Tanzania kupeleka vikosi vyake vya kijeshi Msumbiji

Kamanda Asiyechoka

JF-Expert Member
Sep 13, 2020
3,165
4,581
Tanzania ni sehemu ya kikosi kilichotumwa chini ya mwamvuli wa SADC kupambana na ugaidi katika mkoa wa kaskazini mwa Msumbiji wa Cabo Delgado.

Awali serikali kupitia waziri wa mambo ya nje Liberata Mulamula alisema kwamba Tanzania haitatuma wanajeshi Msumbiji na badala yake inasisitiza juu ya hitaji la mazungumzo kama njia ya kukuza amani na utulivu nchini Msumbiji.

Msemaji wa Jeshi la Wananchi Tanzania, JWTZ, Brigedia Jenerali Juma Sipe amethibitishia hili BBC akisema kuwa wakuu wa nchi za jumuiya ya maendeleo ya kusini mwa Afrika SADC walikwishaazimia kuwa nchi wanachama wa jumuiya hiyo watasaidia kutatua tatizo linaloendelea nchini Msumbiji.

‘’Makubaliano hayo moja kwa moja yanaihusu pia Tanzania, ikumbukwe Tanzania kwa kihistoria imeisaidia sana Jamhuri ya Msumbiji katika mapambano yake ya kupata uhuru wake na hata baada ya uhuru, pia Tanzania imeshiriki katika harakati nyingi zimesaidia sana kutatua mgogoro uliokuwepo kati ya FRELIMO na RENAMO kwa hivyo tatizo la Msumbiji kwa sasa ni tatizo la kikanda na kimsingi kama Watanzania tuna wajibu wa kushirikiana na wanajumuiya ya SADC katika kutatua tatizo hili.’’ Alisema Brigedia Jenerali Sipe.

Haijabainishwa ni wanajeshi wangapi kutoka Tanzania wanashiriki operesheni hiyo nchini Msumbiji, lakini Brigedia Jenerali Sipe amesema kuwa majeshi yote (nchi zinazoshiriki) yanayokwenda yanayokadiriwa kuwa Brigedi moja yanaratibiwa chini ya SADC kwa ujumla wake.

‘’Kila nchi mwanachama ana kiasi Fulani ambayo itapeleka, wengine watapeleka kwenye hospitali, wengine watakwenda vikundi maalum vya majukumu ya aina mbalimbali, jeshi la wana maji n.k. ‘’ Alifafanua Brigedia Jenerali .

Tanzania inapeleka wataalam gani wa kijeshi?

‘’Operesheni za kijeshi kwa kawaida huchukua vikundi vya aina zote kwa pamoja, vita si kama mechi ya mpira, bali operesheniwakati mnaendelea na mkakati hasa mkakati kama huu wa kupambana na vikundi visivyo rasmi kwa maana ya kwamba si majeshi, bali kikundi ambacho kina asili ya kigaidi kwahiyo wakati huohuo wapo wataalam ambao nao watahitajika ambao pia watasaidia kutathimini aina ya watu tunaokabiliana nao na namna bora ya kushauri ili vikundi vyetu viweze kufanya kazi vizuri zaidi''. Alisema Brigedia Jenerali Sipe.

Hatua hiiimeelezwa kuwa muhimu sana kwa uhusiano wa SADC na ukanda mzima kwa ujumla wake nanchi ya Msumbiji, vile vile usalama wa Msumbiji ni sawa na usalama wa nchi wanachama pia.

Operesheni hiyo ya miezi mitatu inahusisha wataalamu wa kijeshi na vifaa kutoka Afrika Kusini, Botswana, Angola, Tanzania, na Lesotho

Gharama ya awali ya operesheni hiyo ni dola milioni 12M.

Chanzo: BBC
 
Vikosi viliishaenda zamani tu,

Yaani unataka kuamini kwamba, nchi zote za Sadsc, ziliogopa kutuma vikosi mpaka Rwanda iende kwanza?

