16 February 2026
Baraza la Dhahabu Duniani laashiria utayari wa kushirikiana na Tanzania kuimarisha sekta ya dhahabu - SADC
View: https://m.youtube.com/watch?v=W9De1WL7Rh8
Baraza la Dhahabu Duniani World Gold Council limeonyesha utayari wake wa kushirikiana na Tanzania kuimarisha sekta ya dhahabu, ikizingatia kuongeza thamani na kuboresha teknolojia ya uchimbaji mdogo wa madini, ikilinganisha mpango huo na juhudi za Tanzania za kuongeza usafishaji wa ndani.
Tangazo hilo lilitolewa Dar Es Salaam na Afisa Mkuu Mtendaji wa WGC, David Tait, kufuatia mashauriano ya kiwango cha juu na mawaziri wa sekta mama wa serikali waliopewa jukumu la kukuza ukuaji wa tasnia ya dhahabu nchini.
Prof. Kitila Mkumbo waziri wa uwekezaji amesema kuwa wanaandaa kubainisha maeneo yenye dhahabu na kutayarisha ramani ikionesha maeneo yepi dhahabu hupatikana ili kurahishisha uwekezaji mdogo na mkubwa kufanyika kwa uhakika
Naye waziri wa madini David Mavunde amesema kwa kutumia satelaiti wataweza kupata takwimu sahihi za maeneo ya dhahabu nchini hivyo kuimarisha uhakika wa kiasi cha dhahabu iliyopo
Hadi sasa serikali ya Tanzania imeweza kutayarisha ramani inayogusa asilimia 15% pekee, WGC itaisaidia Tanzania walau kufikia 50% ya maeneo kiramani lengo lililo ktk Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2050
Baraza la Dhahabu Duniani laashiria utayari wa kushirikiana na Tanzania kuimarisha sekta ya dhahabu - SADC
View: https://m.youtube.com/watch?v=W9De1WL7Rh8
Baraza la Dhahabu Duniani World Gold Council limeonyesha utayari wake wa kushirikiana na Tanzania kuimarisha sekta ya dhahabu, ikizingatia kuongeza thamani na kuboresha teknolojia ya uchimbaji mdogo wa madini, ikilinganisha mpango huo na juhudi za Tanzania za kuongeza usafishaji wa ndani.
Tangazo hilo lilitolewa Dar Es Salaam na Afisa Mkuu Mtendaji wa WGC, David Tait, kufuatia mashauriano ya kiwango cha juu na mawaziri wa sekta mama wa serikali waliopewa jukumu la kukuza ukuaji wa tasnia ya dhahabu nchini.
Prof. Kitila Mkumbo waziri wa uwekezaji amesema kuwa wanaandaa kubainisha maeneo yenye dhahabu na kutayarisha ramani ikionesha maeneo yepi dhahabu hupatikana ili kurahishisha uwekezaji mdogo na mkubwa kufanyika kwa uhakika
Naye waziri wa madini David Mavunde amesema kwa kutumia satelaiti wataweza kupata takwimu sahihi za maeneo ya dhahabu nchini hivyo kuimarisha uhakika wa kiasi cha dhahabu iliyopo
Hadi sasa serikali ya Tanzania imeweza kutayarisha ramani inayogusa asilimia 15% pekee, WGC itaisaidia Tanzania walau kufikia 50% ya maeneo kiramani lengo lililo ktk Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2050