Tanzania sio Mwanza pekee Rais Magufuli!

Tanzania sio Mwanza pekee Rais Magufuli!

Wick

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2012
Posts
8,312
Reaction score
12,194
Declaration of Interest

Mimi kwa kabila ni Msukuma na nafurahia kuwa Msukuma lakini nililelewa kutambua kila kanda, mkoa, eneo Tanzania lina haki sawa kimaendeleo, kiuchumi, kisiasa etc.

Nimeanza kudeclare interest ili wale wasukuma wenzangu msije anza kejeli na matusi.
**********************************

Leo nimesikia habari mheshimiwa JPM katua Mkoani Mwanza na kafika uwanja wa Ndege Mwaka akakataza Mamlaka ya Usafiri wa Anga na Viwanja vya ndege kutohamisha watu kupisha ujenzi wa uwanja wa Ndege Mwanza!, moja ya hoja niliyoisikia ni kwamba walimpigia kura halafu ni kaya nyingi sana!.

Mheshimiwa kwa hili umekosea sana na kumbuka kila unalosema linaingia kwenye record sasa haya mambo ya kila kinachoendelea kanda ya ziwa unayaangalia kwa jicho la upole lakini ukija sehemu nyingine unaona kama wanaishi watoto wa nje ya ndoa hii sio haki kabisa!

Hao watu wa Mwanza ni nusu ya watu wote Tanzania ambao waliamini wanachagua Raisi mchapakazi ma sio mkanda!. Leo unatuletea ukanda baada ya kupata madaraka. Ilianza wamachinga watu tukakaa kimya tukiamini kawaida ikaja bomoa ya wananchi Mwanza ukazuia kisa wapiga kura wako, Mara uwanja wa ndege Chatto ambao wengine tunaweza tusiutembelee japo tumejifunga macho tukiamini umelenga madini yetu!

Wananchi wa jangwani walibomolewa nyumba zao bila fidia na ukali kalia kimya bila tamko lolote, walikuwa na familia zao, wengine wajawazito leo hii wamegeuka omba omba na watangaji wasiokuwa na uhakika wa pakulala. Kimara kulikuwa hakuna ulazima wa kuhamisha watu kwa nguvu bila malipo lakini kilichofanyika inajulikana. Ubungo mkaja na matamko ya kukinzana mara "usipobomoa tukaja bomoa, utatulipa!" watu tukaogopa tukabomoa wenyewe vibanda vyetu baadae linakuja jitu na barua eti "sikuwapa taarifa mbomoe niliwaambia subirini utaratibu" shubaamit!.

Kagera umekaa kimya fidia na michango ya watu, wameteseka wakazoea lakini kidonda kinapoanza kupona unawatonesha kwa kutetea wengine kiboya kabisa!.. Mheshimiwa wengine ni watu pia na Tanzania sio Mwanza pekee ni Sehemu zote zina haki sawa!. 2020 utakuja na mbinu gani?

[HASHTAG]#HapaKaziTu[/HASHTAG]! naona ni kama [HASHTAG]#HapaMwanzaTu[/HASHTAG]. Halafu wote tuna furastuesheni kama wewe hebu tusaidie tuone wajukuu zetu mheshimiwa!..Wale masikini ulioamini wataweza ishi kama wafanyakazi wa malaika tumekua majinamizi kabisa leo!

Vile vihela tulivyojibana enzi za vasco da gama kuweka labda tuje panda ndege zetu wakati wa kuja kusalimia Mwanza leo ukiuliza vimeenda wapi hatutakueleza lakini bado hakyanani Mungu anajua hatukuwa wezi au mafisadi!

Ifike kipindi huu mchakato wa Katiba tuufanyie hima raisi apunguziwe madaraka yake naona kwa wengine inakua too much sasa!

TOO MUCH POWER CORUPT ABSOLUTELY!
 
Bora angetoa kauli nyingine lakini sio Eti Hawa ndio walionipa kura
Uwanja wa musoma wa nyakatende ulifanyiwa uthamin tangu nwaka 2009 lkn hawajalipa na sasa haujengwi kwa sababu fedha sake zimeenda chato na pili mkoa wa Mara hatukumpigia kura Bali tulibanana na cdm.
Na ndio mpka Leo hajai kukanyaga na wazir kaja January tangu aingie madaraka na makamu naye kaja Mara moja,
Hivyo mm naelewa magu anachosema na mwanza ndio waliompa kura na ndio wengi ndugu zake anaowaamin.
Mwanza wasukuma ndio mawazir wake
 
Declaration of Interest

Mimi kwa kabila ni Msukuma na nafurahia kuwa Msukuma lakini nililelewa kutambua kila kanda, mkoa, eneo Tanzania lina haki sawa kimaendeleo, kiuchumi, kisiasa etc.

