Stupidd..!Anaandika Bob T. Kola Kada wa CCM
TETESI; Tanzania inaweza kujikuta kwenye hali mbaya muda si mrefu. Ni wazi kuwa wakubwa wanajua ila wanatuficha ukweli. kubadilishwa kwa Waziri wa Nje ndio ishara namba moja. Kabudi atakabidhiwa jukumu la kutuliza mambo ambayo hayatuliziki. Kiuzalendo itatupasa tuache uvyama na tuungane kutaka suluhu.
Na kuhusu suala la Lissu, tumuombee Chief amuombe huyu Bwana radhi. Kuropoka kwa akina Lugola na wenzake kumetengeneza ushahidi mzito. Kifupi Moto wa Lissu ni hatari maana hata Ratiba zake mbili zilizoko mbele yake hivi sasa sio nzuri kwetu.
Kabudi amewekwa ajaribu kutumia Cheti chake cha Sheria na uzoefu ili kuziba balaa, namtakia mema lakini ni Kazi bure kama hawajamhusisha Tundu Lissu. Hizo ziara mbili zijazo zitaleta mtikisiko usio wa kawaida. Kumbukeni ICC inamtaka, Bunge la USA linamtaka, hizo ni hasi na chanya, moto wake ni mkubwa.
Ukiacha hayo, Tanzania ina Kesi kibao za Makampuni kuhusu Madai tofauti. Kesi zote hizi ukizitazama, ni za kukurupuka tu.
Kinachofanyika Nchini hivi sasa ni Matangazo ya Maigizo tu. Ukitazama Biashara, Kilimo na Masoko vimetupwa. Hata Magazeti nayo kila Siku yanaripoti habari za Wahamaji wa Vyama vya Kisiasa, sasa tutaishi vipi? Hakuna sehemu inayoandikwa zao Bora kwa Kilimo wala hakuna habari inayohusu Ufugaji, tumwambieni Mkuu abadilishe Santuri, vinginevyo mtakuja kukumbuka maneno yangu.
Kukimbilia kulinganisha Tanzania na Libya haisaidii kitu. Kusema mbona na Nyumba ya jirani ilichomwa kwa Moto ni ujinga, unachotakiwa kufanya ni kuzuia ya kwako isichomwe pia. Utetezi wa kusema mbona Kibiti walikufa wengi ni Ufala wa Africa tu. Huwezi kutumia ajali ya Bus kuhalalisha ajali ya Pikipiki.
Huwezi kusimama Mahakama ya The Hague ukawaambia eti na Rufiji walikufa wengi tu, huko watakuzaba Makofi, bado Wanasheria wetu wehu wehu tu hata ngeli ni zero kwao. Wamezoeshwa kupigishiwa Simu kwa Majaji ili kutoa Ushindi.
The Hague kuna Majaji wenye harufu mbaya, akikuangalia tu unasahau hata Jinsia yako, muulizeni huyo Uhuru Kenyaa. Msidhani kushughulikia Amani kule kwake na kupatana na Wapinzani anapenda, aliuona Moto wake na alikonda.
Bob T. Kola