Tanzania na Finland kuimarisha Ushirikiano katika Usimamizi wa Amani na Usuluhishi wa migogoro

Tanzania na Finland kuimarisha Ushirikiano katika Usimamizi wa Amani na Usuluhishi wa migogoro

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,770
Reaction score
1,173
Tanzania na Finland kuimarisha Ushirikiano katika Usimamizi wa Amani na Usuluhishi wa migogoro

Rais wa Jamhuri ya Finland, Mhe. Alexander Stubb amesema Serikali ya Finland itaendelea kuimarisha ushirikiano na Tanzania ili kuhakikisha juhudi za pamoja zinatekelezwa katika usimamizi wa amani na usuluhishi wa migogoro Barani Afrika na duniani kwa ujumla.

publer-1747350249373.jpg
Mhe. Rais Stubb ameyasema hayo Mei 15, 2025 wakati akifungua semina ya kuenzi mchango wa Rais wa zamani wa Jamhuri ya Finland, Hayati Martti Ahtisaari katika kuleta amani na upatanishi duniani, iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Mhe. Rais Stubb amesema kuwa, Hayati Martti Ahtisaari ni hazina na mwongozo kwa dunia ya leo, kwani aliifuindisha Dunia kuwa amani ni kitu kinachowezekana, kama watatuzi wa amani watakuwa tayari kusikilizana na kushirikiana kwa dhati.

“Hayati Ahtisaari, alijulikana kwa juhudi zake za kusuluhisha migogoro katika nchi za Kosovo, Namibia, na jimbo la Aceh nchini Indonesia, ambapo alitumia njia ya mazungumzo na maridhiano, katika kuleta usuluhu endelevu kwenye maeneo yaliyoathirika na migogoro ya muda mrefu” alifafanua Mhe. Rais Stubb.

publer-1747350261752.jpg
Awali, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), ameishukuru Finland kwa ushirikiano na mchango wake katika miradi ya maendeleo nchini na ufadhili wa program mbalimbali katika Taasisi ya Uongozi na Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahamed Salim, hatua ambayo imeimarisha utekelezaji wa majukumu ya taasisi hizo katika ngazi ya Kitaifa na Kimataifa.

publer-1747350254661.jpg
Kuhusu mchango wa Finland katika kukuza amani na utatuzi wa migogoro Waziri Kombo amesisitiza, Tanzania itaendelea kuwa mstari wa mbele katika juhudi za kutafuta amani, huku ikizingatia falsafa nne ambazo ni, Maridhiano, Ustahimilivu, Mageuzi na Kujenga upya taifa (4R), zilizoanzishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ili kujenga jamii zenye mshikamano na amani ya kudumu.

publer-1747350256423.jpg
publer-1747350258216.jpg
 

Attachments

  • publer-1747350265958.jpg
    publer-1747350265958.jpg
    65.7 KB · Views: 17
  • publer-1747350252957.jpg
    publer-1747350252957.jpg
    56.9 KB · Views: 15
  • publer-1747350247632.jpg
    publer-1747350247632.jpg
    69.4 KB · Views: 17
  • publer-1747350264239.jpg
    publer-1747350264239.jpg
    71.7 KB · Views: 14
  • publer-1747350271543.jpg
    publer-1747350271543.jpg
    92.6 KB · Views: 15
  • publer-1747350269528.jpg
    publer-1747350269528.jpg
    91 KB · Views: 18
  • publer-1747350273541.jpg
    publer-1747350273541.jpg
    93.9 KB · Views: 13
  • publer-1747350267767.jpg
    publer-1747350267767.jpg
    68.3 KB · Views: 17
  • publer-1747350277270.jpg
    publer-1747350277270.jpg
    83.3 KB · Views: 15
  • publer-1747350275500.jpg
    publer-1747350275500.jpg
    66.5 KB · Views: 15
Back
Top Bottom