Pleaseee!! Vikosi vya sadc vipo msumbiji kwa muda mrefu, magaidi hao hawakuja jana, wapo tangu mwaka jana, sasa unafikiri nani alikuwa anaweka amani huko msumbiji?
 
Aisee Rwanda kiboko Magaidi imewabidi kukimbilia maporini hahahaa!!
Hivi unaaamini kabisa kwmaba,nchi zote za SADC ziliogopa kupereka wanajeshi,mpaka Rwanda aende kwanza?!!give us a bleak,don't be naive!

Vita ya huko ilianza kitambo sana, Rwanda ameenda hatua za mwisho? Ini mtu mwepesi anaweza kuamini kwamba vikosi vya Rwanda ni bora na imara kuriko vikosi vya South Afrika, na Tanzania ambao wanampaka na Msumbiji.

Vita ya ukombozi ya kusini mwa Afrika, JWTZ ilianza zamani, wakati huo majeshi ya makaburu yalikuwa yanapata msaada kutoka USA,na UK, tuliwachapa wale, sembuse Hawa islamists
 
Hivi unaaamini kabisa kwmaba,nchi zote za SADC ziliogopa kupereka wanajeshi,mpaka Rwanda aende kwanza?!!give us a bleak,don't be naive!

Vita ya huko ilianza kitambo sana, Rwanda ameenda hatua za mwisho? Ini mtu mwepesi anaweza kuamini kwamba vikosi vya Rwanda ni bora na imara kuriko vikosi vya South Afrika, na Tanzania ambao wanampaka na Msumbiji.

Vita ya ukombozi ya kusini mwa Afrika, JWTZ ilianza zamani, wakati huo majeshi ya makaburu yalikuwa yanapata msaada kutoka USA,na UK, tuliwachapa wale, sembuse Hawa islamists
Tulia kwanza uangalie dynamics
 
Hivi unaaamini kabisa kwmaba,nchi zote za SADC ziliogopa kupereka wanajeshi,mpaka Rwanda aende kwanza?!!give us a bleak,don't be naive!!!
Vita ya huko ilia
Kwa kusoma vyombo vya habari vya Kimataifa nimeelewa kuwa huo mgogoro ulikuwa unalihusha jeshi la Msumbiji na Mamluki waliokodishwa na Serikali ya Msumbiji na baadae Majeshi ya Rwanda sasa kama kuna ushahidi kuwa Majeshi yetu yalikuwa huko ni vizuri ukatuwekea ushahidi ili tuelewe.
 
Tanzania ni sehemu ya kikosi kilichotumwa chini ya mwamvuli wa SADC kupambana na ugaidi katika mkoa wa kaskazini mwa Msumbiji wa Cabo Delgado.

Awali serikali kupitia waziri wa mambo ya nje Liberata Mulamula alisema kwamba Tanzania haitatuma wanajeshi Msumbiji na badala yake inasisitiza juu ya hitaji la mazungumzo kama njia ya kukuza amani na utulivu nchini Msumbiji.

Msemaji wa Jeshi la Wananchi Tanzania, JWTZ, Brigedia JeneraliJuma Sipe amethibitishia hili BBC akisema kuwa wakuu wa nchi za jumuiya ya maendeleo ya kusini mwa Afrika SADC walikwishaazimia kuwa nchi wanachama wa jumuiya hiyo watasaidia kutatua tatizo linaloendelea nchini Msumbiji.

‘’Makubaliano hayo moja kwa moja yanaihusu pia Tanzania, ikumbukwe Tanzania kwa kihistoria imeisaidia sana Jamhuri ya Msumbiji katika mapambano yake ya kupata uhuru wake na hata baada ya uhuru, pia Tanzania imeshiriki katika harakati nyingi zimesaidia sana kutatua mgogoro uliokuwepo kati ya FRELIMO na RENAMO kwa hivyo tatizo la Msumbiji kwa sasa ni tatizo la kikanda na kimsingi kama Watanzania tuna wajibu wa kushirikiana na wanajumuiya ya SADC katika kutatua tatizo hili.’’ Alisema Brigedia Jenerali Sipe.