Nimeanza kudeclare interest ili wale wasukuma wenzangu msije anza kejeli na matusi.
**********************************

Leo nimesikia habari mheshimiwa JPM katua Mkoani Mwanza na kafika uwanja wa Ndege Mwaka akakataza Mamlaka ya Usafiri wa Anga na Viwanja vya ndege kutohamisha watu kupisha ujenzi wa uwanja wa Ndege Mwanza!, moja ya hoja niliyoisikia ni kwamba walimpigia kura, halafu ni kaya nyingi sana!

Mheshimiwa kwa hili umekosea sana na kumbuka kila unalosema linaingia kwenye record sasa haya mambo ya kila kinachoendelea kanda ya ziwa unayaangalia kwa jicho la upole lakini ukija sehemu nyingine unaona kama wanaishi watoto wa nje ya ndoa hii sio haki kabisa!

Hao watu wa Mwanza ni nusu ya watu wote Tanzania ambao waliamini wanachagua Raisi mchapakazi ma sio mkanda!. Leo unatuletea ukanda baada ya kupata madaraka. Ilianza wamachinga watu tukakaa kimya tukiamini kawaida ikaja bomoa ya wananchi Mwanza ukazuia kisa wapiga kura wako, Mara uwanja wa ndege Chatto ambao wengine tunaweza tusiutembelee japo tumejifunga macho tukiamini umelenga madini yetu!

Wananchi wa jangwani walibomolewa nyumba zao bila fidia na ukalikalia kimya bila tamko lolote, walikuwa na familia zao, wengine wajawazito leo hii wamegeuka omba omba na watangaji wasiojua uhakika wa kulala. Kimara kulikuwa hakuna ulazima wa kuhamisha watu kwa nguvu bila malipo lakini kilichofanyika inajulikana. Ubungo mkaja na matamko ya kukinzana mara "usipobomoa tukaja bomoa utatulipa!" watu tukaogopa tukaogopa tukabomoa wenyewe baadae linakuja jitu na barua eti "sikuwapa taarifa mbomoe niliwaambia subirini utaratibu" shubaamit!.

Kagera umekaa kimya fidia na michango ya watu, wameteseka wakazoea lakini kidonda kinapoanza kupona unawatonesha kwa kutetea wengine kiboya kabisa!.. Mheshimiwa wengine ni watu pia na Tanzania sio Mwanza pekee ni Sehemu zote zina haki sawa!. 2020 utakuja na mbinu gani?

[HASHTAG]#HapaKaziTu[/HASHTAG]! naona ni kama [HASHTAG]#HapaMwanzaTu[/HASHTAG]. Halafu wote tuna furastueni kama wewe hebu tusaidie tuone wajukuu zetu mheshimiwa!..Wale masikini uliamini wataweza ishi kama wafanyakazi wa malaika tumekua majinamizi kabisa leo!

Vile vihela tulivyojibana enzi za vasco da gama kuweka labda tuje panda ndege zetu wakati wa kuja Mwanza leo ukiuliza vimeenda wapi hatutakueleza lakini bado hakyanani Mungu anajua hatukuwa wezi au mafisadi!

Ifike kipindi huu mchakato wa Katiba tuufanyie hima raisi apunguziwe madaraka yake naona kwa wengine inakua too much sasa!

TOO MUCH POWER CORUPT ABSOLUTELY!
Kama inakuuma jitundike!! Nani kakuuliza wewe kabila gani?? Nyanoko!!
 
Wewe sio Msukuma. Msukuma hawezi kutoa lawama kwa kuangalia sentensi moja tu. Tafuta kabila lako huko huko chadema.
We lofa mie ni msukuma tena wa misungwi!!.. Halafu sijaangalia sentensi moja tu hebu nambie tamko gani mheshimiwa alilitoa watu wa jangwani dsm walipovunjiwa nyumba, watu wa ubungo alitoa tamko?, je watu wa kimara alisema nini?.. iweje inapokuja Mwanza anasimama!..
Na mie nimesimamia ishu hii ya kuijali sana Mwanza sikatai Nyumba ni Nyumbani lakini hakukuhitajika nguvu inayotumika hadi tunaona!.
Matokeo yake nikisimama na kujiita msukuma naonekana mkanda/katili/mbinafsi wakati hatupo hivyo!..
Wasukuma tupo almost Tanzania yote na tunajulikana wapole wajali maendeleo ya sehemu tulizopo lasivo tungekua tumeujenga sana ukanda huo kuliko mikoa tuliyopo!.
 
Back
Top Bottom