Tanzania has started to build its own helicopters

Aliyesema hayo ya DIT baadaye alihamia Arusha na ndiye aliyesema hayo ya chopa kwa njia ya ujanjaujanja. Huyu jamaa ni tatizo la Taifa, anapenda sana kucheza na akili za wanasiasa na anachukua taaluma kama jambo la kisiasa-siasa tu.

Mtu huyu hathamini taaluma lakini leo anaiambia Tanzania na Dunia kwamba atatumia taaluma kufanya mambo makubwa kama kutengeneza/kuunda chopa! Mtu huyu anatumia njia za mkato kutengeneza mitaala ya chuo lakini tafakari kwamba mtu huyo huyo anasema atatumia taaluma wakati hafuati matakwa/misingi ya kitaaluma!

Kwa upande mwingine, Serikali imekuwa ikitenga pesa kwa ajili ya wanataaluma wa chuo kwenda viwandani kukagua maendeleo ya wanafunzi ikiwa ni pamoja na kuona na kubadilishana mawazo na wataalamu wa viwanda kwa muda wa siku 15. Lakini mtu huyu alivyo wa ajabu amekuwa akifikiri wanataaluma wakisafiri kwenda viwandani ni anasa.

Nia ya Serikali kupeleka wanataaluma viwandani kukagua wanafunzi pamoja na mambo mengine ni kuona viwanda vina nini kipya au vijana wetu wanapwaya au wako vizuri katika maeneo gani ili kuweza kuboresha zaidi taaluma inayotolewa na chuo.

Tofauti yake Mtu huyu huyu anayeongopea Taifa na Dunia kwamba atatengeneza chopa anafikiri kwamba wanataaluma watapata pesa au maarifa kama akiwapa per diem ya siku 15. Ndani yake mtu huyu hataki wanataaluma wa chuo wapate pesa wala maarifa na hivyo anawalipa wanataaluma wa chuo siku tano tu, hapo watajifunza kitu gani cha maana kwa muda huo? Je unadhani mtu wa aina hiyo anaweza kufanya watu kutengeneza chopa?

Kwa ufupi, hicho kinachosemwa kwamba kuna jambo la utengenezaji wa chopa chuoni hakipo. Ili kushuhudia kwamba jambo hili halipo, watu wafike na kufanya uchunguzi wa kina kama kuna jambo hilo. Hakuna kitu hicho, huo ni uongo kabisa.
Duh, unanifumbua zaidi..
Kumbe ni yuleyule !
 
Wewe sio mhandisi, huwezi nipa uhakikisho.

Jameni, ndo motisha unayopeana kwa vizazi vya keaho hili??? Tambua kuwa the Wright brothers wa Marekani walichekwa hadi na kuitwa wenda wazimu. Leo hii, ukitizama jinsi teknolojia,biashara na vyote kuhusu aviation imenawiri tukiweka 1902 kama base year, utashangaa. Naona ubakie tu pale karne ya 19 na kwenda nyuma.
Binafsi ningewasihi wabunifu na wanasayansi kwa ujumla waepuke na watu kama wewe.

Iweje leo Mtanzania aanza kufikiria teknolojia ya kupaa na chopa wakati barabara ya lami ya kwenda kijijini hakuna? Isitoshe, what's the point of reinventing the wheel? Tutegemee nini kipya kiteknolojia, design etc kwenye hiyo chopa ambacho Wamarekani, Warusi, Wafaransa, Wachina etc hawajafanya hadi leo? Au ni mambo ya poor but very expensive "copy and paste work"?
 
Raia nchini Tanzania wameamkia habari za kushangaza kwamba taifa hilo linatengeza ndege .

Gazeti la Tanzania la Daily News limeripoti kwamba ndege hiyo aina ya helikopta inakaribia kukamilika na kwamba habari hiyo imekuwa ikisambaa barani Afrika kwa kasi .
Gazeti la Zambia,Observer linasema kuwa lengo la ndege hiyo itayokuwa ikibeba watu kwa bei rahisi itakabiliana na matatizo ya uchukuzi nchini humo.

Huku gazeti la Cameron, Concord likisema kuwa mradi huo ni wa kihistoria linaongezea kuwa lengo lake ni kutengeza ndege 20 kwa mwaka.

Ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba watu wawili inakaribia kukamilika katika chuo cha ufundi cha Teknolojia cha Arusha na itaanza kufanyiwa majaribio ya kuruka angani baada ya kuruhusiwa na mamlaka ya uchukuzi wa angani nchini Tanzania kulingana na Daily News.
 
Hii mimi kuamini hadi niende chuoni nione kwa macho wanavyotengeneza, na vifaa wanavyotumia kutengenezea ndo takua na imani.
 
Safi na hongereni sana wahandisi wetu najua kazi ngumu sana bila suport yeyote toka popoteb ni moyo wa kujitoalea na kujiongeza!
 
Go Tanzania, naamini unaweza,nchi zetu za E.Africa, kenya, Uganda, Tanzania&Rwanda,zikishirikiana katika nyanjz za teknolojia,tutafka mbali.Uganda wanatengeza gari Sina KIIRA EV,Tanzania , chopper, nasubiri kuona ndugu zetu wakenya na Rwanda watakuja na kipi,naamini watatengeneza vizuri sana. Tunawaombea
 
Kama ni kweli, Mungu awabariki sana. Urushaji wa moja tu, unabadili mitazamo ya watu wengi hata mifumo yetu ya Elimu
 
TANZANIA has started to build its own helicopters in a project that will see the first batch of such choppers taking into the sky sometimes in 2018.
54d107ab3314b1f7a831fa7e509dd847.jpg


Already, the prototype model, a two-seater aircraft is in its final stages of completion at the Mechanical and Engineering Department of the Arusha Technical College, which runs a fully-fledged factory producing various forms of machinery, including a prototype motor vehicle and a number of industrial engines.

