Tanzania haina Mufti, Tanzania haina sheikh mkuu!

Chifu mkuu

JF-Expert Member
Jan 6, 2025
552
650
TANZANIA HAINA MUFTI !
TANZANIA HANA SHEKH MKUU!

Kwa muda mrefu tumekuwa tukisikia kiongozi mkuu wa taasisi ya kidini iitwayo Baraza kuu la waislamu wa Tanzania bara akitajwa kama mufti na sheikh mkuu wa Tanzania na mtazamo huu ni makosa makubwa sana na uamebeba maudhui ya upotoshaji kwa kumvika mtu cheo ambacho kiuhalisia hakipo na hakiwezekani kuwepo kwa sababu zifuatazo;

1️⃣ Unapozungumzia Tanzania ni pamoja na visiwa vya unguja na Pemba ambavyo vipo chini ya serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ndani ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa sababu kimataifa tunajulikana kama taifa moja tunaotumia sarafu moja na passport moja iliyoandikwa TANZANIA.
Zanzibar hawana passport maalumu kwa ajili yao kwakuwa wao ni watanzania na wanatumia Passport ya Tanzania.
Lakini pamoja na hayo upande wa maswala ya kidini taasisi za kiislamu za Tanzania bara hasa bakwata ni kama vile haziruhusuwi kuwa na office katika visiwa vya unguja na Pemba.!.
Waislamu wa Zanzibar wanaye mufti wao anayeteuliwa na mh Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi na yeye mufti na wasaidizi wake ambao baadhi yao huteuliwa na mh waziri wa katiba na sheria wa Zanzibar hufanya kazi chini ya wizara ya katiba na sheria ya Zanzibar .
Ofisi ya Mufti wa Zanzibar inafanya kazi chini ya serikali ya Zanzibar na BAKWATA hawana office katika visiwa vya unguja na pemba jambo linaloonyesha kwamba kama bakwata ingekuwa taasisi ya kisiasa tungesema BAKWATA sio katika mambo ya muungano kwakuwa majukumu ya bakwata ni upande wa Tanzania bara tu!
Sasa ikiwa hali iko hivyo BAKWATA wanajiitaje Baraza kuu la waislamu Tanzania wakati hawana ofisi upande wa Zanziba?!.
Na tunasemaje kiongozi mkuu wa BAKWATA ni mufti na sheikh mkuu wa Tanzania wakati hana wawakilishi wanaofanya kazi chini yake upande wa Zanzibar kama ilivyo katika mikoa , wilaya na kata za Tanzania bara?!

2️⃣ Sababu ya pili kwanini Tanzania haina Mufti wala sheikh mkuu ni kwakuwa serikali ya Tanzania imetoa uhuru wa kuabudu na imeruhusu uwepo wa taasisi nyingine za kiislamu kuanzishwa.!
Kupitia ruhusa hiyo na kwakuwa kuna baadhi ya waislamu ambao hawakubaliani na itikadi, fikra , sera na misimamo ya Bakwata wameanzisha taasisi nyingine za kiislamu na kuweka viongozi wanaowakubali ambao kulingana na katiba ya kila taasisi viongozi hao nafasi zao huwa na majina tafauti tafauti kama vile MUDIRU, AMIRI, MWENYEKITI, KATIBU MKUU NK na kimajukumu unakuta kila kiongozi mkuu ndani ya taasisi yake anafanya kazi sawa na zilezile anazozifanya sheikh mkuu wa BAKWATA na pia kila taasisi ya kiislamu inajitegemea katika kujiendesha bila kutegemea wala kuingilia mambo ya taasisi nyingine!
Ingekuwa Mufti wa BAKWATA ndiye msimamizi na kiongozi mkuu wa waislamu wote Tanzania serikali isingeruhusu kuanzishwa taasisi nyingine za kiislamu kufanya kazi zilezile zinazofanywa na BAKWATA kwasababu uwepo wa taasisi hizi kunasababisha migongano baina ya waislamu.
Ndio maana kila unapoingia na kumalizika mwezi wa Ramadhani utamsikia mufti wa BAKWATA akiwalalamikia watu wanaotangaza kuandama kwa mwezi wa kuingia Ramadhani au kumaliza Ramadhani kwa kuwa yeye Mufti anaamini kwamba ni shehe wa waislamu wote na kwamba haitakiwi mtu mwingine atangaze habari za kuingia au kumalizika Ramadhani kabla yake na AMEKUWA AKIICHOCHEA SERIKALI KUWACHUKILIA HATUA WATU WANAOTANGAZA MWEZI KABLA YAKE LAKINI SERIKALI IMEKUWA IKIMPUUZA KWAKUWA SIO KAZI YA SERIKALI KUINGILIA MAMBO YA IBADA ZA WATU KATIKA NCHI HII.
Kwahiyo yeye anatakiwa atambulike kama Mufti na sheikh mkuu wa BAKWATA na siyo sheikh wa Tanzania kwa sababu ndani ya nchi hii Kuna waislamu wengi ambao hawakubaliani na madhehebu, fikra na sera za bakwata na wana viongozi wao wanaowakubali kulingana na itikadi zao za kimadhehebu na wanazo taasisi ambazo serikali inazitambua.
 
