Umekuwa msemaji wa jangili? Kinana alikiri kuwa meli ni yake. Haiwezekani mwenye meli asijue kilichobebwa na meli yake. Mara kadhaa meli zake zimekamatwa zikiwa zimebeba nyara za taifa naye hajakanusha. Wewe ni nani wa kukanusha? Pitia thread zake humu, zipo nyingi tu.Hakuna mahali ambapo kinana anahusika hapa.ni chuki tu na siasa za kupakana matope
kama inashindikana kuchukua hatua kwa watu wanopanga kuuwa watu,na ushahidi wanao.watachukuaje hatua kwa kuuwawa tembo myama. hii ni serikali ya kutoa madarakani.wanajeshi siwanaliona hili. ajabu watawaacha hao walioiba na kuuwa tembo wataanza kutuandama sisi tunaolalamikaKizazi cha sasa tumegubikwa na wimbi la uvivu wa kushughulisha bongo zetu, kila tunaloambiwa tunameza lilivyo bila kutafakari malengo ya anaeongea au kuandika
Kwani kinana ni kiongoz wa serikali, mbona hamueleweki,yakiwa kwenu mnataka yasingiliwe ila ya ccm nyie ndo mnataka muwe polisi,waendesha mashtaka,mawakili na hata mahakimu, kama mnaona KATIBU MKUU kakosa hamna haja ya kumwomba awajibike, mnachotakiwa kufanya nenden kunakohusika mkamshtaki sio kuchafuana bila sababu,.
Hapa niko nchini Hong Kong, taarifa za awali nilizo nazo ni kwamba: Kontena za meno (vipusa) ya ndovu zilizotangazwa kukamatwa huko china siyo mbili kama inavyojulikana. Hali halisi ni kwamba kontena zilizokamatwa ni kumi... lakini mchezo mchafu umechezwa na vigogo serikalini kuzima moto (soo) huo ili ionekane kuwa siyo nyingi kiviiile. Ikumbukwe kuwa Tanzania (serikali) ina-stack kubwa za meno ya tembo katika maghara yake. Ni miongoni mwa-stack hizo wajanja wamekwepua kontena 10. Vigogo wa sirikali wamo... Nafuatilia taarifa za kina zaidi nitaziweka jamvini ASAP... "TUNA MATATIZO MAKUBWA"
Mimi kizungu sikijui lakini mbona hapo hujaonesha ni jinsi gani kinana anahusika. Mmiliki wa meli anatakiwa kukagua mizigo kabla haijasafiri au? Msianzie kwa Kinana anzieni mwanzo. Kwani hao tembo waliuawa kurasini au meli za kinana zinaenda mpaka mbugani kupakia mizigo? Je afisa wanyapoli ni watoto wa kinana? Polisi wasiokagua magari njiani ni shemeji zake na Kinana? Maafisa forodha na TRA wa bandarini pamoja na watu wa usalama wa Taifa wanatokea ukoo wa Kinana? Msijedhani mie namtetea Kinana ila nataka tuanzie kwenye chanzo sio mwisho. Mnaodhani JK atasaidia kwenye hili mmenoa kwani alishawahi tamka kuwa analyo orodha ya watu wanaohusika na madawa ya kulevya lakini mpaka leo kimefanyika nini? Kama ni kulinganisha heli Tembo wote wafe lakini japo vijana 1000 wa kitanzania waokoke kutokana na madhara ya madawa ya kulevya.
Mimi kizungu sikijui lakini mbona hapo hujaonesha ni jinsi gani kinana anahusika. Mmiliki wa meli anatakiwa kukagua mizigo kabla haijasafiri au? Msianzie kwa Kinana anzieni mwanzo. Kwani hao tembo waliuawa kurasini au meli za kinana zinaenda mpaka mbugani kupakia mizigo? Je afisa wanyapoli ni watoto wa kinana? Polisi wasiokagua magari njiani ni shemeji zake na Kinana? Maafisa forodha na TRA wa bandarini pamoja na watu wa usalama wa Taifa wanatokea ukoo wa Kinana? Msijedhani mie namtetea Kinana ila nataka tuanzie kwenye chanzo sio mwisho. Mnaodhani JK atasaidia kwenye hili mmenoa kwani alishawahi tamka kuwa analyo orodha ya watu wanaohusika na madawa ya kulevya lakini mpaka leo kimefanyika nini? Kama ni kulinganisha heli Tembo wote wafe lakini japo vijana 1000 wa kitanzania waokoke kutokana na madhara ya madawa ya kulevya.
Wallisha anza ya Albino,tembo waishe tu ili tuangalie watafanya biashara gani
Hakuna mahali ambapo kinana anahusika hapa.ni chuki tu na siasa za kupakana matope
MKuu hili silijui ndoo unanipa picha wewe. Ila hoja yangu ni kwamba kwasasa serikali inameno ya tembo ambayo jumuia ya kimataifa wameikataza isiuze. sasa uuzaji wa chinichini unaweza kuhusishwa na pembe hizo. Hivyo basi kuuza pembe sio tatizo lakini inavyokuja kwenye madawa ya kulevya yanayoua na kuharibu vijana wetu huku mkulu akiwa anajua na ametulia kimya ni soo.Kwakuwa unajua wakala mkuu wa madawa ni Mtot wa JK unataka achukuliwe hatua kabla ya kinana kuadhibiwa amasivyo hapakaliki.
Wamekusikia.
La karatu tumelifunika na kulifumbia macho ee?