But it is the Tanzanian-made new helicopter that seems to be turning heads here; “We are complementing President Magufuli’s industrialisation policy in pioneering the first locally made helicopters that will be available to ordinary residents at affordable prices,” explained the man behind the ATC chopper project, Engineer Abdi Mjema.

The Permanent Secretary in the Ministry of Education, Science and Technology, Ms Maimuna Tarishi, who also toured the project over the weekend seemed surprised at the development and wanted to know when exactly the chopper will hit the skies.

“We are contacting the Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA) for the permission to fly the chopper for trials,” said Engineer Mjema.

He assured the PS that the future of the ‘affordable,’ chopper -- to ease the country’s transport woes -- is approaching. “The Tanzania-made helicopters will fly before 2020 -- and specifically 2018, which is two years from now,” he added.

The idea was hatched two months ago by two engineers at the Arusha Technical College; Engineer Adisai Msongole, now serving as the ATC Bursar, and Engineer Abdi Mjema. The chassis as well as airframe for the pioneer chopper is ready -- complete with a mounted flat engine.

“We had initially intended the two-seater helicopter to be used for surveillance, rescue and agricultural purposes. However, as the project takes shape, we may increase the airframes to carry more people for serious transportation,” said the engineer.

The helicopter is currently 50 per cent complete and features the popular gasolinepowered VW flat engine on board. The motors, manufactured by Volkswagen in Germany, are the same used to make the ‘Robinson’ helicopters in the United States. “Once we get the aviation authority approval, we shall complete the most sensitive part of the helicopter -- mounting the main rotor.

This should be ready in threeweek’s time,” said Eng Mjema, adding that Arusha will set history as the first region to fly the first-ever Tanzanian manufactured helicopter in July 2016. With a non-pressurised cabin, the Prototype ATC helicopter has a flying ceiling of 400 feet for starters, taking into consideration that Arusha is already at a higher altitude.

But the flying height is set to increase with more complete and accomplished models. Most commercial choppers can fly up to 8,000 feet above sea level. On how many choppers the college can manufacture in a year once the project gets a nod from higher authorities, Eng Mjema said that depended on demand.

“But with serious work we can roll out up to 20 such helicopters in a year,” boasted the engineer.

The Rector of Arusha Technical College, Dr Richard Masika, had previously stated that, ATC was moving from being an ordinary college of technical, engineering and technological training towards becoming a fully-fledged factory, which will deal in vehicle and heavy machinery repair and manufacturing.

Next August ATC will be completing the first phase of Kikuletwa Hydropower Station Project and training centre setup, through which the college is going to churn electricity and hold training at the site based in Kilimanjaro Region.

Source: Choppers - Made in Tanzania
wanatengeneza au wana assemble? Kwa vyovyote itakuwa jeneza la angani
 
Raia nchini Tanzania wameamkia habari za kushangaza kwamba taifa hilo linatengeza ndege .

Gazeti la Tanzania la Daily News limeripoti kwamba ndege hiyo aina ya helikopta inakaribia kukamilika na kwamba habari hiyo imekuwa ikisambaa barani Afrika kwa kasi .
Gazeti la Zambia,Observer linasema kuwa lengo la ndege hiyo itayokuwa ikibeba watu kwa bei rahisi itakabiliana na matatizo ya uchukuzi nchini humo.

Huku gazeti la Cameron, Concord likisema kuwa mradi huo ni wa kihistoria linaongezea kuwa lengo lake ni kutengeza ndege 20 kwa mwaka.

Ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba watu wawili inakaribia kukamilika katika chuo cha ufundi cha Teknolojia cha Arusha na itaanza kufanyiwa majaribio ya kuruka angani baada ya kuruhusiwa na mamlaka ya uchukuzi wa angani nchini Tanzania kulingana na Daily News.
Hii ni habari ya kupika iliyotolewa na chuo kwa lengo la kutaka kutenda uhalifu wa kifisadi. Habari hii imeleta taharuki kubwa Duniani na kama hatua za haraka za kukanusha hazitachukuliwa, Dunia itaishangaa Tanzania kwa kuwa habari hizi siyo za kweli.

Habari hizi zimeandikwa na kutangazwa na chuo huku menejimenti ya chuo ikiwa na tuhuma lukuki za ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka. Aidha tuhuma zingine nzito zinamhusu Mkuu wa chuo hicho kuwa na tabia ya kudanganya mamlaka za juu ikiwemo Bunge na Wizara ya Elimu.
 
Kheee. ....hii sera imepitishwa lini tena??

toka uti wa mgongo kilimo hadi kwy helkopta??! .

tafadhari sana jamani hiyo siku ya majaribio naomba mkae mbali na hapo chini mtandike magodoro, mambo ya kumsingizia Mungu eti ni mipango yake hapana aisee....tujiandae mapema kabisaa
 
Power tiller au tractor zingeweza kusaidia wananchi kama chuo kina uwezo wa ubunifu wa kiasi hicho. Kama hata maboresho ya turbine ya kufua umeme iliyoachwa na wataalamu wa UDSM ambayo ilidaiwa kwamba imetengenezwa na mafundi wa chuo cha Ufundi Arusha yalishindikana itakuwa chopa kweli?
 
Back
Top Bottom