Kwani una maslahi gani nayo Mkuu? Acha complication nyiiiingi labda useme unadeclare interest na ni ipi.. hapo nitakuelewa
 
Serikali huwatambua viongozi wa dini wenye watu wengi majority Tanzania kwenye kila dini

Kiongozi wa Bakwata ndie Mwenye waumini wengi waislamu Tanzania bara na Zanzibar kuliko hao wavaa vikobazi na visuruali vifupi na kufuga midevu kama osama bin laden
 
TANZANIA HAINA MUFTI !
TANZANIA HANA SHEKH MKUU!

Kwa muda mrefu tumekuwa tukisikia kiongozi mkuu wa taasisi ya kidini iitwayo Baraza kuu la waislamu wa Tanzania bara akitajwa kama mufti na sheikh mkuu wa Tanzania na mtazamo huu ni makosa makubwa sana na uamebeba maudhui ya upotoshaji kwa kumvika mtu cheo ambacho kiuhalisia hakipo na hakiwezekani kuwepo kwa sababu zifuatazo;

1️⃣ Unapozungumzia Tanzania ni pamoja na visiwa vya unguja na Pemba ambavyo vipo chini ya serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ndani ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa sababu kimataifa tunajulikana kama taifa moja tunaotumia sarafu moja na passport moja iliyoandikwa TANZANIA.
Zanzibar hawana passport maalumu kwa ajili yao kwakuwa wao ni watanzania na wanatumia Passport ya Tanzania.
Lakini pamoja na hayo upande wa maswala ya kidini taasisi za kiislamu za Tanzania bara hasa bakwata ni kama vile haziruhusuwi kuwa na office katika visiwa vya unguja na Pemba.!.
Waislamu wa Zanzibar wanaye mufti wao anayeteuliwa na mh Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi na yeye mufti na wasaidizi wake ambao baadhi yao huteuliwa na mh waziri wa katiba na sheria wa Zanzibar hufanya kazi chini ya wizara ya katiba na sheria ya Zanzibar .
Ofisi ya Mufti wa Zanzibar inafanya kazi chini ya serikali ya Zanzibar na BAKWATA hawana office katika visiwa vya unguja na pemba jambo linaloonyesha kwamba kama bakwata ingekuwa taasisi ya kisiasa tungesema BAKWATA sio katika mambo ya muungano kwakuwa majukumu ya bakwata ni upande wa Tanzania bara tu!
Sasa ikiwa hali iko hivyo BAKWATA wanajiitaje Baraza kuu la waislamu Tanzania wakati hawana ofisi upande wa Zanziba?!.
Na tunasemaje kiongozi mkuu wa BAKWATA ni mufti na sheikh mkuu wa Tanzania wakati hana wawakilishi wanaofanya kazi chini yake upande wa Zanzibar kama ilivyo katika mikoa , wilaya na kata za Tanzania bara?!