Haijabainishwa ni wanajeshi wangapi kutoka Tanzania wanashiriki operesheni hiyo nchini Msumbiji, lakini Brigedia Jenerali Sipe amesema kuwa majeshi yote (nchi zinazoshiriki) yanayokwenda yanayokadiriwa kuwa Brigedi moja yanaratibiwa chini ya SADC kwa ujumla wake.

‘’Kila nchi mwanachama ana kiasi Fulani ambayo itapeleka, wengine watapeleka kwenye hospitali, wengine watakwenda vikundi maalum vya majukumu ya aina mbalimbali, jeshi la wana maji n.k. ‘’ Alifafanua Brigedia Jenerali .

Tanzania inapeleka wataalam gani wa kijeshi?

‘’ Operesheni za kijeshi kwa kawaida huchukua vikundi vya aina zote kwa pamoja, vita si kama mechi ya mpira, bali operesheniwakati mnaendelea na mkakati hasa mkakati kama huu wa kupambana na vikundi visivyo rasmi kwa maana ya kwamba si majeshi, bali kikundi ambacho kina asili ya kigaidi kwahiyo wakati huohuo wapo wataalam ambao nao watahitajika ambao pia watasaidia kutathimini aina ya watu tunaokabiliana nao na namna bora ya kushauri ili vikundi vyetu viweze kufanya kazi vizuri zaidi''. Alisema Brigedia Jenerali Sipe.

Hatua hiiimeelezwa kuwa muhimu sana kwa uhusiano wa SADC na ukanda mzima kwa ujumla wake nanchi ya Msumbiji, vile vile usalama wa Msumbiji ni sawa na usalama wa nchi wanachama pia.

Operesheni hiyo ya miezi mitatu inahusisha wataalamu wa kijeshi na vifaa kutoka Afrika Kusini, Botswana, Angola, Tanzania, na Lesotho

Gharama ya awali ya operesheni hiyo ni dola milioni 12M.

Chanzo: BBC
Finally Tanzania has entered the Capitalist Geopolitical warfares in Cabo delgado.

Sadly, After Cabo Delgado mtwara is another targeted zone because of Gas
 
Rwanda wanajinasibu kuimaliza hii vita. Pia haijulikani kwa nini Rwanda ilikimbilia huko wakati SADC wakijiandaa kwenda kusaidia. Yasije yakatokea yale ya DRC ambapo Rwanda walichabangana na Uganda!

Walikimbilia au Rais Nyusi aliwakimbilia kuomba msaada?Sadc tangu 2017 mpk leo wanaweka vikao tu wakimaliza wanafanya strategic planning wakimaliza hapo unawasikia wanasema tunafanya security analysis then kinafuata Security protocal yaani ni kupoteza muda tu.
 
Hivi unaaamini kabisa kwmaba,nchi zote za SADC ziliogopa kupereka wanajeshi,mpaka Rwanda aende kwanza?!!give us a bleak,don't be naive!!!
Vita ya huko ilianza kitambo sana,Rwanda ameenda hatua za mwisho?!ni mtu mwepesi anaweza kuamini kwamba vikosi vya Rwanda ni bora na imara kuriko vikosi vya South Afrika,na Tanzania ambao wanampaka na Msumbiji.
Vita ya ukombozi ya kusini mwa afrika,JWTZ ilianza zamani,wakati huo majeshi ya makaburu yalikuwa yanapata msaada kutoka USA,na UK,tuliwachapa wale,sembuse Hawa islamists
Unafananisha kizazi cha wakurya na hawa madogo mtori mtori😅
 
Back
Top Bottom