngorongoro?

Najiuliza swali hili kutokana na mateso na manyanyaso ambayo inaelezwa wenzetu Wamasai wanapata kutoka kwa vyombo vyetu vya dola vikiwemo Polisi, JWTZ na Askari wa TANAPA.

Inaelezwa kuwa Wamasai wanapigwa risasi, mabomu, mijeredi na kunyimwa chakula ili kuwalazimisha kuhama katika maeneo yao ya asili! Inadaiwa Wamasai wanawindwa kama Swala mwituni, wanafungwa Magerezani, wanapotezwa kusikojulikana yaani ni mateso kwa kwenda mbele kama siyo wananchi, kama siyo watu na kama wahaini wanaotaka kupindua Serikali!

Kama ni fedha ni kiasi gani hicho ambacho Serikali ya Samia inajivua utu hadi kudaiwa kutekeleza mauaji ya kutisha kwa raia wake?

Kwamba sasa Serikali inaondoa huduma zote za jamii kama elimu, afya na utawala ili kupisha wawekezaji! Kwamba fedha na wawekezaji wana thamani kuzidi wananchi wake na utu wa binadamu?

Waandishi wa habari mna mchango mkubwa sana katika madhila na mateso yanayowapata wamasai. Mnalipwa na Serikali kuandika uongo kwa ajili ya matumbo yenu! Mmesahau majukumu yenu ya kutoa taarifa za ukweli bila upendeleo kwa sababu ya fedha! Ninyi pia ni wauaji wakubwa! Mateso ya wamasai yatawafuata na hakika malipo yenu yapo hapa hapa duniani!

Iwapo yanayodaiwa ni kweli, Serikali ya Samia acha kutoa mateso kwa raia wako. Wamasai ni raia na zaidi ya yote ni binadamu wanastahili kutendewa utu! Mbaya zaidi mnawaondoa wamasai mnapeleka watu wenu, mngeeleweka kama mngeacha mapori wazi!

Hakika Mungu yupo na anawaona!


View: https://twitter.com/BabaMwita/status/1694667616298655855?t=8MXbt0ZGvUwr2FnVCpnfpA&s=09
 
Hapo wanaonufaika ni Waarabu tu na baadhi ya Watwana wao. Hao Wamasai hawana chao. Nakumbuka waliingia rasmi nchini wakati wa awamu ya pili kupitia mkataba wa Kimangungo, kama huu wa DP WORLD.

Si unajua ule msemo wa Waarabu ni ndugu zetu? Halafu Wamasai eti ni wahamiaji haramu/wavamizi kutoka Kenya!
 
Hapo wanaonufaika ni Waarabu tu na baadhi ya Watwana wao. Hao Wamasai hawana chao. Nakumbuka waliingia rasmi nchini wakati wa awamu ya pili kupitia mkataba wa Kimangungo, kama huu wa DP WORLD.

Si unajua ule msemo wa Waarabu ni ndugu zetu? Halafu Wamasai eti ni wahamiaji haramu/wavamizi kutoka Kenya!
Inasikitisha Sana hii
 
Wananchi tumezidi sana uwoga.nguvu ya umma ikiamua hakuna cha polisi jeshi au nani anayeweza kuzuia.wananchi wanatakiwa kushirikaian kuwakabili hawa wauza nchi kw a nguvu zote
Hiki ndio kirusi kikubwa kinachotafuna taifa hili, uoga na ujinga wa wananchi, bahati nzuri hao wanaojiita viongozi wanalijua hili, watanzania tusipoacha uoga, tutamaliza kulia tukiwa tumeuziwa hadi vijiko vyetu majumbani!
 
Hakuna kitu maana nchi inategemea zaidi TOZO, POMBE, KAMARI, SIGARA na WAFANYAKAZI.

IMG_20230810_185040.jpg
 
wana mkataba toka enzi za mwinyi, walipewa miaka 100 hao, sasa jaribu kuwatoa halafu tuone kama kuna mswahili ataingia dubai kununua visimu vyenu vya bei poa
Sasa hivi wameshafikisha miaka mingapi?
Mapato na matumizi wanayatolea wapi?,maana sijawahi kuwasikia kwenye bajeti ya nchi wakiongelea mapato toka Loliondo.
 
Wananchi tumezidi sana uwoga.nguvu ya umma ikiamua hakuna cha polisi jeshi au nani anayeweza kuzuia.wananchi wanatakiwa kushirikaian kuwakabili hawa wauza nchi kw a nguvu zote
Hilo ni gumu kwa kuwa watawala washajua udhaifu wa raia ulipo. Wakiona wanapingwa kwa hoja wakakosa majibu wanapenyeza udini. Oooh, hao wanapinga kwa kuwa anayeuza nchi siyo wa dini yao!
 
Kama ni fedha ni kiasi gani hicho ambacho serikali ya Samia inajivua utu hadi kutekeleza mauaji ya kutisha kwa raia wake? Kwamba sasa serikali inaondoa huduma zote za jamii kama elimu, afya na utawala ili kupisha wawekezaji! Kwamba fedha na wawekezaji wana thamani kuzidi wananchi wake na utu wa binadamu!
FaizaFoxy
Njoo ufafanue huku
 
Back
Top Bottom