Tukiendelea kulalamika tu, na sisi tutakuwa wananchi dhaifu, hii haihitaji kusubiri 2015, sio suala lachadema, tunaongelea maslahi yetu na ya vizazi vijavyo wawe ccm au cdm.
India mtu kafa kwa kubakwa lakini tumeona wananchi walivyonyesha kwa vitendo jinsi ambavyo hakufurahishwa na hicho kitendo.
Napenda sana amani, lakini hii serikali haihitaji ustaarabu tena, kwa mwendo huu unadhani utawatoa madarakani kidiplomasia au kwa uchaguzi huru ambao haupo? mfumo wote wa serikali umeharibika.
Na hata hiyo katiba mpya ikija, kwangu naona tunapoteza hela bure, watu wanaivunja iliyopo na hakuna kitu kinafanyika.
Matatizo yetu sio ya katiba, ni ya kuwa na viongozi wasio na uzalendo na wapenda rushwa.