2️⃣ Sababu ya pili kwanini Tanzania haina Mufti wala sheikh mkuu ni kwakuwa serikali ya Tanzania imetoa uhuru wa kuabudu na imeruhusu uwepo wa taasisi nyingine za kiislamu kuanzishwa.!
Kupitia ruhusa hiyo na kwakuwa kuna baadhi ya waislamu ambao hawakubaliani na itikadi, fikra , sera na misimamo ya Bakwata wameanzisha taasisi nyingine za kiislamu na kuweka viongozi wanaowakubali ambao kulingana na katiba ya kila taasisi viongozi hao nafasi zao huwa na majina tafauti tafauti kama vile MUDIRU, AMIRI, MWENYEKITI, KATIBU MKUU NK na kimajukumu unakuta kila kiongozi mkuu ndani ya taasisi yake anafanya kazi sawa na zilezile anazozifanya sheikh mkuu wa BAKWATA na pia kila taasisi ya kiislamu inajitegemea katika kujiendesha bila kutegemea wala kuingilia mambo ya taasisi nyingine!
Ingekuwa Mufti wa BAKWATA ndiye msimamizi na kiongozi mkuu wa waislamu wote Tanzania serikali isingeruhusu kuanzishwa taasisi nyingine za kiislamu kufanya kazi zilezile zinazofanywa na BAKWATA kwasababu uwepo wa taasisi hizi kunasababisha migongano baina ya waislamu.
Ndio maana kila unapoingia na kumalizika mwezi wa Ramadhani utamsikia mufti wa BAKWATA akiwalalamikia watu wanaotangaza kuandama kwa mwezi wa kuingia Ramadhani au kumaliza Ramadhani kwa kuwa yeye Mufti anaamini kwamba ni shehe wa waislamu wote na kwamba haitakiwi mtu mwingine atangaze habari za kuingia au kumalizika Ramadhani kabla yake na AMEKUWA AKIICHOCHEA SERIKALI KUWACHUKILIA HATUA WATU WANAOTANGAZA MWEZI KABLA YAKE LAKINI SERIKALI IMEKUWA IKIMPUUZA KWAKUWA SIO KAZI YA SERIKALI KUINGILIA MAMBO YA IBADA ZA WATU KATIKA NCHI HII.
Kwahiyo yeye anatakiwa atambulike kama Mufti na sheikh mkuu wa BAKWATA na siyo sheikh wa Tanzania kwa sababu ndani ya nchi hii Kuna waislamu wengi ambao hawakubaliani na madhehebu, fikra na sera za bakwata na wana viongozi wao wanaowakubali kulingana na itikadi zao za kimadhehebu na wanazo taasisi ambazo serikali inazitambua.
Nimependa sana hoja zako mkuu,umejenga hoja vizuri sana.

Mimi naomba nikuulize kidogo ili nipate faida.

Tufanye hizo ni changamoto za kitaratibu ama mapungufu.

Lakini jee kitendo cha sheria kusema kwamba huyu ni mufti wa Tanzania unaona hiyo haitoshi kuwa yeye ni mufti wa Tanzania ?

Kama ambavyo tunaona kwamba logically sio watanzania wote wamwmchagua raisi aliyeko madarakani,je jmhiyo inafanya raisi wa madarakani asiwe raisi wa watu wote kwa kuwa tu logically ili uwe raisi wa wote basi ni lazima hao wote wakupigie kura ?
 
Hata Rais wa Tanzania hakuna maana Zanzibar wana Rais wao mwenye mamlaka kamili anateua baraza lake la mawaziri,anateua wakuu wa mikoa,wakuu wa wilaya,manispaa na jiji la Zanzibar wakurugenzi wake wanateuliwa na Rais wa Zanzibar pamoja na taasisi zote za serikali wakurugenzi wake wanateuliwa na Rais wa Zanzibar.
Huyu anayeitwa Rais wa Muungano hana mamlaka ya kumteua yeyote kule Zanzibar na kwa bahati mbaya hivi sasa Tanganyika inatawaliwa na Mzanzibar yaani Tanganyika kwa sasa ni koloni la Zanzibar.
 
