Tanzania: Maisha ya Tembo wetu hatarini!

Tanzania: Maisha ya Tembo wetu hatarini!

blueray

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2012
Posts
2,217
Reaction score
426
Kama hali hii ya ujangili wa tembo itaendelea basi mjue itachukua takriban miaka 5 hadi zaidi kidogo ya miaka 10 kwa tembo wetu kumalizika!

Ingawa ni taarifa ya January 2012 lakini majibu yake yameanza kujitokeza karibuni kwa kukamatwa mfululizo meli mbili (moja baada ya nyingine katika mwezi mmoja) huko Hongkong zilizosheheni nyara za taifa zenye thamani ya mabilioni ya pesa za kitanzania.

Hebu soma mwenyewe kipande cha hii taarifa;

The latest news is from Tanzania, where reports indicate that elephant numbers have fallen by as much as 42% over the past 3 years. This is a hugely significant number – almost half the Tanzanian elephant population!

The elephant census was carried out at the Selous Game Reserve and Mikumi National Park both important and protected game reserves in Tanzania. The census revealed elephant numbers had plunged from 74,900 in 2006 down to just 43,552 in 2009.

The census was carried out by the east African country's wildlife authority who are deeply concerned about the dwindling population and the escalation of poaching.

...The rapid fall prompted Tanzanian President Jakaya Kikwete to order an investigation, announced his office last Tuesday ( 03.01.2012)

Conservationists estimate Tanzania has a total elephant population of between 110,000 and 140,000

My take
Katika miaka 3 tu tembo wetu 31,348 wameuawa kwa ajili na kuvunwa pembe. Hii ina maana tembo 10,450 kila mwaka.

kwa hesabu ya haraka baada ya miaka 5 hadi 10 au zaidi kidogo watanzania tutakuwa hatuna tembo!

Kama inavyoonyesha hapo juu JK aliahidi kushughulikia hili swala takribani mwaka mmoja uliopita. Ingawa hatukuona kushughulikiwa kwake, ni dhahiri baada ya shehena mbili kubwa kukamatwa huko Hongkong ambapo wamiliki wa meli zilizotumika kufanyia uhalifu huo wanajulikana mmoja wa wamiliki hao akiwa ni Mh Kinana (Kama alivyokiri yeye mwenyewe) basi hata wenye mizigo nao wanajulikana. Pamoja na uchunguzi kuendelea bwana Kinana anapaswa kuwajibika kwa meli yake/zake kuhusishwa na biashara hii haramu.
Hata kama hatapatikana na hatia hii ni kashfa kubwa inayomweka doa kisiasa.

Vinginevyo tutahitimisha kwamba serikali yetu ni dhaifu sana; kama meli zinaweza kuingia Tanzania na kutoka bila kufahamika kilichopo kwenye meli hizo. Kwani hata makundi mengine ya uhalifu yanaweza kusafirisha hata silaha, madini nk kwa kupitia hizi meli za kina Kinana bila kujulikana.

Kwa kawaida chombo kinapokamatwa na nyara za taifa nacho huhusishwa moja kwa moja na pia huwa ni moja ya mashahidi muhimu in the court of law. Mfano mzuri ni 'Samaki wa Magufuli' meli haikuachiwa kwa sababu yenyewe ilitumika tu.

Wanajamvi mnaonaje hili swala limekaaje na nani awajibishwe. Tutafakari kwa manufaa ya nchi yetu sisi na vizazi vijavyo
 
Hawa kuwaacha kwenye uongozi majibu yake ndio hayo Raisi Kikwete sio tuu ameshindwa kuboresha maisha ya wananchi ameshindwa hata kulinda rasilimali zetu toka aingie madarakani 2005 Tembo kwa asilimia 42 wameshavunwa unadhani nani anafanya biashara hiyo itakuwa na mkono wake

Tanzanite imekuwa ikiuzwa nje na nchi za India kenya na South Africa nani anawafanya hawa wawe wauzaji wa Tanzanite wakati wao si wenye Tanzanite

Barrick kuongezewa mkataba wa uchimbaji bila hata Bunge Kuambia
Kukatwa pande la ardhi ya mbuga ya selous ili uvunaji wa uranium ufanyike huyu ni Raisi kweli tuliyempa dhamana au ni mhujumu uchumi
I wonder akili za watanzania halafu bado tko naye eti Kiongozi wa nchi ambaye approval rate ya utawala wake inashuka kila siku iendayo kwa Mungu
Kinana anaweza akawa anavuna kiasi anachotaka si amepewa kibali na mwenyekiti wake wa chama
 
Chama dhaifu! Serikali dhaifu! Wanachama dhaifu!

