Tanzania kwanza: Ndoto tunayotamani kwa manufaa ya nchi yetu

Malemi

New Member
May 5, 2021
1
0
Tanzania kwanza kwa neno hilo tu! Tunapata picha ya kizalendo na kitaifa inayo ibua hisia na kuleta maswali ya kwanini na lini kuhusu mstakabari makin na misingi imara ya kisiasa, kielimu, kiuchumi na kiutamaduni kwa Tanzania.

Ifikie mahali tukubali kuwa tumeshindwa kuipambania tanzania kwa kuijenga na kuwajenga Watanzania katika nyanja muhimu za kitaifa na kimataifa, sio kwamba hatuna viongozi imara, sera nzuri, wasome wenye taaruma mbalimba na Watanzania wenye vibaji maarum(GENIUS) wote hao tunao lakini hapa tulicho shindwa ni kujisacrifai(kujisadaka).

Ulimwengu wa sasa unahitaji high technology ili kuendesha maisha na uchumi wa nchi High technology inajumuisha uwepo wa vitu vyote walivyo navyo nchi tajiri kama viwanda kwa kila bidhaa, elimu kuzingatia ufupishwaji wa miaka mingi ya kusoma na, ujenzi wa aina yake unao fanywa na watu wetu wenyewe katika maeneo yote ya nchi yetu, uongozi bora kwa kuzingatia demokrasia na sera za taifa za kimaendeleo zilizo beba maono ya tanzania mpya na mambo mengi yatakayotoa fursa kwa wasomi wetu, vipaji maalim na wataarumu kutumika ndani ya nchi kulingana na uwezo wao kama ilivyo kwa nchi zilizo endelea.

Je, tunawezaje kuyapata yote hayo ambayo ni gharama kubwa sana? na Je, wenzetu walianzaje? sio kwamba hatuna majibu ya nini cha kufanya ila tumezoea kuwa watumwa wa wengine na Mwisho wa utumwa huu ni sisi wenyewe kuamua kuanzia Mheshimiwa Rais kwa maana ya SERIKALI na miimli ya BUNGE na MAHAKAMA.
 
Utumwa hauwezi kuishi kama Bi Mkubwa gesi yetu inasainiwa mkataba Kenya na wala haijulikani kuna nini within hizo kurasa za hila, like Mangungo Treaty. Kiswahili kinapigwa chini hata kwenye hotuba kwa Mzee M7 na majirani hapa kwa Mr Freedom.

Miradi mizuri aliyoianzisha JPM inapigwa vita left, right, centre --- hakuna kuitembelea wala kuikagua wala kuipatia kipaumbele. Sasa kwa mtaji huo, utumwa na utegemezi na ombaomba vitaishaje-ishaje!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom