waltham,
..Tanzania ina vivutio vyote ambavyo viko kwa majirani zenu. Mtalii akifika Tanzania ataweza kuona gorillas, wanyama, fukwe za bahari, na kupanda mlima Kilimanjaro, hivyo kutokuwa na ulazima wa kutembelea Kenya, Uganda, au Rwanda.
..also, katika revenues zinazotokana na tourist sector, Tanzania ndiyo inapata mapato makubwa kushinda wenzetu wa Afrika Mashariki. kwa msingi huo so far tunaona we are on the right track, tunachotakiwa kufanya ni kuboresha huduma zetu na kuwa more creative and aggressive kujitangaza zaidi.
..kuhusu LAND huku Tanzania kuna matatizo makubwa ya ardhi sasa hivi. kama utakuwa unafuatilia vyombo vya habari kuna mapigano ya mara kwa mara kati ya wakulima na wafugaji. katika hali kama hiyo siyo busara kufungua mipaka yetu na kuruhusu wageni toka nchi majirani kumiliki ardhi huku Tanzania.
..asilimia kubwa ya wa-Tanzania ni wakulima na wafugaji wadogo wadogo hivyo access to the land is key to their sustenance. Watanzania wanaamini sheria[land laws] za umiliki ardhi za Kenya na Uganda zinamkandamiza mtu wa chini. Hali hiyo ndiyo inayosababisha wa-Tanzania wawe wakali every time it is suggested kwamba ardhi iwe suala la East African community.
..The fact kwamba Kenya na Uganda mlifikia kupigana vita kuhusu eneo dogo la ardhi ktk kisiwa cha Migingo halileti picha nzuri kwa wa-Tanzania.
..Siyo kweli kwamba wa-Tanzania hatutaki ushirikiano na majirani zetu. Kenya inashika nafasi ya pili kati ya wawekezaji wa nje nchini Tanzania. Tungekuwa hatutaki ushirikiano na majirani zetu tusingeruhusu hali hiyo. Mimi nadhani wa-Kenya mnatumia muda mwingi kuishambulia Tanzania instead of looking at the bright side of the relations btn our two countries.
..Kuhusu makao makuu ya EAC kuhamishwa toka Arusha, sidhani kama wa-Tanzania wata-object ikiwa uamuzi huo utakuwa umefanyika ktk mazingira ya kindugu kwa manufaa ya jumuiya yetu.
cc
Geza Ulole,
Ngongo,
Mungi