Unategemea hatua za dhati kuchukuliwa kweli?!
 
Hawa kuwaacha kwenye uongozi majibu yake ndio hayo Raisi Kikwete sio tuu ameshindwa kuboresha maisha ya wananchi ameshindwa hata kulinda rasilimali zetu toka aingie madarakani 2005 Tembo kwa asilimia 42 wameshavunwa unadhani nani anafanya biashara hiyo itakuwa na mkono wake

Tanzanite imekuwa ikiuzwa nje na nchi za India kenya na South Africa nani anawafanya hawa wawe wauzaji wa Tanzanite wakati wao si wenye Tanzanite

Barrick kuongezewa mkataba wa uchimbaji bila hata Bunge Kuambia
Kukatwa pande la ardhi ya mbuga ya selous ili uvunaji wa uranium ufanyike huyu ni Raisi kweli tuliyempa dhamana au ni mhujumu uchumi
I wonder akili za watanzania halafu bado tko naye eti Kiongozi wa nchi ambaye approval rate ya utawala wake inashuka kila siku iendayo kwa Mungu
Kinana anaweza akawa anavuna kiasi anachotaka si amepewa kibali na mwenyekiti wake wa chama

Inatia uchungu sana!

Kama unavyosema inawezekana hapa kuna go ahead ya mkuu.

Lakini ngoja tusubiri inawezekana pia akawajibishwa au kuwajibika mwenyewe
 
Hakuna mahali ambapo kinana anahusika hapa.ni chuki tu na siasa za kupakana matope
 
La karatu tumelifunika na kulifumbia macho ee?
 
Kama hali hii ya ujangili wa tembo itaendelea basi mjue itachukua takriban miaka 5 hadi zaidi kidogo ya miaka 10 kwa tembo wetu kumalizika!

Kwa taarifa zaidi unaweza kusoma hii taarifa hapa Tanzania

Mkuu source yako hii ni Blog kama tunavyoandika hapa JF.
 
Chama dhaifu! Serikali dhaifu! Wanachama dhaifu!

Unategemea hatua za dhati kuchukuliwa kweli?!

Ni kweli, ila pamoja na udhaifu wao kwa hili tuwape chansi tuone
 
Kinana na ukoo wa watoka somaliland wote ni ma poucher,sishangai.magamba wamejimaliza.
 
Hakuna mahali ambapo kinana anahusika hapa.ni chuki tu na siasa za kupakana matope

subiri pale wajukuu zako watakapokuja cholewa picha za tembo kama wanyama waliokuepo na wamepotea ndo utajua chuki binafsi
 
Kwa wengi tunaotumia usafiri wa umma aka public transport kila gari huandikwa abiria chunga mzigo wako...TANAPA wanapaswa kuchunga mizigo yetu
 
Inaelekea Kinana ana nyumba ndogo nyingi, naona anatetewa kwa mambo yaliyo dhahili.
 
Kwani kinana ni kiongoz wa serikali, mbona hamueleweki,yakiwa kwenu mnataka yasingiliwe ila ya CCM nyie ndo mnataka muwe polisi, waendesha mashtaka, mawakili na hata mahakimu, kama mnaona KATIBU MKUU kakosa hamna haja ya kumwomba awajibike, mnachotakiwa kufanya nendeni kunakohusika mkamshtaki sio kuchafuana bila sababu,.
 
Kizazi cha sasa tumegubikwa na wimbi la uvivu wa kushughulisha bongo zetu, kila tunaloambiwa tunameza lilivyo bila kutafakari malengo ya anaeongea au kuandika
 
Mkuu mtu akiamua kuchanganya mlenda na ndizi basi wacha iwe hivyo.Basi lishtakiwe kwa kuwa lina abiria aliyevuta bangi
Mkuu naona hapa umechanganya mambo.

Kwani kuzaa ukiwa padri ni kosa la jinai?
 
....kila mara nimekuwa nikisema kuwa dhambi kubwa kuliko zote Duniani ni Uoga na Hofu , hakuna gereza baya Duniani kama uoga na hofu na gereza hili limeweka watu vifungoni kwa muda mrefu bila wao kujua na huku wakitafakari na kuamini kuwa wako huru ...... woga na hofu ni dhambi kubwa kuliko dhambi zote Duniani

....mateso ya Maisha ya mwanadamu katika Taifa letu yanasababishwa na hofu na uoga ndio maana tunawajua wezi lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa dhidi yao kwa sababu ya hofu na uoga ya majina yao na vyeo vyao , huu ni upumbavu mkubwa sana.....


....G.LEMA..
 
Back
Top Bottom