Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,195
- 10,709
Hivi karibuni, tumeshuhudia video mitandaoni kutoka kwa kina Photogenic Mtoto na kikosi chake. Wametupitisha kwenye madaraja ya kifahari ya meli mpya ya MV Mwanza "Hapa Kazi Tu", kuanzia VIP hadi daraja la kawaida.
Kusema kweli, meli ni nzuri sana! Ina mvuto wa aina yake, na kwa mbali unaweza kudhani ni hoteli ya nyota tano inayocheza sebene juu ya maji.
Katika hali ya kushangaza, video hizo zimejaa sifa kedekede kwa viongozi wa sasa, huku picha kubwa la Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba, likipepea kama bendera ya taifa. Sasa, jamani, hebu tuwe waungwana! Hata kama tunapenda "shobo" za kisiasa, kuna mahali penye ukweli wa kihistoria.
Wazo la ujenzi wa MV Mwanza halikuzaliwa juzi kwenye kikao cha baraza la mawaziri aliloliteua Samia. Huu ulikuwa ni mpango mkakati, ndoto, na jasho la Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. Ni yeye aliyepiga msumari wa kwanza wa ahadi hiyo, akiamini kuwa Warangi, Wakerewe, Wamaasai, Wahehe, Wajita, na Wasukuma wanastahili usafiri wa hadhi ya ndege ndani ya maji.
Lakini kama usemavyo mtaani, "Internet never forgets" (Mtandao hausahau). Wakati kina Photogenic Mtoto wakijaribu kupaka rangi mpya kwenye ukuta wa zamani, Watanzania kwenye comments wamegeuka kuwa walimu wa historia.
Inafurahisha kuona jinsi wananchi walivyowatandika "makavu" live! "Ebo! Meli ni ya Magufuli, sifa mnampelea Mwigulu? Kwani Mwigulu ndiye aliyeweka msingi wa ujenzi huu?"
Wapo wengine wameenda mbali na kusema kuwa hata kama meli imekamilika chini ya Rais Samia (ambaye anastahili sifa kwa kuendeleza miradi), mzizi wa mradi huu una chapa ya chuma ya JPM, na anapaswa kutajwa wazi.
Mpeni Kaisari Kilicho cha Kaisari.
Ubunifu wa maudhui usitufanye tuwe viziwi wa historia. Unaweza kupiga picha nzuri, lakini ukishindwa kusema ukweli, picha yako inapoteza kabsa uaminifu. MV Mwanza ni baraka tulizozipata kutokana na maono ya Hayati Magufuli, na ni vyema influencers wetu wakajifunza kutofautisha kati ya "anayekamilisha mradi" na "aliyeasisi ndoto."
Vinginevyo, tutaanza kuamini kuwa siku hizi hata mvua ikinyesha, influencers watasema ni jitihada za wizara ya Maji, na si baraka za Mungu.
Kusema kweli, meli ni nzuri sana! Ina mvuto wa aina yake, na kwa mbali unaweza kudhani ni hoteli ya nyota tano inayocheza sebene juu ya maji.
Katika hali ya kushangaza, video hizo zimejaa sifa kedekede kwa viongozi wa sasa, huku picha kubwa la Waziri Mkuu, Mwigulu Nchemba, likipepea kama bendera ya taifa. Sasa, jamani, hebu tuwe waungwana! Hata kama tunapenda "shobo" za kisiasa, kuna mahali penye ukweli wa kihistoria.
Wazo la ujenzi wa MV Mwanza halikuzaliwa juzi kwenye kikao cha baraza la mawaziri aliloliteua Samia. Huu ulikuwa ni mpango mkakati, ndoto, na jasho la Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. Ni yeye aliyepiga msumari wa kwanza wa ahadi hiyo, akiamini kuwa Warangi, Wakerewe, Wamaasai, Wahehe, Wajita, na Wasukuma wanastahili usafiri wa hadhi ya ndege ndani ya maji.
Lakini kama usemavyo mtaani, "Internet never forgets" (Mtandao hausahau). Wakati kina Photogenic Mtoto wakijaribu kupaka rangi mpya kwenye ukuta wa zamani, Watanzania kwenye comments wamegeuka kuwa walimu wa historia.
Inafurahisha kuona jinsi wananchi walivyowatandika "makavu" live! "Ebo! Meli ni ya Magufuli, sifa mnampelea Mwigulu? Kwani Mwigulu ndiye aliyeweka msingi wa ujenzi huu?"
Wapo wengine wameenda mbali na kusema kuwa hata kama meli imekamilika chini ya Rais Samia (ambaye anastahili sifa kwa kuendeleza miradi), mzizi wa mradi huu una chapa ya chuma ya JPM, na anapaswa kutajwa wazi.
Mpeni Kaisari Kilicho cha Kaisari.
Ubunifu wa maudhui usitufanye tuwe viziwi wa historia. Unaweza kupiga picha nzuri, lakini ukishindwa kusema ukweli, picha yako inapoteza kabsa uaminifu. MV Mwanza ni baraka tulizozipata kutokana na maono ya Hayati Magufuli, na ni vyema influencers wetu wakajifunza kutofautisha kati ya "anayekamilisha mradi" na "aliyeasisi ndoto."
Vinginevyo, tutaanza kuamini kuwa siku hizi hata mvua ikinyesha, influencers watasema ni jitihada za wizara ya Maji, na si baraka za Mungu.