Serikali huwatambua viongozi wa dini wenye watu wengi majority Tanzania kwenye kila dini

Kiongozi wa Bakwata ndie Mwenye waumini wengi waislamu Tanzania bara na Zanzibar kuliko hao wavaa vikobazi na visuruali vifupi na kufuga midevu kama osama bin laden
Wewe dogo siku tukikutana viwanja vya Zakhem nitakutoa utumbo ! Utakula mabanzi ya kutosha Ili uwe na adabu na wavaa kobazi. Waheed
 
Cheo hicho wapo watu wanakitaka wameona Rais tu hapana tunataka na Shekhe Mkuu atokee Zenji Bar
Mufti hachaguliwi na serikali waislamu wenyewe walio dhehebu kubwa ndani ya uislamu kuliko mengine ndio humchagua kwa kura
 
Serikali huwatambua viongozi wa dini wenye watu wengi majority Tanzania kwenye kila dini

Kiongozi wa Bakwata ndie Mwenye waumini wengi waislamu Tanzania bara na Zanzibar kuliko hao wavaa vikobazi na visuruali vifupi na kufuga midevu kama osama bin laden
Bakwata hawana muumini yeyote kule Zanzibar kule wana Mufti wao na wana kadhi wao.
Mufti wa Bakwata na kadhi wake wa mchongo kwa sababu hana "meno" na hukumu zake hazitambuliwi na chombo chochote cha serikali wao wanahudumu Tanganyika tu tena kinguvu maana waumini hatuwataki,hawapo pale kwa ajili ya kuwa chawa wa ccm tunawataka waachie hizo nafasi wakaungane na ma ccm wenzao pale lumumba wamuombee mgombea wao kura kutoka kwa majini.
 
Bakwata hawana muumini yeyote kule Zanzibar kule wana Mufti wao na wana kadhi wao.
Mufti wa Bakwata na kadhi wake wa mchongo kwa sababu hana "meno" na hukumu zake hazitambuliwi na chombo chochote cha serikali wao wanahudumu Tanganyika.
Hicho cheo cha Mufti hugombewa kama una usongo nacho nenda na wewe ukagombee uache porojo zako humu
 
Mufti hachaguliwi na serikali waislamu wenyewe walio dhehebu kubwa ndani ya uislamu kuliko mengine ndio humchagua kwa kura
Kwa hio sababu Rais mmeweza mkaona sasa Rais haitoshi tunataka Shekhe Mkuu wa Tanzania atokee Zenji Bar basi muombeeni afekwanza afu yule Shekhe makamu simjui atakua Mwanamke anatokea Zenji Bar ndio achukue uongozi wa Shekhe Mkuu wa Tanzania, na hapo unasemaje?
 
Nimependa sana hoja zako mkuu,umejenga hoja vizuri sana.

Mimi naomba nikuulize kidogo ili nipate faida.

Tufanye hizo ni changamoto za kitaratibu ama mapungufu.

Lakini jee kitendo cha sheria kusema kwamba huyu ni mufti wa Tanzania unaona hiyo haitoshi kuwa yeye ni mufti wa Tanzania ?

Kama ambavyo tunaona kwamba logically sio watanzania wote wamwmchagua raisi aliyeko madarakani,je jmhiyo inafanya raisi wa madarakani asiwe raisi wa watu wote kwa kuwa tu logically ili uwe raisi wa wote basi ni lazima hao wote wakupigie kura ?
Raisi atatambulika kikatiba hata kama hukumchagua au huungani na sera za chama chake.
Mtu ili awe rais Kuna mchakato wa kisheria kwa kachaguliwa na inadadi ya watu wanaozingatiwa kisheria, tume ya uchaguzi imemtangaza kuwa ni mshindi wa uchaguzi na mwisho kaapishwa kuwa rais wa jamhuri.
Upande wa mufti wa Zanzibar anatambulika na sheria ya Zanzibar kwa kuwa anateuliwa na rais wa Zanzibar.
Mufti wa bakwata hatambuliwi na sheria yoyote na kama wewe unatambua sheria inayomtambua mufti wa bakwata na mchakato wa kuchaguliwa au kuteuliwa kwake kisheria ukoje naomba uniwekee hapa ni sheria gani!
 
Kwa hio sababu Rais mmeweza mkaona sasa Rais haitoshi tunataka Shekhe Mkuu wa Tanzania atokee Zenji Bar basi muombeeni afekwanza afu yule Shekhe makamu simjui atakua Mwanamke anatokea Zenji Bar ndio achukue uongozi wa Shekhe Mkuu wa Tanzania, na hapo unasemaje?
Hayo myaongee misikitini kwenu huko
Sio kazi ya serikali kuteua sheikh mkuu wala Mufti
 
Back
Top Bottom