Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,885
- 2,766
Ila zaidi ya redio hakuna majukwaa mengine ambapo unaweza kutembelea na kupata taarifa za kimichezo (hasa soka) kwa wakati na za kutosheleza.
Nakumbuka enzi hizo alianza Dr Leakey tukimsikiliza kipindi cha kombe la dunia - 1994 to 1998. Kipindi hicho ni yeye alitamba kwenye uchambuzoi wa soka tena la kimataifa kwa majina ya wachezaji, mchezo wenyewe, historia zao pamoja na masihara kibao. Alivuma sana. Miaka ya 2002 ndio wakaibuka kina Haji Manara na wengine na baada ya hapo yakatokea mafuriko ya wachambuzi wa soka la kitaifa na kimataifa. Leo hadi asubuhi unasikia kuna vipindi vya uchambuzi wa michezo redioni.
Ilitakiwa sambamba na hilo la mafuriko ya wachambuzi pangekuwepo na majukwaa mengine hasa ukichukulia kuna social media kwa sasa. Huwezi kupata taarifa za kimichezo kwa wakati na usahihi katika jukwaa moja na ukaridhika. Si Yanga, si Simba, wala si NBC Premier League wenye taarifa za kuridhisha za kimichezo. Hapo tumekwama sana.
Kupata tu taarifa za mchezo wa Yanga kesho Jumapili hadi uanze kuvizia redio. Hii ni challenge kwa wapenda michezo na wadau wa burudani kufanyia kazi. Wenzetu nje wako very active. Tazama EPL, Bundesliga, Serie a, La Liga, etc
Sijui hawa vijana wanakwama wapo wakati ukiwasikiliza ni kama wana taarifa zote vichwani mwao. SImu wanazo, intaneti wanayo (tena 4G, 5G), laptop wanazo. Wanafahamiana na developers kwa ajili ya kuwatengenezea aidha app nzuri au tovuti ambazo kazi yao ni ku update tu taarifa kama zinavyowafikia. Hili nalo hawaliwezi. Wanachotaka ni kuchukua taarifa kwa kudonoa toka mitandaoni na kukaa redioni kudadavua. Tunahitaji Sports Hub
Nakumbuka enzi hizo alianza Dr Leakey tukimsikiliza kipindi cha kombe la dunia - 1994 to 1998. Kipindi hicho ni yeye alitamba kwenye uchambuzoi wa soka tena la kimataifa kwa majina ya wachezaji, mchezo wenyewe, historia zao pamoja na masihara kibao. Alivuma sana. Miaka ya 2002 ndio wakaibuka kina Haji Manara na wengine na baada ya hapo yakatokea mafuriko ya wachambuzi wa soka la kitaifa na kimataifa. Leo hadi asubuhi unasikia kuna vipindi vya uchambuzi wa michezo redioni.
Ilitakiwa sambamba na hilo la mafuriko ya wachambuzi pangekuwepo na majukwaa mengine hasa ukichukulia kuna social media kwa sasa. Huwezi kupata taarifa za kimichezo kwa wakati na usahihi katika jukwaa moja na ukaridhika. Si Yanga, si Simba, wala si NBC Premier League wenye taarifa za kuridhisha za kimichezo. Hapo tumekwama sana.
Kupata tu taarifa za mchezo wa Yanga kesho Jumapili hadi uanze kuvizia redio. Hii ni challenge kwa wapenda michezo na wadau wa burudani kufanyia kazi. Wenzetu nje wako very active. Tazama EPL, Bundesliga, Serie a, La Liga, etc
Sijui hawa vijana wanakwama wapo wakati ukiwasikiliza ni kama wana taarifa zote vichwani mwao. SImu wanazo, intaneti wanayo (tena 4G, 5G), laptop wanazo. Wanafahamiana na developers kwa ajili ya kuwatengenezea aidha app nzuri au tovuti ambazo kazi yao ni ku update tu taarifa kama zinavyowafikia. Hili nalo hawaliwezi. Wanachotaka ni kuchukua taarifa kwa kudonoa toka mitandaoni na kukaa redioni kudadavua. Tunahitaji Sports Hub